Naiona Tanzania isiyo na Ugaidi na Ujambazi. CHADEMA waacheni polisi wafanye kazi zao

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Amani iwe kwenu wadau.

Kwa viki sasa, zimeripotiwa taarifa na jeshi la polisi zikieleza mafanikio yao katika mapambano dhidi ya Ujambazi na Ugaidi. Taarifa hizo zimetoa takwimu ya watu waliokamatwa na kuuawa katika operesheni ya kupambana na Ugaidi na ujambazo. Idadi ya waliokamatwa kwenye operesheni hiyo kwa mujibu wa polisi ni kubwa na wote waliokamatwa wamekutwa na vitu kadhaa ikiwa ni pamoja na silaha za kivita.

Aidha, kwa siku ya juzi na jana, zimeripotiwa taarifa kuwa magaidi na majambazi watano wameuawa Dar es Salaam na Tanga. taarifa hizo zinasema kuwa watatu wameuawa kwenye mapango ya Tanga ambako walijificha wale waliochinja ndugu zetu huko Tanga. Polisi ilifanikiwa kuwaua watu hao baada ya majibizano ya risasi kwa muda wa masaa matano.

Wiki mbili zilizopita, magaidi watatu waliohusika kuchinja watu Msikitini huko Mwanza nao wameuawa ikiwa ni pamoja na mtu anayesadikiwa kuwa ni kiongozi wao. Nachukua fursa hii kulipongeza jeshi letu la polisi kwa mafanikio waliyofikia. Aidha, niwapongeze pia Watanzania wote wanaojitolea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambazo zinawasaidia katika harakati zao.

Niwaombe sana ndugu zangu wa CHADEMA. Waliache jeshi la polisi lifanye kazi yake. Kama walidhani kuwa jeshi la polisi ni kwa ajili ya CCM basi ifike wakati tuwapime akili zao maana inawezekana kabisa wana matatizo ya akili. Hawa waliouawa ni majambazi na magaidi. Polisi wamefanya kazi zao kwa weledi na ufanisi Mkubwa.

Tanzania bila ya Ugaidi na Ujambazi inawezekana. Naamini kuwa mpaka 2020, Tanzania tutakuwa hatuna matukio ya Ugaidi na Ujambazi kama ilivyo kwa majirani zetu wa Rwanda. Kama wao wameweza, sisi tutashindwaje? Ni vema kujifunza kutoka kwa waliofanikiwa.
 
Wasipojitokeza watetezi wao pia na wafahili wao wakijitoa tutafanikiwa mapema
 
Amani iwe kwenu wadau.

Kwa viki sasa, zimeripotiwa taarifa na jeshi la polisi zikieleza mafanikio yao katika mapambano dhidi ya Ujambazi na Ugaidi. Taarifa hizo zimetoa takwimu ya watu waliokamatwa na kuuawa katika operesheni ya kupambana na Ugaidi na ujambazo. Idadi ya waliokamatwa kwenye operesheni hiyo kwa mujibu wa polisi ni kubwa na wote waliokamatwa wamekutwa na vitu kadhaa ikiwa ni pamoja na silaha za kivita.

Aidha, kwa siku ya juzi na jana, zimeripotiwa taarifa kuwa magaidi na majambazi watano wameuawa Dar es Salaam na Tanga. taarifa hizo zinasema kuwa watatu wameuawa kwenye mapango ya Tanga ambako walijificha wale waliochinja ndugu zetu huko Tanga. Polisi ilifanikiwa kuwaua watu hao baada ya majibizano ya risasi kwa muda wa masaa matano.

Wiki mbili zilizopita, magaidi watatu waliohusika kuchinja watu Msikitini huko Mwanza nao wameuawa ikiwa ni pamoja na mtu anayesadikiwa kuwa ni kiongozi wao. Nachukua fursa hii kulipongeza jeshi letu la polisi kwa mafanikio waliyofikia. Aidha, niwapongeze pia Watanzania wote wanaojitolea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambazo zinawasaidia katika harakati zao.

