Namna ya kuiandika Katiba mpya

Namna ya kuiandika Katiba mpya

winnerian

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2015
Posts
407
Reaction score
638
1. Lijengwe jukwaa la mtandao ambalo watanzania wengi wanaweza kujiandikisha kupitia nyaraka mbalimbali. Jukwaa hili litasaidia sana kukusanya mawazo ya watu wengi wenye uchu wa maendeleo na maboresho ya nchi yetu.

2. Tume/timu maalumu ya kukusanya maoni na kuyachambua yanafanana kukaa sehemu moja (cartegorization) iundwe kwa kufuata uadilifu wa mtu na uzalendo. Bahati mbaya hatujawa na idara ya kukusanya majina ya watanzania ambao ninwazalendo na kuyahifadhi yawe yanatumika pindi tunapohitaji hao watu.

3. Maoni yakatiba mpya yafanyiwe kazi na watanzania ambao sio wanasiasa na hawafungamani na siasa.

4. Kisha mapendekezo yote yaletwe kwa wananchi kupigiwa kura ya wazi kabisa.

5........

6........


7.......

8........
 
Rasimu ya warioba ipo tayari. Mambo mengine yooote yalikuwa sawa isipokuwa utata uliikuwa ni serikali ziwe mbili? au tatu? Basi kwa ujinga wa chadema wakakwamisha mchakato mzima.

Kwa hiyo pa kuanzia ni kupiga kura ya maoni kuwe na serikali mbili au tatu? Wala hatuhitaji tena kutumia muda na fedha nyingi.
 
1. Lijengwe jukwaa la mtandao ambalo watanzania wengi wanaweza kujiandikisha kupitia nyaraka mbalimbali. Jukwaa hili litasaidia sana kukusanya mawazo ya watu wengi wenye uchu wa maendeleo na maboresho ya nchi yetu.

2. Tume/timu maalumu ya kukusanya maoni na kuyachambua yanafanana kukaa sehemu moja (cartegorization) iundwe kwa kufuata uadilifu wa mtu na uzalendo. Bahati mbaya hatujawa na idara ya kukusanya majina ya watanzania ambao ninwazalendo na kuyahifadhi yawe yanatumika pindi tunapohitaji hao watu.

3. Maoni yakatiba mpya yafanyiwe kazi na watanzania ambao sio wanasiasa na hawafungamani na siasa.

4. Kisha mapendekezo yote yaletwe kwa wananchi kupigiwa kura ya wazi kabisa.

5........

6........


7.......

8........
Wewe unapoteza muda mwingi,
Nchi zilizoungana ni 2 ,kila nchi ilete mapendekezo yake katika lipi liwemo kwenye muungano.
Kisha kamati iundwe ili kumage mapendekezo na kutowa muongozo utakaoitwa Katiba.
Iwekwe nafasi kwa nchi nyingine ikipenda kuingia kwenye Muungano wetu.
Serikali ya Muungano iwe ndogo na yenye Majukumu maalumu.

Yaliyobakia Tanganyika iandike Katiba yake na Zanzibar yake ,
Zanziobar na Tanganyika ziwe ni shirikisho.
 
Kuandaa michakato kama ya Warioba ni upotevu wa Fedha na Muda kwa Jambo ambalo kimsingi CCM hawana nia ya kulifanikisha, bali wanatupotezea tuu.
 
Back
Top Bottom