tamimusalim
JF-Expert Member
- Jun 17, 2014
- 1,822
- 499
Mzungu mmoja uko wilaya arumeru mkoani arusha , imethibitika ameweza kuinunua shule moja ya msingi mali ya serikali katika kijiji cha doli, na kisha kuwajengea shule ya kisasa kabisa nje kabisa ya eneo hilo lilipokuwa shule hiyo, inasemekana kabisa kuwa eneo hilo ilipokuwa shule ilionunuliwa limesheheni madini ya tazanite" kwa mujibu wa mwanakikiji mmoja aliepewa kazi ya kuchimba shimo la choo kabla ya kuninuliwa na mzungu uyo na kubaini kiasi kikubwa cha madini hayo katika eneo hilo kwa sasa eneo hilo limepigwa uzio wenye kulidwa na umeme, walinzi na mbwa, baada ya wanakijiji kuridhia kuuza eneo hilo la heka 1 na shule hiyo ambayo ilikuwa aina hata madirisha, pia choo mzungu huyo aliwazawadia shule ya kisasa na kuninua gari la walimu na wanafunzi kama asante, kwa kumpa eneo hilo, kwa sasa lina ulinzi mkali ambapo marufuku kuingia eneo hilo, mbunge wa arumeru mashariki anajua hilo.
Wakati huohuo Geta
Sakata la kuporwa kwa kiwanja cha shule ya msingi Nyankumbu Wilayani Geita Mkoani hapa limechukua sura mpya baada ya wananchi kumgomea mwekezaji kujenga mpaka serikali itakapomaliza mgogoro ulipo.
Wakizungumza na Channel Ten iliyofika kwenye eneo hilo na kukuta ujenzi ukiwa umesimama, wananchi hao wamesema kitendo cha Serikali kupora eneo hilo na kuwauzia watu wenye fedha bila wao kujulishwa hakikubaliki hata kidogo.
Wananchi hao wametoa ushauri wao kwa kusema ni bora serikali iwe inawashirikisha wahusika wa maeneo ili kuepuka migogoro isiyokuwa ya lazima kama inavyoweza kutokea katika eneo hilo.
Kaimu Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Jacob Katira amesema kuporwa kwa maeno hayo na kuuziwa watu wenye fedha kumesababisha matatizo makubwa kwa wanafunzi wake.
Kuporwa kwa nguvu maeneo na viwanja vya shule katika Mkoa wa Geita na kupewa watu wenye fedha kunazidi kushamili huku watoto wakiwa wanawarundikana kwenye vyumba vidogo vya madarasa kwa kukosa maeneo ya kujengwa madarasa.
Chanzo: Channel ten
Wakati huohuo Geta
Sakata la kuporwa kwa kiwanja cha shule ya msingi Nyankumbu Wilayani Geita Mkoani hapa limechukua sura mpya baada ya wananchi kumgomea mwekezaji kujenga mpaka serikali itakapomaliza mgogoro ulipo.
Wakizungumza na Channel Ten iliyofika kwenye eneo hilo na kukuta ujenzi ukiwa umesimama, wananchi hao wamesema kitendo cha Serikali kupora eneo hilo na kuwauzia watu wenye fedha bila wao kujulishwa hakikubaliki hata kidogo.
Wananchi hao wametoa ushauri wao kwa kusema ni bora serikali iwe inawashirikisha wahusika wa maeneo ili kuepuka migogoro isiyokuwa ya lazima kama inavyoweza kutokea katika eneo hilo.
Kaimu Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Jacob Katira amesema kuporwa kwa maeno hayo na kuuziwa watu wenye fedha kumesababisha matatizo makubwa kwa wanafunzi wake.
Kuporwa kwa nguvu maeneo na viwanja vya shule katika Mkoa wa Geita na kupewa watu wenye fedha kunazidi kushamili huku watoto wakiwa wanawarundikana kwenye vyumba vidogo vya madarasa kwa kukosa maeneo ya kujengwa madarasa.
Chanzo: Channel ten