Nahitaji pikipiki aina ya boxer kwa laki 8

Nahitaji pikipiki aina ya boxer kwa laki 8

Kwa uzoefu wangu mdogo,

Bei hiyo usijaribu wala kufikiria kununua Boxer,maana kwa bei hiyo laizma Engine itakuwa imeishafunguliwa. Boxers ni Imara sana na zinadum muda mrefu,lakini tambua kwamba Spare zake ni ghali sana.

Sasa kama imefunguliwa Engine basi jua unahamisha mtaji kwenda kwenye pikipiki,utanunua spare kila siku unless ubadilishe Engine. Ni mtizamo wangu tu,ila kama unaweza bei hiyo utapa Mchina alie kwenye hali nafuu kidogo ila kwa Boxer ni ile ambayo ipo ICU.
 
...una maanisha kwa bei hiyo nitapata hizi san lg, fekon etc?
Je boxer nitapata kwa sh ngap angalau??
 
...una maanisha kwa bei hiyo nitapata hizi san lg, fekon etc?
Je boxer nitapata kwa sh ngap angalau??
Ndio kwa bei hiyo utapa hizo hapo ambazo zimetumika wastan wa mwaka au zaidi.

Boxer angalua uwe na 1.5 ndio utapata ambayo ipo kwenye hali nzuri na haijapindwa sana na Engine ilipo vizuri.

Unajua engine ya Boxer mpya ni ghali sana utaona bora ununue mpya kabisaa.
Sasa usije ukauziwa kimeo cha boxer kisha engine ika noki,ndugu yangu utajuta kununua kwa laki 8.

We nenda kaulizie side miror tu ya boxer bei yake halafu ndio utajua kama vioo tu bei hiyo je chuma chake itafika bei gani.

Boxer ni nzuri sana,lakini ni bora ununue huku unauhakika na chombo hicho,maana hata kama ni 1m bado unatauziwa maiti tu.
Hivi vyombo wengi wanavitumia bila kufanya servicies ndio tatizo kubwa sana.
Boxer unaweza kutumia zaidi ya miaka 3 na ikawa ipo kwenye hali nzuri sana,hapo ni kwamba Services inafaywa kwa uhakika wa hali yajuu.
Tatizo hawa madereva wanopewa kuendesha Boxers na pikipiki nyingine services hawapeleki,yaani wao hadi pikipiki izime njiani ndio wanapeleka Services.Ndio maana unakuta Pikipiki zimenunuliwa muda moja na hali nzuri lakini mlio wake kama Generator.
Kwa wastan wa chni kabisa kwa Pikipiki kama inatumika kama Bodaboda kwenda Services ni wiki mbli,na sio service ya kubahatisha.Sasa Driver anaona duhhh,nitoe pesa karibia elfu kumi na kitu kwa services,yeye anapotezea.mwisho wa siku ugonjwa unakuwa mkubwa,na mara Engine inaanza kufa,hapo ndio inabidi ifunguliwe ili kubadilisha vifaa baadhi vya ndani vilivyokufa kwa uzembe wa kuzembea muda wa Services na kwa uhakika.
 
leta 1.2m nikuachie boxer iko poa na haina tatizo lolote!
 
....duh, asante sana mkuu Zanzibar Spices, naona nijipange nitafute chombo kizuri, maana napenda sana boxer ni kwa ajili ya matumizi yangu binafsi
 
tunegotiate tu mkuu, naomba uni attachie picha yake then twende pm
Safi sana Chagga,acha akutupie picha hapa ili tutathmini kisha ndio PM ifuate.
Ya muhim kujua ni haya:-
-Imetembea Km Ngapi
-Imenunuliwa lini
-Ilikuwa inatumika kama bodaboda au Binafsi
-Ina bima ya ina gani na inaisha lini
-Aina gani ya Boxer,maana kuna aina mbili muhim

kisha hapo mengine yafuate,

Muhim kwako:-
Ukipata Pikipiki yoyote,hakikisha unaenda na fundi kuikagua,tafuta fundi mpe kama buku kumi hivi ili umtoe sehem yake ya kazi.
Mie nikitaka kunua gari basi natoa Sh:50,000 kwa kumtoa fundi ili akanikagulie gari na kunishauri kama ni chaguo sahihi.
Unajua wengi tunafanya dharau juu ya hili lakini ni muhim sana,unaweza kuona gari bodi safii,ila ndani au model yake ni majanga au wengine unakuta gari nyingine imewekwa Engine nyingine.
Sasa nenda na fundi ili aikague na ai test,kisha atakushauri,na atakuambia nini vya kubadilisha ili irudi kuwa sawa.
 
Mkuu Zanzibar Spices umetoa ushauri Bab kubwa Sana aisee, dah hivi vitu kumbe siyo vya kukurupuka, naufata kwa asilimia 100, subiri nicheki Na wadau hapa alafu nijue tunafanyaje. Asante mkuu
 
Ongeza ongeza hela ununue mpya kama unataka utumie mwenyewe maana utanunua majanga maana pikipiki zinasumbua kuliko hata gari
 
Ndio kwa bei hiyo utapa hizo hapo ambazo zimetumika wastan wa mwaka au zaidi.

Boxer angalua uwe na 1.5 ndio utapata ambayo ipo kwenye hali nzuri na haijapindwa sana na Engine ilipo vizuri.

Unajua engine ya Boxer mpya ni ghali sana utaona bora ununue mpya kabisaa.
Sasa usije ukauziwa kimeo cha boxer kisha engine ika noki,ndugu yangu utajuta kununua kwa laki 8.

We nenda kaulizie side miror tu ya boxer bei yake halafu ndio utajua kama vioo tu bei hiyo je chuma chake itafika bei gani.

Boxer ni nzuri sana,lakini ni bora ununue huku unauhakika na chombo hicho,maana hata kama ni 1m bado unatauziwa maiti tu.
Hivi vyombo wengi wanavitumia bila kufanya servicies ndio tatizo kubwa sana.
Boxer unaweza kutumia zaidi ya miaka 3 na ikawa ipo kwenye hali nzuri sana,hapo ni kwamba Services inafaywa kwa uhakika wa hali yajuu.
Tatizo hawa madereva wanopewa kuendesha Boxers na pikipiki nyingine services hawapeleki,yaani wao hadi pikipiki izime njiani ndio wanapeleka Services.Ndio maana unakuta Pikipiki zimenunuliwa muda moja na hali nzuri lakini mlio wake kama Generator.
Kwa wastan wa chni kabisa kwa Pikipiki kama inatumika kama Bodaboda kwenda Services ni wiki mbli,na sio service ya kubahatisha.Sasa Driver anaona duhhh,nitoe pesa karibia elfu kumi na kitu kwa services,yeye anapotezea.mwisho wa siku ugonjwa unakuwa mkubwa,na mara Engine inaanza kufa,hapo ndio inabidi ifunguliwe ili kubadilisha vifaa baadhi vya ndani vilivyokufa kwa uzembe wa kuzembea muda wa Services na kwa uhakika.
mkuu uko vizuri na unaonyesha wazi unawafahamu vyema madereva na hii biashara ya bodaboda na boxer yenyewe. Boxer ikitunzwa vizuri aaahhh iko poa sanaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom