Nafikiria kuachana na kampuni ya simu TIGO ....

Nafikiria kuachana na kampuni ya simu TIGO ....

mkandaboy

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2012
Posts
257
Reaction score
89
Habari zenu wana JF? Naomba ku-share nanyi machungu ambayo TIGO wamekuwa wakinisababishia. Nimekuwa mteja mwaminifu wa kampuni hii tangu mwaka 2000 (enzi hizo ikiitwa BUZZ). Kiukweli nimefurahia sana huduma zao tangu wakati huo mpaka mwaka jana na sasa nafikiria kuchukua maamuzi magumu ya kuachana nao nihamie kwingine. Sababu kubwa ni hizi;
1. Wamekuwa wakinipora airtime kila mara ikitokea nimeongeza salio na sijalitumia kwa wakati huo. Kwa mfano naweza kuweka salio la sh 2,000/. Baada ya robo saa tu unakuta sh 500/ au zaidi imepungua, bila kupiga simu wala kutuma sms. Au napiga simu dakika nne tu wanachukua sh 1,000/. Ukipiga simu kuuliza wanaku-hold on hata robo saa na mwisho simu inakatika (au labda wanakata-sijui?).
2.Niliwahi ku-subscribe huduma ya kutumiwa ratiba na matokeo ya ligi mbalimbali za mpira wa miguu (mfano ya Uingereza, Uhispania). Huduma hiyo nimekuwa nikiipata vizuri. Imefikia wakati sasa nataka kujitoa kwa utaratibu ule ule walionielekeza wakati najiunga lakini wananing'ang'ania mno. Kila nikituma sms ya kujitoa wanaipokea lakini hawatekelezi ombi langu. Nikiwapigia simu yale yale ya kusubirishwa robo saa bila msaada.

Vipi wana JF wenzangu nanyi mmeshakutana na madhila kama hayo yangu? Kiukweli kabisa nafikiria kuachana na kampuni hii...
 
Nafikiri unachofanya ni kosa sana kwa biashara ya Tigo. Kwani ukiangalia kiundani sana una nia kuuwa biashara zao na kutukuza nyingine ambao ujajipambanua.

Ushauri wangu.

Pasi na shaka yoyote paleka malalamiko yako kwenye customer care zao na watatazama katika system zao na kukurudishia kilicho chako.

Vile vile huko Tanzania kuna TCRA na ukipitia website yao wana kitengo cha kutetea maslahi ya watumiaji wa huduma za simu. Please pitia hapo na weka malalamiko yako watakusaidia.

Huo ni ushauri wangu nikiangalia mada yako kwa jicho la kiuchumi zaidi.
 
Huwezi kujitoa mpaka uweke uzi?
OTIS
 
Tatizo la kuchukua airtime tigo wanalo wiki iliyopita nilikatwa 450 kwa siku mbili mfurulizo mpaka nikakosana na dogo nikijua amehamisha salio, alafu ukipiga huduma kwa mteja hawapokei mwisho wanakata 50.
 
Kujiunga sikuomba ushauri, wala hapa leo sijaomba ushauri...Soma text vizuri usikurupuke!!!!!
 
Hilo huwa linatokea kama umejiunga kutumiwa nyimbo mbali mbali au ratiba za michezo. Kama ulisha jiunga kupata huduma zao, nenda kajitoe vinginevyo wataendela kukata. Kuna Jamaa yangu walikuwa wanamkata hivyo, mpaka alipoenda kuwaona ofisini kwao.
 
Hilo huwa linatokea kama umejiunga kutumiwa nyimbo mbali mbali au ratiba za michezo. Kama ulisha jiunga kupata huduma zao, nenda kajitoe vinginevyo wataendela kukata. Kuna Jamaa yangu walikuwa wanamkata hivyo, mpaka alipoenda kuwaona ofisini kwao.

Thanx sawabho kwa ushauri
 
mi mwenewe leo najitoa..cjui ni cmu hangu vocher haziingiii toka asubuhi..Hapa mjini Arusha..hawa jamaa ni kuachana nao tu..
 
Back
Top Bottom