Naiona "imaginary line" iliyochorwa awamu hii kati ya wanasiasa na watumishi wa umma ikishika kasi

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,323
152,136
Watumishi wa umma na vyama vya wafanyakazi mnapaswa kuzinduka tunakoelekea sasa siko.

Wanasiasa sasa wameamua kujisafisha kupitia watumishi wa umma huku wao wakionekana kulindana na bahati mbaya sana watumishi wa umma wamelala usingizi wa pona huku wakiwa wamefunikwa na blanketi la hapa kazi tu linaowatia woga wasithubutu hata kuhoji juu ya haki zao.

Tujiulize hivi nchi hii wabadhirifu na wanaotumia vibaya madaraka ni watumishi wa umma tu?Hivi ni kweli wanasiasa wa nchi hii mpaka sasa hakuna aliestahili kuwajibika?

Hivi karibuni iliripotiwa kuwa wakurugenzi wanaotakiwa kwenda Dodoma kwenye maswala ya Bajeti watatakiwa kusafiri na gari la pamoja na asietaka aende na usafiri wake binafsi kwa gharama zake mwenyewe.

Cha kushangaza,mawaziri,manaibu mawaziri na vigogo wengine wanasafiri na mashangingi tena kila mtu na lake kutoka Dar hadi Dodoma.

Hivi kama hoja ni kubana matumizi,ni kwanini basi mawaziri hawa wasiende Dodoma na RAV4 au magari mengine yenye CC ndogo?

Ukweli ni kwamba,ukiwa Dodoma sasa hivi, wingi wa mashangingi haya hapa mjini unaondoa kabisa maana nzima ya kinachoitwa kubana matumizi kwani ni magari haya ya anasa ya serikali ndio yanatawala hapa mjini.

Leo hii Makonda kaja na mkataba unaotakiwa kusainiwa na maofisa utumishi wa Halamashauri za mkoa wa Dar-es-salaam kuhusiana na watumishi hewa.

Cha kujiuliza,hivi ni kwanini tusiwe na mikataba ya aina hii kwa wateule wa raisi wanapotuhumiwa wawajibike mara moja mfano mawaziri?Makonda nae ana mkataba maalumu wa aina hii kuhusu watumishi hewa na boss wake?

Hivi sasa kuna juhudi kubwa za kukabiliana na watumishi hewa (jambo jema kabisa).Lakini tujiulize, wabunge (wanasiasa) wana sheria inayowalazimisha kusaini mwanzo wa kikao na mwisho wa kikao kabla ya kulipwa posho zao za siku?

Naamini kadri siku zinavyokwenda huu mstari utajidhihirisha kwa wengi.
 
Watumishi wa umma na vyama vya wafanyakazi mnapaswa kuzinduka tunakoelekea sasa siko.

Wanasiasa sasa wameamua kujisafisha kupitia watumishi wa umma huku wao wakionekana kulindana na bahati mbaya sana watumishi wa umma wamelala usingizi wa pona huku wakiwa wamefunikwa na blanketi la hapa kazi tu linaowatia woga wasithubutu hata kuhoji juu ya haki zao.

Tujiulize hivi nchi hii wabadhirifu na wanaotumia vibaya madaraka ni watumishi wa umma tu?Hivi ni kweli wanasiasa wa nchi hii mpaka sasa hakuna aliestahili kuwajibika?

Hivi karibuni iliripotiwa kuwa wakurugenzi wanaotakiwa kwenda Dodoma kwenye maswala ya Bajeti watatakiwa kusafiri na gari la pamoja na asietaka aende na usafiri wake binafai kwa gharama zake mwenyewe.

Cha kushangaza,mawaziri,manaibu mawaziri na vigogo wengine wanasafiri na mashangingi tena kila mtu na lake kutoka Dar hadi Dodoma.

Hivi kama hoja ni kubana matumizi,ni kwanini basi mawaziri hawa wasiende Dodoma na RAV4 au magari mengine yenye CC ndogo?

Ukweli ni kwamba,ukiwa Dodoma sasa hivi, wingi wa mashangingi haya hapa mjini unaondoa kabisa maana nzima ya kinachoitwa kubana matumizi kwani ni magari haya ya anasa ya serikali ndio yanatawala hapa mjini.

