Jumong S
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 7,427
- 10,749
Baba wa Taifa hili Mwl J. K Nyerere alikuchagua na kukuamini na hakika pamoja na mapungufu yako ulilitendea haki Taifa. Uchumi wetu ulipanda, uliinua uwekezaji, deni la Taifa lilipungua sana na ulikuwa hakika na maamuzi ya ki-uongozi.
Sasa ona, wale aliokuwa akiwakataa Baba wataifa kwa nia nzuri kuwa hawataweza kuwatetea masikini ndio wanagombania urithi wa Taifa hili. Sasa ni dhahiri, wenye pesa tusizojua wanazitoa wapi wanakusanyana viwanjani, wanapeana kampani huku wakionesha jeuri ya pesa ndio wanaelekea kutuchagulia viongozi wanyonge tusio na sauti.
Wamemuandaa kiongozi uliyempinga kwa niaba yetu ili akakikalie kit chako Ikulu. Je, mnyonge atapona? Viongozi mlioaminiwa na Mwalimu mko wapi? Hamuyaoni haya? Mbona mmekaa kimya?
TANZANIA INAHITAJI KIONGOZI MWENYE MENO MAKALI, ANAYEJITEGEMEA, ASIYEAMRIWA NA WENYE PESA.
Ndg Mkapa na wenzako mkikaa kimya mjue mtabeba dhambi hii.
Sasa ona, wale aliokuwa akiwakataa Baba wataifa kwa nia nzuri kuwa hawataweza kuwatetea masikini ndio wanagombania urithi wa Taifa hili. Sasa ni dhahiri, wenye pesa tusizojua wanazitoa wapi wanakusanyana viwanjani, wanapeana kampani huku wakionesha jeuri ya pesa ndio wanaelekea kutuchagulia viongozi wanyonge tusio na sauti.
Wamemuandaa kiongozi uliyempinga kwa niaba yetu ili akakikalie kit chako Ikulu. Je, mnyonge atapona? Viongozi mlioaminiwa na Mwalimu mko wapi? Hamuyaoni haya? Mbona mmekaa kimya?
TANZANIA INAHITAJI KIONGOZI MWENYE MENO MAKALI, ANAYEJITEGEMEA, ASIYEAMRIWA NA WENYE PESA.
Ndg Mkapa na wenzako mkikaa kimya mjue mtabeba dhambi hii.