Niwaombe sana ndugu zangu wa CHADEMA. Waliache jeshi la polisi lifanye kazi yake. Kama walidhani kuwa jeshi la polisi ni kwa ajili ya CCM basi ifike wakati tuwapime akili zao maana inawezekana kabisa wana matatizo ya akili. Hawa waliouawa ni majambazi na magaidi. Polisi wamefanya kazi zao kwa weledi na ufanisi Mkubwa.

Tanzania bila ya Ugaidi na Ujambazi inawezekana. Naamini kuwa mpaka 2020, Tanzania tutakuwa hatuna matukio ya Ugaidi na Ujambazi kama ilivyo kwa majirani zetu wa Rwanda. Kama wao wameweza, sisi tutashindwaje? Ni vema kujifunza kutoka kwa waliofanikiwa.


Sijawahi kumskia mkuu wa polisi akisema amepambana na magaidi katika nchi hii. Wanasema nchini hakuna ugaidi ni majambazi yanayotumia silaha za kivita.
Naomba usiharibu taswira ya nchi hii kuwa tayari magaidi wako na wanaoperate TZ!!!!!!!! Ni hatari kwa ustawi wa taifa letu.
 
Kwa hiyo CHADEMA ndiyo imekuwa ikakwamisha jeshi la polisi kutekeleza majukumu yake?!!!
Hebu ifike muda siasa uchwara na post za kujikomba kwa wakubwa kuwe na mipaka. Sote tunajua mfumo wa kiutendaji wa jeshi la polisi na udhaifu wake.
 
Sijawahi kumskia mkuu wa polisi akisema amepambana na magaidi katika nchi hii. Wanasema nchini hakuna ugaidi ni majambazi yanayotumia silaha za kivita.
Naomba usiharibu taswira ya nchi hii kuwa tayari magaidi wako na wanaoperate TZ!!!!!!!! Ni hatari kwa ustawi wa taifa letu.
Ahsante Mkuu kwa tahadhari yako. Ila kama mtu anachinja watu msikitini na kijijini hakuna tafsiri nyingine zaidi ya magaidi. Kani magaidi lengo lao ni kuleta hofu katika jamii na majambazi haja yao kubwa ni mali.
 
Kwa hiyo CHADEMA ndiyo imekuwa ikakwamisha jeshi la polisi kutekeleza majukumu yake?!!!
Hebu ifike muda siasa uchwara na post za kujikomba kwa wakubwa kuwe na mipaka. Sote tunajua mfumo wa kiutendaji wa jeshi la polisi na udhaifu wake.
Yeah! Nimesikia Clip ya Ole Sosopi akitangaza vita na jeshi la Polisi. Ndio maana nikafikia hatua ya kuwaasa CHADEMA waliache jeshi la polisi lifanye kazi zake
 
Sijawahi kumskia mkuu wa polisi akisema amepambana na magaidi katika nchi hii. Wanasema nchini hakuna ugaidi ni majambazi yanayotumia silaha za kivita.
Naomba usiharibu taswira ya nchi hii kuwa tayari magaidi wako na wanaoperate TZ!!!!!!!! Ni hatari kwa ustawi wa taifa letu.
Kweli mkuu huyu kanjanja Lizaboni anataka kuaminisha umma kuwa ugaidi upo ama ulishaanza kustawi hapa TZ, kitu ambacho yeye anafahamu hakuna ila ni kujipendekeza tu kwa jeshi la polisi na kujifanya kuwafundisha kazi.
 
Yeah! Nimesikia Clip ya Ole Sosopi akitangaza vita na jeshi la Polisi. Ndio maana nikafikia hatua ya kuwaasa CHADEMA waliache jeshi la polisi lifanye kazi zake
Kama yupo mtu/chama kinatangaza vita (sijui ya aina gani) dhidi ya jeshi la polisi basi utaratibu uchukue mkondo wake.
 
Ahsante Mkuu kwa tahadhari yako. Ila kama mtu anachinja watu msikitini na kijijini hakuna tafsiri nyingine zaidi ya magaidi. Kani magaidi lengo lao ni kuleta hofu katika jamii na majambazi haja yao kubwa ni mali.
Umewasiliana na IGP au JPM kwa uhakika wa tafsiri yako. Sitaki ununue matatizo maana uwepo wako jamvini una maana sana.
 
Back
Top Bottom