Wakuu, wataalamu. Nimeanza kuhisi maumivu makali sana maeneo ya chini ya kifua. Ni siku ya tano toka nimeanza kuiExperience. Nimekuwa nikitumia dawa za maumivu kutuliza maumivu.
Kama kuna anayejua dawa inayowesa kunisaidia anisaidie, maana hii hali nasikia wanasema huwa inatibiwa kienyeji, lakini hapa nipo Dar.
Bado natafuta hela ya kwenda hospitalini, ila kama kuna dawa naweza kutumia kwa muda basi naomba mniambia. Maumivu ni makali hasa muda wa usiku.
View attachment 3515552
Umeandika kwa Hisia na maelezo yako yako bayana, hivyo sitarajii ukichukulia jambo kwa mzaha.
Bushdokta ni daktari wa mitishamba, hata hivyo ktk eneo hili tumewezeshwa kutambua maradhi yanayoweza kutibiwa kwa dawa na vipimo vya hospitali.
Maumivu yako ni eneo la Epigastrium yaani Chembe ya Moyo kwa lugha za kiswahili
Maumivu haya huashiria, Michubuko ktk njia ya Chakula Esophagus( Esophagistis), Gastric( Gastritis) na pia ni dalili za vidonda vya tumbo- Peptic Ulcer Disease.
Kama umri wako ni kuanzia miaka 40 kwenda Juu hakikisha
1. Unapima Blood Presha yako, BP
2. Kama presha iko juu hata kidogo tu pima Kipimo cha Moyo, ECG
Ikiwa Presha yako iko sawa basi Pima kipomo cha Maambukizi ya Bakteria wa Helicobacter Pylori ktk choo kikubwa, huyu bacteria husababisha michubuko, vidonda vya tumbo na acid nyingi.
Umesema umekuwa ukitumia dawa za maumivu kwa siku tano. Nakushauri uziache kuanzia leo kwani husababisha vidonda, michubuko na hata kuongeza maumivu zaidi.
Msisitizo; Kama una umri wa kuanzia 40 kwenda juu, nakuomba uende hospitali muda huu zingatia niliyoandika hapo juu. Na pengine kwrnye familia kuna ndugu wenye presha au maradhi ya moyo zingatia zaidi.
Kama umri sio ktk kiwango hicho, pata dawa za kupunguza acid tumboni za maji na vidonge then kesho nenda hospitali kwa H.Pylori testing.
Kuhusu matumizi ya mitishamba ni mpaka uwe umetimiza hayo juu, usipoteze muda na pesa zako