mghoshimgima
Member
- Sep 20, 2014
- 6
- 0
Kwa muda mrefu kumekuwa na mzozo kati ya mzee Yusuph Makamba na viongozi wa BAKWATA wilaya ya Lushoto kwa kuwa mzee Makamba hautambui uongozi wa BAKWATA wilaya hiyo.
Mzee Makamba alianzisha taasisi yake ya dini bila ridhaa ya BAKWATA wilaya ya Lushoto lakini akafanikiwa kuisajiri bila kushirikisha wilaya ya Lushoto na kumekuwa na mizozo mikubwa ambayo mingine ilibidi hata polisi kuingilia kati baada ya dalili za machafuko, leo hii huko nyumbani kwa mzee Makamba, Mahezangulu waislamu wamegawanyika na taasisi yake imechukua mali zote za waislamu ambazo mzee Makamba aliwahi kuzichangia na kuziweka chini ya taasisi yake.
Baada ya kuona BAKWATA wilaya ya Lushoto haimuungi mkono, mzee Makamba amepigania chinichini kupata BAKWATA wilaya ya Bumbuli, maana sasa Bumbuli ni halmashauri ndani ya wilaya ya Lushoto, lakini nia yake kulazimisha iwepo BAKWATA wilaya ya Lushoto, baada ya kutumia njia zake akafanikiwa kupata usajiri kinyuma na utaratibu unaotakiwa na yeye mwenyewe kuteua viongozi wa BAKWATA hiyo.
Tofauti na matarajio yake, alipoitisha mkutano wa viongozi wa bakwata na masheikh ndani ya bumbuli, viongozi wale waliipinga na kumuambia hawatambui utaratibu huo na shekh wa mkoa wa Tanga aliyetumwa kuongea nao alishangaa alipoambiwa ukweli na kuona msimamo wa waislamu wale, na kwakuwa yeye alitumwa na mzee Makamba akawaambia viongozi wale waandike barua ya kupinga ndio viongozi wale wa kata 14 kati ya 16 ndani ya bumbuli walipo sign kupinga mpango huo wa mzee makamba.
Itakumbukwa pia mzee makamba amemshitaki mwenyekiti wa BAKWATA wilaya na kumdai fidia ya mil 20 kwa kuwa alimpinga hadharani.
Barua ya waislamu imeambatanishwa.
Huu ni muendelezo wa upinzani anaoupata mzee makamba na mwanae ndani ya jimbo la Bumbuli.
Mzee Makamba alianzisha taasisi yake ya dini bila ridhaa ya BAKWATA wilaya ya Lushoto lakini akafanikiwa kuisajiri bila kushirikisha wilaya ya Lushoto na kumekuwa na mizozo mikubwa ambayo mingine ilibidi hata polisi kuingilia kati baada ya dalili za machafuko, leo hii huko nyumbani kwa mzee Makamba, Mahezangulu waislamu wamegawanyika na taasisi yake imechukua mali zote za waislamu ambazo mzee Makamba aliwahi kuzichangia na kuziweka chini ya taasisi yake.
Baada ya kuona BAKWATA wilaya ya Lushoto haimuungi mkono, mzee Makamba amepigania chinichini kupata BAKWATA wilaya ya Bumbuli, maana sasa Bumbuli ni halmashauri ndani ya wilaya ya Lushoto, lakini nia yake kulazimisha iwepo BAKWATA wilaya ya Lushoto, baada ya kutumia njia zake akafanikiwa kupata usajiri kinyuma na utaratibu unaotakiwa na yeye mwenyewe kuteua viongozi wa BAKWATA hiyo.
Tofauti na matarajio yake, alipoitisha mkutano wa viongozi wa bakwata na masheikh ndani ya bumbuli, viongozi wale waliipinga na kumuambia hawatambui utaratibu huo na shekh wa mkoa wa Tanga aliyetumwa kuongea nao alishangaa alipoambiwa ukweli na kuona msimamo wa waislamu wale, na kwakuwa yeye alitumwa na mzee Makamba akawaambia viongozi wale waandike barua ya kupinga ndio viongozi wale wa kata 14 kati ya 16 ndani ya bumbuli walipo sign kupinga mpango huo wa mzee makamba.
Itakumbukwa pia mzee makamba amemshitaki mwenyekiti wa BAKWATA wilaya na kumdai fidia ya mil 20 kwa kuwa alimpinga hadharani.
Barua ya waislamu imeambatanishwa.
Huu ni muendelezo wa upinzani anaoupata mzee makamba na mwanae ndani ya jimbo la Bumbuli.