wa habari juu ya umiliki wa shirika la Uda ambalo kampuni yake ndiye mmiliki wake kwa sasa.Kisena alikuwa akijibu tuhuma zilizotolewa bungeni na baadhi ya wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam. Kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa kampuni hiyo, Patrick Mtani.PICHA: SELEMANI MPOCHIKampuni ya Simon Group imesema kwamba ni mmiliki wa Shirika la Usafirishaji Dar es Salaam (UDA) kwa asilimia 76 huku serikali ikimiliki hisa asilimia 23.Kampuni hiyo imesema ilinunua hisa za UDA kutokakwa waliokuwa wamiliki ambao ni Jiji la Dar es Salaam.Mkurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena, alizungumza na waandishi wa habari jana kufafanuakuhusu kauli ya Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, aliyoitoa bungeni Alhamisi iliyopita kuwa UDA ni mali ya serikali kupitia Msajili wa Hazina na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.Kisema alisema serikali inamiliki hisa zenye thamani ya Sh. 3,488,651 huku Simon Group ikimilikihisa zenye thamani ya Sh. 7,880,303.Nyingine ni hisa zenye thamani ya Sh. 3,631,046 kutoka Jiji la Dar es Salaam na kuwa thamani yan hisa zote ni Sh. 15,000,000.Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alihoji utaratibu uliotumika wakati wa uuzaji wa hisa zilizokuwa za UDA.Kisena alitoa uthibitisho huo kwa kutoa mikataba mbalimbali waliyo kubaliana kuanzia Kamati ya Kudumu ya Bunge ilipotembelea kampuni hiyo mwaka 2011 na kukubaliana pande zote mbili zichukue hatua kuhakikisha uwekezaji unawanufaisha wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kupata usafiri wa uhakika.Kisena alieleza kuwa inawezekana wabunge wanaohoji suala la UDA ni kukosa taarifa za uhakika kuhusiana na umiliki wa UDA.Aidha alisema Novemba15, 2011 walikaa na Msajili wa Hazina, Meya wa Jiji la Dar es Salaam na Mwanasheria wa Jiji kuzungumzia malalamiko yanayotolewa juu ya uwekezaji katika UDA na kubaini malalamiko yalikuwa ni Shirika kuuzwa kwa bei ndogo.¡°Tulikutana wote tukakubaliana kuunda bodi nami nikasema waseme bei yao nitalipa, mwisho tukakubaliana kwa pamoja tulipe kiasi cha Shilingi bilioni tano, ukiangalia hizi nyalaka utaona saini ya Meya Dk. Didas Masaburi, Robert Kisena na John Msella mwakilishi wa hazina,¡± alisema Kisena.Alisema baada ya makubaliano walikutana na kamati ya bunge na kila mwana hisa alipeleka taarifa yake kamati ikaagiza wakae pamoja wakubaliane kwa pamoja Agosti 16, 2013.Alisema walikutana tena wakiwamo wabunge wa Jiji la Dar es Salaam Agosti 22, 2013 wanahisa wakakubaliana kuuza hisa zao ili wakawekeze kwenye Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (DART) na kuwa Agosti 28, 2013 wanahisa pamoja na kamati ya jiji ikiongozwa na Mkuu wa mkoa walikubaliana kupeleka suala hili kwenye kamati ya bunge.¡°Tulipokubaliana tulikwenda Dodoma kukutana na kamati ya bunge tukiongozana na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadiki meya wa jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi wajumbe kutoka TRA, mimi mwenyewe pamoja na Mkurugenzi wa Jiji, Wilson Kabwe, na wabunge wote wa Dar es Salaam,¡± alisema.Alisema katika kikao cha mwisho walichokaa Dodoma kamati ilikubaliana na maamuzi yaliofikiwa na wanahisa kuachia kampuni ya Simon Group kuendesha shirika hilo.Alisema makubaliano hayo yalisainiwa na Dk. Masaburi; Msajili wa Wizara ya Fedha, Mwakibinga Mhelela na Robert Kisena, Mkurugenzi wa Simon Group.SOURCE: NIPASHE