Namtafuta shemeji yangu JUMA IDDI

Namtafuta shemeji yangu JUMA IDDI

Aiseee hii heading imenistua sana, Nina mjomba angu ndo jina Lake hilo hilo na anawatoto mpaka wengine hawafahamu, tofauti ni kwamba yeye siyo mtu wa songea na wala hakuwahi kufanya Kazi huko...kama angekua kapita huko ningekutafuta pm.
labda hebu jaribu kumdadisi
 
Msomeshe mtoto huyo, acha nyimbo hizo, angeokota pochi ungemtafuta huyo shemeji yako?
 
Mkuu mpambanie mjomba wako asome mengine atafanya mwenyewe akikua na wakati huo wewe ukimiminikiwa na baraka kutoka mbinguni.
 
Huyo Bwana alizaa na dada yangu mwaka 2003, lakini wakati wanazaa huyo mtoto hawakuoana, yani kwa kiswahili cha sasa alizaa na dada yangu nje ya ndoa. Huyo Bwana walizaa huyo mtoto wakiwa Mlandizi, Pwani. Bwana alikuwa anafanya kazi eti Dawasco/ingawa naye hakuwa mkweli kwa dada yangu kwa miaka hiyo. Baada ya kuzaa na yule dada yangu ndani ya wiki 1 mtoto kuzaliwa akamtelekeza dada yangu akarudi kijijini/ Tanga tangu 24.08.2003 hadi sasa ni miaka 15 hatujui alipo. Yeye baada ya yule mtoto kuzaliwa alimpa jina tu la Ibrahim, baada ya hapo mpaka sasa kimyaaa. Mtoto saivi amefaulu STD VII anatakiwa ajiunge na form 1 - 2019 ni mtoto wa kiume. So popote pale alipo if is still alive anitafute mimi ni mjonba wa huyo mtoto.
Mlipieni tu Ada atawafaa baadae
 
Unachofanya ni jambo jema,ila si kazi rahisi sana kwako isipokuwa dada yako anaweza akawa na historia ya huyo bwana na hata ndugu wa karibu wa huyo jamaa yake....ni vema ungeanzia huko kwana,mwambie sister atoe info zinazoweza saidia ambazo hamzijui
Ni sawa Mr. Mkorinto nitamsomesha ila nimeona ngoja kwanza nijiridhishe kumtafuta if failed basi.
 
Wanaume wa Kiafrika baadhi yao kazi kupachika Mimba Na Kukimbia majukumu. Tabia mbaya kabisa hii.
Wadada muwe makini sana na sisi wanaume.
Pambana mkuu safari ya dogo kujitegemea ipo karibu. Mtoto wa kiume atakomaa na maisha mda si mrefu.
Hongera sana kwa kumkuza.
 
Huyo atakuwa siyo wa mtu wa Songea, watu wa Songea hawatelekezi watoto, in between msomeshe tu yajayo Mungu ndo anajua
 
Huwa kuna baba wa kambo wanasomesha watoto wa wake zao, ukiona huwezi kumsomesha, mshauri aolewe na huyo mume anaweza kusomesha mtoto wa mkewe, hoping one day atakuwa na uwezo huko mbele atasomesha wadogo zake.
Ungefanya markerting ya mama wa toto pia, kusema kama bado yuko single, au ni dada mwema, ni mzuri, and kazi au elimu fulani.
Hiyo inaweza kukusaidia kuutua huo mzigo in away by passing responsibilities kwa baba wa kambo a.k.a shemeji poa.
 
Mkuu somesha Civil Engineer huyo atakutunza baadae,mimi miliwahi kuwa kama mpwa wako huyohuyo ,uncle zangu walikomaa nami kiubishi
Civil form one?amuache mtoto achague kile anachopenda watu wamelazimishwa masomo wasioyataka mwisho wanajutia....amsomeshe kuwa nani ajichagulie yeye!
 
Ni sawa Mr. Mkorinto nitamsomesha ila nimeona ngoja kwanza nijiridhishe kumtafuta if failed basi.
Mimi nimekomaa na mpwangu sasa hivi Nina mjukuu ambae ameshajiunga na chuo Mtwara mwaka huu. Huyo amekimbia kwa makusudi atakusumbua huyo komaa nae mpwao hamna jinsi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom