Nebuchadinezzer
JF-Expert Member
- Oct 1, 2018
- 1,403
- 2,545
Nianze kwa kusema vita dhidi ya Mabeberu sio vita lelemama, inahitaji vijana wa kike na wakiume walioiva na kujitoa kwa mioyo yao hata mauti ili kuipigania nchi yao.
Kushindana na watu wenye fedha (matajiri waliojaa utajiri wa udhalimu) sio kazi rahisi. Hayati JPM, kama mashujaa wengi waliopigania nchi zao tangu akiwa waziri, atakumbukwa milele hasahasa kwa watanzania maskini.
Sishangai baada ya kulala kwake, usingizi wa mauti, kuanza kuibuka kwa kashifa nyingi dhidi yake, kwani yeye sio shujaa wa kwanza kuandamwa na kivuli cha kinyume cha mambo aliyokuwa akiyafanya.
Leo mtu aliyejitoa kupigana na mafsadi; mtu aliyewakamata Seth na Rugemalila, kwa kuhusika na wizi wa Escrow ac. ataonekana alikurupuka, na watugumiwa wataachiwa huru na kuonekana ni washindi.
Kuzikwa kwa Magufuli kutazika mambo mengi sana. Waliokuwa wanakula nchi na maadui zetu wanaingia madarakani sasa.
Wachimbaji wadogo wadogo, jiandaeni kuachia maeneo mliyoyagundua muwaachie wawekezaji maana wao wanalipa kodi.
Nchi jiandaeni kupokea misaada yote iliyokuwa imezuiwa kuingia nchini. Zama zimebadilika sasa.
Muda utaongea...
NB: Sitaandika tena kwenye hili jukwaa.
Mods. naombaa huu uzi usifutwa ili uwe kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.
Ndimi mzalendo wa taifa langu.
King. Nebu.
Kushindana na watu wenye fedha (matajiri waliojaa utajiri wa udhalimu) sio kazi rahisi. Hayati JPM, kama mashujaa wengi waliopigania nchi zao tangu akiwa waziri, atakumbukwa milele hasahasa kwa watanzania maskini.
Sishangai baada ya kulala kwake, usingizi wa mauti, kuanza kuibuka kwa kashifa nyingi dhidi yake, kwani yeye sio shujaa wa kwanza kuandamwa na kivuli cha kinyume cha mambo aliyokuwa akiyafanya.
Leo mtu aliyejitoa kupigana na mafsadi; mtu aliyewakamata Seth na Rugemalila, kwa kuhusika na wizi wa Escrow ac. ataonekana alikurupuka, na watugumiwa wataachiwa huru na kuonekana ni washindi.
Kuzikwa kwa Magufuli kutazika mambo mengi sana. Waliokuwa wanakula nchi na maadui zetu wanaingia madarakani sasa.
Wachimbaji wadogo wadogo, jiandaeni kuachia maeneo mliyoyagundua muwaachie wawekezaji maana wao wanalipa kodi.
Nchi jiandaeni kupokea misaada yote iliyokuwa imezuiwa kuingia nchini. Zama zimebadilika sasa.
Muda utaongea...
NB: Sitaandika tena kwenye hili jukwaa.
Mods. naombaa huu uzi usifutwa ili uwe kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.
Ndimi mzalendo wa taifa langu.
King. Nebu.