Leo hii Makonda kaja na mkataba unaotakowa kusainiwa na maofisa utumishi wa Halamashauri za mkoa wa Dar-es-salaam kuhusiana na watumishi hewa.

Cha kujiuliza,hivi ni kwanini tusiwe na mikataba ya aina hii kwa wateule wa raisi wanapotuhumiwa wawajibike mara moja mfano mawaziri?

Hivi sasa kuna juhudi kubwa za kukabiliana na watumishi hewa (jambo jema kabisa).Lakini tujiulize, wabunge (wanasiasa) wana sheria inayowalazimisha kusaini mwanzo wa kikao na mwisho wa kikao kabla ya kulipwa posho zao za siku?

Naamini kadri siku zinavyokwenda huu mstari utajidhihirisha kwa wengi.
Salary Slip , A true great thinker .
 
Wanahani labda sijakuelewa au sijaelewa uhusiano wa kichwa cha habari na content iliyoko chini.
Umegusia jambo la makonda. Yeye kadili na wale anaokuwa na uwezo nao ( yaani wako chini yake ) na pia linahusu watumishi hewa.. Maana kuna maafisa utumishi wanavheza dili.
Jambo la wanasia JPM alishawasahinisha mkataba pia. Labda utekelezaji na uwajibikajinwake ndio hatujuwi inakuwaje.
Pamoja na hayo, jambo la mashangingi na gharama kubwa wanazozitumia wanasiasa, hivyo vgama vya siasa vina uwezo gani navyo... ?
All in all, kumbuka miaka iliyopita, mashangingi hayo yooote unayoyaona yalikuwapo, na bado wakurugenzi walikuwa wanaongeza gharama zaidi kwa kusafiri kwa gharama za secta zao ambazo huandikiana night, na pia magari yao yalikuwa yanagharamiwa na ofisi pia. Kwahiyo kimtindo, bado kuna upunguzaji kidogo wa matumizi ya ofisi za serikali. Ingawa bado matumizi yako kama ulivyoyaona mashangingi hayo huko dodoma.
Kumbuka wakuu wa mikoa na wakurugenzi wa halmashauri nao pia wamepigwa stop ya kwenda dodoma, kwani nao walikuwa wanaenda huko kwa gharama za ofisi...
Kwahiyo mie naona kwa post yako, sioni sehemu ambayo vyama vya wafanya kazi vinatakiwa viingilie kati... Au ulikuwa na maaana vyama viwatetee hao watumishi wa umma kama maafisa utumishi wanaopigwa chini au kusignishwa mikataba ya maadili?
Naomba nieleweshe mkuu wangu.... Smaahani lakini.....
 
Awamu ya Tano Wanasiasa(Mawaziri) Wamewajibishwa sana kwa makosa ya watendaji wa Serikali.. Kila zama na kitabu chake, nakumbuka ilifika kipindi JK alisema sasa inabidi na watendaji wawe katika uwajibikaji, sio Wanasiasa TU
 
Na kadri tunavyo zidi kwenda mbele nahisi kuna watu watalazwa chini na kuchapwa viboko,na kama haitoshi wananchi hawawatei tena watumishi kwani wameungana na wanasiasa wanao waaminisha kuwa umasiki wa nchi hii umeletwa na watumishi!na kwa kuwa wako wachache hao watumishi,wanasiasa hawaoni haya kuwatoa sadaka kwani wanajua kwanza hawapendwi na wananchi masikini,ambao wana waonea kijicho baadhi ya watumishi!wanasiasa wanacho fanya ni kuongeza petroli kwenye moto tu!
 
Wanasiasa hawashiki pesa ya serikali. Wao ni watazamaji tu (watch dogs) kwa niaba ya wananchi wanaowawakilisha. Wenye pesa ya serikali ni watendaji wa serikali wakiongozwa na maafisa masuhuli wao -- accounting officers. Waziri hawezi kufanya ufisadi wo wote kama afisa masuhuli ni muadilifu.
 
Na kadri tunavyo zidi kwenda mbele nahisi kuna watu watalazwa chini na kuchapwa viboko,na kama haitoshi wananchi hawawatei tena watumishi kwani wameungana na wanasiasa wanao waaminisha kuwa umasiki wa nchi hii umeletwa na watumishi!na kwa kuwa wako wachache hao watumishi,wanasiasa hawaoni haya kuwatoa sadaka kwani wanajua kwanza hawapendwi na wananchi masikini,ambao wana waonea kijicho baadhi ya watumishi!wanasiasa wanacho fanya ni kuongeza petroli kwenye moto tu!
Tungekuwa na watu wengi wanaona mambo kwa mtazamo huu, tusingeburuzwa na hawa wanasiasa kiasi hiki.
 
Nadhani unajifanya tu hujui how the government system operates. It is operated by the civil and millitary servants. The politicians on behalve of the people have the power to hire and fire(kuwatumbua) them.
Wenye madaraka ya kuwatumbua watumishi wa umma ni wanasiasa na wenye uwezo wa kuwatumbua wanasiasa siyo rais bali ni wananchi kupitia sanduku la kura.
 
Wanahani labda sijakuelewa au sijaelewa uhusiano wa kichwa cha habari na content iliyoko chini.
Umegusia jambo la makonda. Yeye kadili na wale anaokuwa na uwezo nao ( yaani wako chini yake ) na pia linahusu watumishi hewa.. Maana kuna maafisa utumishi wanavheza dili.
Jambo la wanasia JPM alishawasahinisha mkataba pia. Labda utekelezaji na uwajibikajinwake ndio hatujuwi inakuwaje.
Pamoja na hayo, jambo la mashangingi na gharama kubwa wanazozitumia wanasiasa, hivyo vgama vya siasa vina uwezo gani navyo... ?
All in all, kumbuka miaka iliyopita, mashangingi hayo yooote unayoyaona yalikuwapo, na bado wakurugenzi walikuwa wanaongeza gharama zaidi kwa kusafiri kwa gharama za secta zao ambazo huandikiana night, na pia magari yao yalikuwa yanagharamiwa na ofisi pia. Kwahiyo kimtindo, bado kuna upunguzaji kidogo wa matumizi ya ofisi za serikali. Ingawa bado matumizi yako kama ulivyoyaona mashangingi hayo huko dodoma.
Kumbuka wakuu wa mikoa na wakurugenzi wa halmashauri nao pia wamepigwa stop ya kwenda dodoma, kwani nao walikuwa wanaenda huko kwa gharama za ofisi...
Kwahiyo mie naona kwa post yako, sioni sehemu ambayo vyama vya wafanya kazi vinatakiwa viingilie kati... Au ulikuwa na maaana vyama viwatetee hao watumishi wa umma kama maafisa utumishi wanaopigwa chini au kusignishwa mikataba ya maadili?
Naomba nieleweshe mkuu wangu.... Smaahani lakini.....
Anachofanya Makonda ndicho kinachofanyika awamu hii kwa watumishi.

Hapa ni like father,like son.Kila mtu anatenda kwa nafasi yake lengo likuwa moja.

Jiongeze mkuu utaelewa tu.
 
Wanasiasa hawashiki pesa ya serikali. Wao ni watazamaji tu (watch dogs) kwa niaba ya wananchi wanaowawakilisha. Wenye pesa ya serikali ni watendaji wa serikali wakiongozwa na maafisa masuhuli wao -- accounting officers. Waziri hawezi kufanya ufisadi wo wote kama afisa masuhuli ni muadilifu.
Mawaziri aina ya kina Mramba awmu iliyopita hawakuwepo?
 
Wanasiasa hawashiki pesa ya serikali. Wao ni watazamaji tu (watch dogs) kwa niaba ya wananchi wanaowawakilisha. Wenye pesa ya serikali ni watendaji wa serikali wakiongozwa na maafisa masuhuli wao -- accounting officers. Waziri hawezi kufanya ufisadi wo wote kama afisa masuhuli ni muadilifu.
ila kumbuka dili zote za kifisadi,wanasiasa waliinfluence watumishi wapitishwe mikataba ya kifisadi!inakuwa uonevu kuwaona watunga sera mbovu wakiachwa uku watekelezaji wa hizo sera ndio wanao wajibishwa!
Nadhani unajifanya tu hujui how the government system operates. It is operated by the civil and millitary servants. The politicians on behalve of the people have the power to hire and fire(kuwatumbua) them.
Wenye madaraka ya kuwatumbua watumishi wa umma ni wanasiasa na wenye uwezo wa kuwatumbua wanasiasa siyo rais bali ni wananchi kupitia sanduku la kura.
asante,kwa elimu yako ya bure!naukubali uelewa wako ktk uendeshaji wa serikali za mitaa!
 
Wanasiasa hawashiki pesa ya serikali. Wao ni watazamaji tu (watch dogs) kwa niaba ya wananchi wanaowawakilisha. Wenye pesa ya serikali ni watendaji wa serikali wakiongozwa na maafisa masuhuli wao -- accounting officers. Waziri hawezi kufanya ufisadi wo wote kama afisa masuhuli ni muadilifu.



Kweli watumishi wamekosa ujasiri wa kusimamia maadili yao ya kazi na kuwapa ukweli hata kama waziri ni bosi wako akiwa anatoka nje ya mstari.

Lakini pia viongozi wa juu kabisa nao kuwa na kashfa ya ufisadi imeondoa uadilifu katika ngazi zote.
Labda awamu hii ambapo mtendaji anaweza kumshtaki waziri kwa raisi na akachukuliwa hatua.
Lakini sio kwa awamu zilizopita .
 
Watumishi wa umma na vyama vya wafanyakazi mnapaswa kuzinduka tunakoelekea sasa siko.

Wanasiasa sasa wameamua kujisafisha kupitia watumishi wa umma huku wao wakionekana kulindana na bahati mbaya sana watumishi wa umma wamelala usingizi wa pona huku wakiwa wamefunikwa na blanketi la hapa kazi tu linaowatia woga wasithubutu hata kuhoji juu ya haki zao.

Tujiulize hivi nchi hii wabadhirifu na wanaotumia vibaya madaraka ni watumishi wa umma tu?Hivi ni kweli wanasiasa wa nchi hii mpaka sasa hakuna aliestahili kuwajibika?

Hivi karibuni iliripotiwa kuwa wakurugenzi wanaotakiwa kwenda Dodoma kwenye maswala ya Bajeti watatakiwa kusafiri na gari la pamoja na asietaka aende na usafiri wake binafsi kwa gharama zake mwenyewe.

Cha kushangaza,mawaziri,manaibu mawaziri na vigogo wengine wanasafiri na mashangingi tena kila mtu na lake kutoka Dar hadi Dodoma.

Hivi kama hoja ni kubana matumizi,ni kwanini basi mawaziri hawa wasiende Dodoma na RAV4 au magari mengine yenye CC ndogo?

Ukweli ni kwamba,ukiwa Dodoma sasa hivi, wingi wa mashangingi haya hapa mjini unaondoa kabisa maana nzima ya kinachoitwa kubana matumizi kwani ni magari haya ya anasa ya serikali ndio yanatawala hapa mjini.

Leo hii Makonda kaja na mkataba unaotakiwa kusainiwa na maofisa utumishi wa Halamashauri za mkoa wa Dar-es-salaam kuhusiana na watumishi hewa.

Cha kujiuliza,hivi ni kwanini tusiwe na mikataba ya aina hii kwa wateule wa raisi wanapotuhumiwa wawajibike mara moja mfano mawaziri?Makonda nae ana mkataba maalumu wa aina hii kuhusu watumishi hewa na boss wake?

Hivi sasa kuna juhudi kubwa za kukabiliana na watumishi hewa (jambo jema kabisa).Lakini tujiulize, wabunge (wanasiasa) wana sheria inayowalazimisha kusaini mwanzo wa kikao na mwisho wa kikao kabla ya kulipwa posho zao za siku?

Naamini kadri siku zinavyokwenda huu mstari utajidhihirisha kwa wengi.
onduru ogy naomba usome hapa hasa hiyo mistari miwili ya mwisho kabisa.
 
Awamu ya Tano Wanasiasa(Mawaziri) Wamewajibishwa sana kwa makosa ya watendaji wa Serikali.. Kila zama na kitabu chake, nakumbuka ilifika kipindi JK alisema sasa inabidi na watendaji wawe katika uwajibikaji, sio Wanasiasa TU
Is that the reason why ministers should continue using those V8 ? Nyie batanzania have a long way to go
 
Back
Top Bottom