Na Declare War Jamani....CCM ni chama bora!

mzee wa njaa

JF-Expert Member
Jun 16, 2011
1,366
223
CCM ni Chama Bora nchi hii kuliko vyote kwa mema ambayo kimewafanyia Watanzania. Kwani hamna ubishi viongozi wake wamekuwa wachapakazi na wenye utu kwa kuwatumikia wananchi wa nchi hii.

Na Serikali hii inayoongozwa na CCM imekuwa ikijituma kutatua matatizo yanayo wakabili Watanzania na pia serikali hii imejitahidi kuondoa kero za wananchi kwa 99%.

Mambo ambayo CCM imejitahidi ni kama ifuatavyo:

1. Imejenga barabara za Lami Tanzania nzima mpaka vijijini yaani hata peku peku unatembea kwa miguu.

2. Umeme mpaka kwenye nyumba za Makuti na umesambazwa Mjini na vijijini na sehemu ambapo haujafika milingoti ya kuwekea nyaya za umeme ndio tatizo inaliwa na mchwa sana.

3. Wananchi wa Tanzania wanaishi zaidi ya dola 50 kwa siku kutokana na sera safi za CCM. Kwa hili imefanikiwa kupunguza umasikini nchini Tanzania kwa 80%.

4. Tatizo la maji Tanzania limeshakuwa historia kila mtaa maji bwerereeeee. Hii ni kutokana na wizara ya maji kuwa wabunifu katika kutatua kero za wananchi hususani hii ya Maji.

5. Migomo Vyuo kikuu imeisha baada ya kuiboresha bodi ya mikopo hali iliyopelekea kila mwanafunzi aingiaye chuo kikuu anapewa bunda lake kwa wakati husika.

6. Shule za kata ambazo ni sera ya CCM zimeendelea kufaulisha kwa kasi na Mnamo mwaka jana 2010 zaidi ya 80% ya wanafunzi wa kata wale wa kidato cha 4 walifanikiwa kufaulu kwa daraja la kwanza, pili na la tatu hiyo yote ilitokana na sera madhubuti ya serikali ya CCM.

7. Pia kutokana na sera nzuri za CCM katika suala la Ajira. Serikali imefanikiwa kuajiri Watanzania milioni 5 katika mwaka wa ajira 2010/2011 wote wameajiriwa katika taasisi za serikali.

8. CCM ni chama madhubuti na kinachowapenda watanzania na pia kimeendelea kudumisha amani na utulivu nchini na hata kukitokea vurugu wanao uwawa ni wachache sana I mean sio idadi kubwa wanao uwawa na polisi.

9. Migodi mingi iliyobinafsishwa kutokana na sera ya serikali katika Uwekezaji imekuwa ikitoa matunda mengi sana. Mfano kwama wa fedha wa 2010/2011 migodi imechangia 78% katika pato la Taifa hii ukijumuisha migodi ya Tanzanite ( ambayo hupatikana Tanzania peke yake), dhahabu, almasi, rubi (Ulanga), Graphite, Chacoal, Asbesto, Gypsum na aina mbali mbali za madini.

Nawapongeza sana viongozi wa nchi ya Tanzania kwa kuonesha UTU na kuwajali Raia wake. Aluta Continua.


CCM Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.
 
oyeeeeeee......nimependa sana hapo kwenye madini na aina zake.....
 
hebu tukipe imani chama kitukufu na kisikivu cha ccm ccm ni safi tatizo ni viongozi wake hivyo tukipe muda wa kutosha
 
vipofu hawawezi kusoma maandishi haya, wapelekee kwa technologia sahihi labda watakuelewa, usisahau kuandaa semina elekezi, posho ziwepo. uwaalike vipofu nchi nzima, wageni waalikwa wafuatao lazima wa epo 1. ana makinda aka bibi kiroboto 2. mizengwe pinda aka mzee wa kulialia 3. napeegwa nnauye aka .....4. john komba aka fungo. hao mtaelewana, ukimshirikisha ndg. Zitto kabwe utata wa posho utajitokeza patakuwa na maswali magumu umepata wapi fungu na watafaidika nini wananchi kwa hi yo semina, ukimshirikisha ndg. John Mnyika usitumie mtindo wa makanuni kama mjengoni, ukimualika ndg. Tundu Lisu atawasanua kumbi na kumbinga watakustukia, kwa uongo wako ukimualika ndg. Godbless lema ujue ngumi zitafumuka na itawawia ngumu kuwaokoa vipofu, tahadhari, ndg. Wilbrod Slaa anaweza kuhudhuria atawapiga shule kiwango cha PHD nao watauelewa uongo wako na hasira zao zitapanda wakasusia posho kisha hao vipofu wataokota mawe watakupiga sitegemei kama utapona, kwani wananchi kwa ujumla hawatakuokoa kwa vyovyote.
 
NENDA MUHIMBILI WODI ZA WAGONJWA AU WEWE MWENYEWE UUGUE AU UWE NA MGONJWA UJIONEE KISHA ULETE UPUUZI WAKO JAMVINI!maendeleo yanapatikana RWANDA si tanzania.darasa la 4 la mkoloni ni sawa na form 4 ya leo.reli bandari mashamba ya katani kahawa karanga mawese leo yapo wapi?
 
Sasa kama unayosema ni ya kweli basi je ni kwanini Tanzania inajulikana kama nchi masikini sana duniani??? na Chama kilichotawala ni kimoja tu CCM!! Je ni kwasabu hatuna rasilimali, majanga mengi , Uvivu au Sera. Kwa mawazo yangu ni sera na uongozi Mbovu. Na unavyosema CCM imejenga barabara mbona barabara zote zinajengwa kwa misaada!!!. China wamejenga barabara ya Mtwara, Japan wamejengwa Tanga, wanajenga hata sasa hivi kutokea Mwenge Tegeta hapo dar ni pesa ya Japan ambayo kwa sasa ina maafa makubwa na ni nchi ndogo!!. Nimekutana na kiongozi wa Millennium Challenge kwenye Tanzania diaspora MN na anasimamia $680 ma msaada wa USA kwa Tanzania kwenye barabara na nishati na sababu ya yeye kusimamia hizo pesa ni kuuogopa Rushwa ya serikali na kwamba pesa hazitaenda kwenye miradi. Huyu jamaa anajua vijiji kuliko katibu mkuu wa raisi ambaye tulikuwa naye pale!. Sasa CCM imeleta maendeleo gani hata Chuo cha Dodoma kimejegwa na NSSF na Bill gates Foundation.
Mimi naona badala ya kupoteza muda kudanganya watu kuwa tuna maendeleo wakati hatuna hata umeme hapo dar!!! ingekuwa vizuri tutafakari ninini cha kufanya ili nchi yetu iendelee na pengine ni kuwa na Chama kingine kwa miaka mitano tuone maana Watanzania tumechoka umasikini. Huu si wakati wa maendeleo bali ni wakati wa kutatua matatizo. Ukiende Lushoto vijijini hakuna Umeme, maji wala barabara!!! halafu unasema kuna umeme hadi vijijini ! hivyo vijiji vyenye umeme ni kwa Wachagga tu ambao wengi wao sio watu wa CCM. Wachagga wana Umeme, Maji, na barabara ya lami kila mahali hadi kijijini na ni kwasababu hawategemei serikali na wanafanya harambee zao wenyewe. Nenda Lindi na Mtwara kuna Gas nyingi je wana maendeleo!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom