Mzee Mtei ataka iundwe Serikali ya mseto na Rais Magufuli aungwe mkono

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Mtei amesema ili Watanzania wengi, wapate fursa ya kutoa mchango wao katika kuendeleza Taifa ni muhimu kuwepo mabadiliko ya Katiba ambayo yatawezesha kuundwa serikali ya mseto baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2020.

Anasema haiwezekani watu wanaungwa mkono na watu wengi, lakini baada tu ya uchaguzi wanakosa fursa ya kutoa mchango wao kwa maendeleo ya taifa.

“Mfano, Chadema tuna wafuasi wengi sana sio vizuri kuwaacha hivi hivi, baada ya uchaguzi ni muhimu wapate fursa kupitia muungano wa vyama kushiriki katika ujenzi wa taifa lao,” alisema.

Mtei alisema wakati Watanzania, wanamkumbuka Mwalimu ni muhimu pia kuendelea kushirikiana kwa pamoja kudumisha amani na utulivu katika taifa na kujitahidi kuondoa tofauti za kisiasa ili zisiwe chanzo cha vurugu.

Kuhusu Uongozi wa Rais Magufuli.
Mzee Mtei anasema Rais John Magufuli anafanya kazi nzuri katika kuimarisha uchumi na anapaswa kuungwa mkono, lakini kuna mapungufu kuhusu masuala ya demokrasia na uhuru wa watu.

“Rais anafanya kazi nzuri sana, uchumi unakwenda, lakini pia amerejesha nidhamu serikalini na sasa watendaji wa serikali wanatoa huduma nzuri kwa wananchi,” alisema.

Alisema angependa Rais Magufuli, kuungwa mkono katika mambo mazuri ambayo anafanya ingawa bado hajafikia uwezo wa Baba wa Taifa.

Mtei alisema hata hivyo, Rais anapaswa kuwashirikisha watu wengi katika uendeshaji wa nchi, kwani kuna makundi mengine wakiwepo wapinzani wamewekwa nyuma jambo ambalo sio zuri.

CHANZO: Gazeti la Mwananchi.
 
Mawazo ya Mzee Mtei ukiyachambua bila kuangalia uvyama utagundua ni mawazo mazuri sana kwa maendeleo ya haraka nchini.

Siasa zetu ambazo tumezijenga kutokana na msingi wa siasa za Uingereza zenye msingi wa ‘’First past the post(FPTP) AKA winner takes all zinanyima fursa vyama vingine katika ujenzi wa taifa.

Dhana ya First Past the Post inajenga mazingira ya kuwa na kundi la wapinzani ambao kazi yao inakuwa ni kupinga kila kitu kinachofanywa na serikali na wale wanaounda serikali inakuwa kazi yao ni kuunga mkono kila kinachofanywa na serikali.

Hii dhana ya First Past the Post inaleta mgawanyiko wa kisiasa ambao madhara yake hata maendeleo yanakuwa ni kusuasua. Kinachotokea Uingereza kuhusu BREXIT ni matokeo ya siasa za First Past the Post ambao chimbuko lake ilikuwa ni kutafuta kura ili kuunda serikali kwa gharama ya taifa la Uingereza kugawanyika.

Tatizo lililopo ni nani atamfunga paka kengere ya kisiasa?
 
Mbona serikali yetu ni ya mseto. Kina kafulila, shonza, patrobasi, mama mgwira, kitila n.k wameshirikishwa serikalini
Mkuu;
Huwezi kusema hao wameunda serikali ya mseto.

Hao uliwataja walitakiwa wabaki kama wanachama wa vyama vingine kama walivyokuwa kabla ya kupewa wadhifa wa kisiasa ndani ya serikali.

Tatizo lililopo wanaopewa nafasi za kisiasa kwenye serikali baada ya muda wanajiunga kwenye chama cha Rais aliyeko madarakani ili wasionekane wapinzani.
 
Mbona serikali yetu ni ya mseto. Kina kafulila, shonza, patrobasi, mama mgwira, kitila n.k wameshirikishwa serikalini
Una uelewa finyu kuhusu serikali ya mseto (coalition government).
Labda nikupe mfano hai wa serikali ya mseto. Kipindi kile maalim Seif Sharif alipokuwa makamu wa kwanza wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar yeye akiwa kutoka CUF wakati rais anatokea CCM ndio walitengeneza maana halisi ya coalition government japo nayo kwa kiasi kikubwa ilitawaliwa na ma CCM ila angalau inaweza kuwa ya mfano.
 
Zanzibar serikali ya mseto ipo ila chadema hawakuambulia hata mjumbe wa nyumba kumi
Tatizo lililotokea Zanzibar ni ubinafsi wa Maalim Seif.

Badala ya kugawana majukumu ya kuongoza Zanzibar, yeye alitaka cheo!

Matokeo ya kutaka cheo ndio yamekifanya chama cha CUF kujikuta kiko nje ya serikali ya mseto na chama cha ADC kinachoongozwa na Hamad Rashid Mohamed kuingia kwenye serikali ya mseto.
 
