mzee wa njaa
JF-Expert Member
- Jun 16, 2011
- 1,366
- 223
CCM ni Chama Bora nchi hii kuliko vyote kwa mema ambayo kimewafanyia Watanzania. Kwani hamna ubishi viongozi wake wamekuwa wachapakazi na wenye utu kwa kuwatumikia wananchi wa nchi hii.
Na Serikali hii inayoongozwa na CCM imekuwa ikijituma kutatua matatizo yanayo wakabili Watanzania na pia serikali hii imejitahidi kuondoa kero za wananchi kwa 99%.
Mambo ambayo CCM imejitahidi ni kama ifuatavyo:
1. Imejenga barabara za Lami Tanzania nzima mpaka vijijini yaani hata peku peku unatembea kwa miguu.
2. Umeme mpaka kwenye nyumba za Makuti na umesambazwa Mjini na vijijini na sehemu ambapo haujafika milingoti ya kuwekea nyaya za umeme ndio tatizo inaliwa na mchwa sana.
3. Wananchi wa Tanzania wanaishi zaidi ya dola 50 kwa siku kutokana na sera safi za CCM. Kwa hili imefanikiwa kupunguza umasikini nchini Tanzania kwa 80%.
4. Tatizo la maji Tanzania limeshakuwa historia kila mtaa maji bwerereeeee. Hii ni kutokana na wizara ya maji kuwa wabunifu katika kutatua kero za wananchi hususani hii ya Maji.
5. Migomo Vyuo kikuu imeisha baada ya kuiboresha bodi ya mikopo hali iliyopelekea kila mwanafunzi aingiaye chuo kikuu anapewa bunda lake kwa wakati husika.
6. Shule za kata ambazo ni sera ya CCM zimeendelea kufaulisha kwa kasi na Mnamo mwaka jana 2010 zaidi ya 80% ya wanafunzi wa kata wale wa kidato cha 4 walifanikiwa kufaulu kwa daraja la kwanza, pili na la tatu hiyo yote ilitokana na sera madhubuti ya serikali ya CCM.
7. Pia kutokana na sera nzuri za CCM katika suala la Ajira. Serikali imefanikiwa kuajiri Watanzania milioni 5 katika mwaka wa ajira 2010/2011 wote wameajiriwa katika taasisi za serikali.
8. CCM ni chama madhubuti na kinachowapenda watanzania na pia kimeendelea kudumisha amani na utulivu nchini na hata kukitokea vurugu wanao uwawa ni wachache sana I mean sio idadi kubwa wanao uwawa na polisi.
9. Migodi mingi iliyobinafsishwa kutokana na sera ya serikali katika Uwekezaji imekuwa ikitoa matunda mengi sana. Mfano kwama wa fedha wa 2010/2011 migodi imechangia 78% katika pato la Taifa hii ukijumuisha migodi ya Tanzanite ( ambayo hupatikana Tanzania peke yake), dhahabu, almasi, rubi (Ulanga), Graphite, Chacoal, Asbesto, Gypsum na aina mbali mbali za madini.
Nawapongeza sana viongozi wa nchi ya Tanzania kwa kuonesha UTU na kuwajali Raia wake. Aluta Continua.
CCM Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.
Na Serikali hii inayoongozwa na CCM imekuwa ikijituma kutatua matatizo yanayo wakabili Watanzania na pia serikali hii imejitahidi kuondoa kero za wananchi kwa 99%.
Mambo ambayo CCM imejitahidi ni kama ifuatavyo:
1. Imejenga barabara za Lami Tanzania nzima mpaka vijijini yaani hata peku peku unatembea kwa miguu.
2. Umeme mpaka kwenye nyumba za Makuti na umesambazwa Mjini na vijijini na sehemu ambapo haujafika milingoti ya kuwekea nyaya za umeme ndio tatizo inaliwa na mchwa sana.
3. Wananchi wa Tanzania wanaishi zaidi ya dola 50 kwa siku kutokana na sera safi za CCM. Kwa hili imefanikiwa kupunguza umasikini nchini Tanzania kwa 80%.
4. Tatizo la maji Tanzania limeshakuwa historia kila mtaa maji bwerereeeee. Hii ni kutokana na wizara ya maji kuwa wabunifu katika kutatua kero za wananchi hususani hii ya Maji.
5. Migomo Vyuo kikuu imeisha baada ya kuiboresha bodi ya mikopo hali iliyopelekea kila mwanafunzi aingiaye chuo kikuu anapewa bunda lake kwa wakati husika.
6. Shule za kata ambazo ni sera ya CCM zimeendelea kufaulisha kwa kasi na Mnamo mwaka jana 2010 zaidi ya 80% ya wanafunzi wa kata wale wa kidato cha 4 walifanikiwa kufaulu kwa daraja la kwanza, pili na la tatu hiyo yote ilitokana na sera madhubuti ya serikali ya CCM.
7. Pia kutokana na sera nzuri za CCM katika suala la Ajira. Serikali imefanikiwa kuajiri Watanzania milioni 5 katika mwaka wa ajira 2010/2011 wote wameajiriwa katika taasisi za serikali.
8. CCM ni chama madhubuti na kinachowapenda watanzania na pia kimeendelea kudumisha amani na utulivu nchini na hata kukitokea vurugu wanao uwawa ni wachache sana I mean sio idadi kubwa wanao uwawa na polisi.
9. Migodi mingi iliyobinafsishwa kutokana na sera ya serikali katika Uwekezaji imekuwa ikitoa matunda mengi sana. Mfano kwama wa fedha wa 2010/2011 migodi imechangia 78% katika pato la Taifa hii ukijumuisha migodi ya Tanzanite ( ambayo hupatikana Tanzania peke yake), dhahabu, almasi, rubi (Ulanga), Graphite, Chacoal, Asbesto, Gypsum na aina mbali mbali za madini.
Nawapongeza sana viongozi wa nchi ya Tanzania kwa kuonesha UTU na kuwajali Raia wake. Aluta Continua.
CCM Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.