heroone
Member
- Dec 15, 2011
- 24
- 3
Msingi wa sherehe na maonesho ya kilimo (nane nane) ulikuwa ni kutekeleza kwa vitendo falsafa ya Nyerere kuwa Tanzania ni nchi ya wakulima na wafanyakazi ndio maana akaanzisha siku hii maalum kwa heshima ya wakulima kama iliyo Mei mosi kwa wafanyakazi lengo ni kuwapa fursa wakulima kutoa kero na mawazo yao kwa serikal ili kujenga taifa moja lisilo na matabaka. Kwa sasa nchi si ya wakulima na wafanyakazi tena bali ni ya wafanya biashara na viongozi mafisadi na wauza madawa ya kulevya wachache. Wakulima hawathaminik tena, hawana masoko ya mazao yao, bei ni mbaya na miundombinu hafifu. Je kuna haja ya kuendelea na nane nane iliyogeuka ulaji, katka nchi hii ya wamwaga tindikali?