Mkuu;
Nadhani nimeeleza na kufafanua kwenye bandiko la #4
Wenzetu nchi zingine Raisi akishinda hukubali matokeo na kumpongeza.Kwetu hawakubali matokeo hawampongezi.Chadema ilitoa tamko kabisa kuwa hawayakubali matokeo ,hawamtambui Magufuli hata siku ya kuapishwa walisema wanachama wao wasiende Raisi ,alipoenda bungeni wakatoka nje kupinga kutomtambua.Sasa unaundaje serikali ya umoja wa kitaifa kwenye mazingira hayo ya kutotambuliwa.Utaunda Kama Nani wakati hawakuambui?
 
Nyerere wa Chadema na Mchumi nguli, Governor na Waziri wa Fedha Mstaafu a.k.a Baba Mkwe Ndugu Mtei amekiri Ndugu Rais anafanya vizuri sana Kiuchumi, Mie Bavicha kwangu Pakavu mpiga deki wa Barabarani nasubiri nini kumuunga Mkono Rais
 
Leo nimeukubali uchambuzi wako mdogo...una bonge la point
Mawazo ya Mzee Mtei ukiyachambua bila kuangalia uvyama utagundua ni mawazo mazuri sana kwa maendeleo ya haraka nchini.

Siasa zetu ambazo tumezijenga kutokana na msingi wa siasa za Uingereza zenye msingi wa ‘’First past the post(FPTP) zinanyima fursa vyama vingine katika ujenzi wa taifa.

Dhana ya First Past the Post inajenga mazingira ya kuwa na kundi la wapinzani ambao kazi yao ni kupinga kila kitu kinachofanywa na serikali na wale wanaounda serikali inakuwa kazi yao ni kuunga mkono kila kinachofanywa na serikali.

Hii dhana ya First Past the Post inaleta mgawanyiko wa kisiasa ambao madhara yake hata maendeleo yanakuwa ni kusuasua. Kinachotokea Uingereza kuhusu BREXIT ni matokeo ya siasa za First Past the Post ambao chimbuko lake ilikuwa ni kutafuta kura ili kuunda serikali kwa gharama ya taifa la Uingereza kugawanyika.

Tatizo lililopo ni nani atamfunga paka kengere ya kisiasa?
 
Una uelewa finyu kuhusu serikali ya mseto (coalition government).
Labda nikupe mfano hai wa serikali ya mseto. Kipindi kile maalim Seif Sharif alipokuwa makamu wa kwanza wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar yeye akiwa kutoka CUF wakati rais anatokea CCM ndio walitengeneza maana halisi ya coalition government japo nayo kwa kiasi kikubwa ilitawaliwa na ma CCM ila angalau inaweza kuwa ya mfano.
Haya mambo usiyachukulie siriaz Sana mkuu utakufa kabla ya siku zako. Tatizo mnaanzusha mada ambazo haziwezekani. Chama kilichojiandaa kutawala milele hakiwezi kufikiria serikali ya mseto. Ndo Mana hawawezi kurudia makosa waliyoyafanya Zanzibar
 
Wenzetu nchi zingine Raisi akishinda hukubali matokeo na kumpongeza.Kwetu hawakubali matokeo hawampongezi.Chadema ilitoa tamko kabisa kuwa hawayakubali matokeo ,hawamtambui Magufuli hata siku ya kuapishwa walisema wanachama wao wasiende Raisi ,alipoenda bungeni wakatoka nchi kupinga kutomtambua.Sasa unaundaje serikali ya umoja wa kitaifa kwenye mazingira hayo ya kutotambuliwa.Utaunda Kama Nani wakati hawakuambui?
Mkuu;
Kama nilivyoeleza kwenye bandiko langu la #2, tatizo hilo ukilichunguza sana utagundua linatokana na mfumo wa First Past the Post.

Kama CHADEMA wangejua kuwa watakuwa sehemu ya serikali nadhani ingekuwa rahisi kwao kukubaliana na matokeo kwa sababu wangejua kuwa watakuwa ni sehemu ya serikali pamoja na kwamba wameshindwa katika Uchaguzi Mkuu.
 
Tatizo lililotokea Zanzibar ni ubinafsi wa Maalim Seif.

Badala ya kugawana majukumu ya kuongoza Zanzibar, yeye alitaka cheo!

Matokeo ya kutaka cheo ndio yamekifanya chama cha CUF kujikuta kiko nje ya serikali ya mseto.
Na hili ndio tatizo kubwa sana hapa Tanzania, wanasiasa wengi hawajali mustakabari wa raia wao wanachojali ni vyeo tu. Mtu anapigana kufa na kupona ili apate cheo akishakipata anaona malengo yake yameshatimia
 
Mbona serikali yetu ni ya mseto. Kina kafulila, shonza, patrobasi, mama mgwira, kitila n.k wameshirikishwa serikalini

Katiba inasemaje kuhusu hilo?
Je mwanasheria mkuu wa serikali na viongozi wengine waandamizi wanaostahili kumshauri Mhe. Rais hawakumshauri/ kumkumbusha Rais ?
 
Mkuu;
Huwezi kusema hao wameunda serikali ya mseto.

Hao uliwataja walitakiwa wabaki kama wanachama wa vyama vingine kama walivyokuwa kabla ya kupewa wadhifa ndani ya serikali.

Tatizo lililopo wanaopewa nafasi za kisiasa kwenye serikali baada ya muda wanajiunga kwenye chama cha Rais aliyeko madarakani.
Mrema alisema mtaunda ukawa yenu na TLP. Kule Zanzibar tayari Hamad Rashid na chama chake ni sehemu ya Serikali. Serikali Mseto tayari.
 
Back
Top Bottom