Nahitaji Emegency Temporary Passport kabla ya Jumatatu

Nahitaji Emegency Temporary Passport kabla ya Jumatatu

Nenda uhamiaji humu utaishia kilizwa tu ujanja wote huo hata passport huna
 
Nilipata ndani ya masaa 6. Nenda kwenye ofisi ya Uhamiaji iliyokaribu na wewe. Ongea nao vizuri.
 
Daah hadi passport za katatasi nayo ya masaa matatu mnataka kusaidiwa?
Nenda uhamiaji iliyo karibu yako ukachukue Sidhani kama inazidi Tsh 25,000 kwa malipo ya Serikali..
Uwe na barua ya mtendaji kukutambulisha ya kwako mwenyewe kuomba hiyo passport dhumuni lako la safari na picha 4 za Passport zinazoonyesha masikio yako yote na nyuma ya background iwe Blue sio nyeupe wanakupa siku hiyo hiyo...ni haki yako kuwa na passport na wale wapo pale kwa ajili ya kukupa passport...
 
Ukiwa Dar tulia kunywa maji ingia online jaza fomu timiza vigezo Magufuli stand huduma ya temporary ipo masaa 24 imewekwa maalumu kusaidia wasafiri Kama wewe kupata passport za emergency tu fika uliza ofisi ya uhamiaji ipo wapi watakuonyesha ilipo ndani ya stand
Kama utakuwa umeshindwa kukimbizana na muda wa ofisi za Serikali saa Tisa ni hadi jumatatu Tena ndo zinafunguliwa.
 
1. Nenda kwa Mtendaji, akuandikie barua ya utambulisho.
2. Nenda kwa mpiga picha, piga picha za passport na uwe nazo walau nne
3. Fika ofisi za uhamiaji karibu nawe. Eleza sababu za safari yako. Jaza form maalum.
4. Pata control number, lipia 20,000.
5. Pata passport yako

Chomoka. Kila la kheri..
Kama hakuna foleni, ndani ya lisaa limoja umeshapata.
 
1. Nenda kwa Mtendaji, akuandikie barua ya utambulisho.
2. Nenda kwa mpiga picha, piga picha za passport na uwe nazo walau nne
3. Fika ofisi za uhamiaji karibu nawe. Eleza sababu za safari yako. Jaza form maalum.
4. Pata control number, lipia 20,000.
5. Pata passport yako

Chomoka. Kila la kheri..
Kama hakuna foleni, ndani ya lisaa limoja umeshapata.

Umenena vyema.

Nilipata yangu ndani ya masaa 2 tu.
 
Ukiwa Dar tulia kunywa maji ingia online jaza fomu timiza vigezo Magufuli stand huduma ya temporary ipo masaa 24 imewekwa maalumu kusaidia wasafiri Kama wewe kupata passport za emergency tu fika uliza ofisi ya uhamiaji ipo wapi watakuonyesha ilipo ndani ya stand
Kama utakuwa umeshindwa kukimbizana na muda wa ofisi za Serikali saa Tisa ni hadi jumatatu Tena ndo zinafunguliwa.
Nilishawahi patumia hapo kwa ishu kama hii. Ni njia rahisi pia.
Muhimu kuelewana nao tu
 
Back
Top Bottom