Mzee Kikwete pumzika sasa, mpe nafasi Magufuli

mwanamichakato

JF-Expert Member
Mar 20, 2015
887
705
Salaam,
Naheshimu sana uamuzi wa hekima wa kutong'ang'ania madaraka ya kuendelea kuongoza taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanywa na mzee wetu Dr Jakaya Kikwete..Angeliweza kabisa kutumia nguvu ya dola/Nguvu ya ushawishi kwenye chama/Kofia zake zote za kimamlaka kubadiri katiba ili kuongeza vipindi vingine vya kuongoza lakini hakuthubutu kufanya japo kauli za watu fulani fulani kutaka aendelee zilikuwapo huku na kule kama ambavyo zilikuwapo wakati wa Hayati Mwl J.K.Nyerere,Alhaji Mzee A.H.Mwinyi na Hatimae Mzee B.W.Mkapa.

Si kazi rahisi kuachia enzi kuu kama ya urais wa nchi yenye vinono vya kiuongozi japo pia ni mzigo mzito mnoo.Rais wa JMT ana mamlaka makubwa sana tena sana kikatiba yahusuyo mamlaka,nguvu na uweza wa utendaji kazi zikiwepo amri,teuzi,maelekezo,kukata majina/kupitisha majina ya wanaotakiwa ama wasiotakiwa na taifa/nchi kiuongozi n.k.Umaarufu wa Dr. Jakaya Kikwete ndani na nje ya mipaka ya JMT si wa kubezwa kuzingatia ya kuwa ni juzi juzi tu alikuwa madarakani kama raia namba moja wa taifa lenye kuinuka katika nyanja nyingi za kifulsa,rasilimali {madini,mafuta,gesi,etc} na wingi wa ukarimu kwa wawekezaji na wageni mbalimbali.

Taratibu Mh. Rais JPM ameanza kuchomoza katika shughuri za kitaifa na kiplomasia kimataifa kwa kushiriki matukio ya kitaifa katika nchi jirani kama Rwanda kisha Uganda yamkini baadae Kenya n.k n.k. Haiba ya kisiasa hujiweka wazi kwa sasa mahari wanapokutana mh. Rais JPM na Mh.Dr. Kikwete kama ambavyo imejitokeza nchini Uganda{Hekima itumike kulielewa hili}.Dr.J.Kikwete bado amekuwa na mwonekano rasmi kana kwamba bado ni rais wa JMT na hili limekuwa likijidhihirisha maeneo kadhaa anakopita ama kunena jambo lenye mguso wa kimamlaka {Mfano:Alipotembelea daraja la Nyerere,n.k}.

Kwa desturi tumeshuhudia na tulishuhudia ukimya na utulivu mkubwa ktk tamalaki ya kimamlaka pale Mzee Mwinyi alipomwachia madaraka Mzee Mkapa,Vivo hivyo Mzee Mkapa alipomwachia madaraka Mzee Kikwete.Kwamba ilifika wakati Mzee Mkapa alikataa baadhi ya miariko/Ushiriki wa matukio/n.k kuepuka kuikwadha serikali {Rais} aliepo madarakani

Nadhani Mh. JPM na Serikali yake anapaswa kupewa nafasi pana zaidi katika kutekeleza/kujiachia/kujinafasi kiuongozi na majukumu yake yakinifu kimadaraka.Hivyo ni ushauri kwa marais waliomaliza vipindi vyao,waliostaafu kuwa wakimya,watulivu,wapole,ikibidi kujichimbia mahari ambako awatavuta attention ya namna yeyote kuepusha mgongano wa nguvu/mwangwi/vigelegele vya madaraka.

Yawezekana nakashindwa kueleweka kwa baadhi ya wabobezi ktk uandishi ulionyooka,hata hivyo nina imani kubwa ujumbe wangu yawekekana umeeleweka
 
Umenena kweli kabisa mkuu.

Ni bora JK ajifunze busara za mzee Mwinyi na Mzee Mkapa waliotulia kama hawapo vile, mpaka watafutwe na serikali.

Juzi nilishangaa kumuona JK Uganda wakati tarifa ya Uganda haikumtaja kama mualikwa, badala yake ilimtaja mzee Mwinyi lakini ghafla JK akatokelezea from nowhere.

Ndani ya miezi mitatu ya mwaka huu keshaenda China, Marekani, Uganda, Kenya, Sudani na kwingineko.

Hii ina tafsiri moja tu kwamba, jamaa ni "kiguu na njia" na "mdandiaji wa ishu zisizomuhusu".

Kwa Rais mstaafu haifai kwenda kutembelea daraja la Kigamboni kwa mbwembwe kama zile, huku ukikusanya waandishi wa habari na bashasha kibao za viongozi wa chama, na haitoshi, kulikuwa na taarifa rasmi kwa vyombo vya habari siku tatu kabla kuwa JK atafanya ziara rasmi ya kutembelea daraja la Kigamboni.

Mbona Mkapa hakufanya ziara rasmi ya kutembelea uwanja wa Taifa alioujenga??

JK apumzike sasa, amuache Magufuli afanye kazi.
 
Mto hufuata bahari, bahari haifuati mto
Charisma ya Kikwete inawafanya wanaomualika wamualike tu kwa sababu uwepo wake unawafanya wajisikie vizuri!

Kikwete hakutoa Amri darajani, bali alitoa ushauri!

Kitu kingine, Serikali yenyewe inamuomba aiwakilishe katika mambo kadha wa kadha, na hili ni jambo la utamaduni kwa raisi aliyeko madarakani kumuomba mtangulizi wake katika uwakilishi wa mambo kadhaa hususan ya kidiplomasia.

Acheni chuki.
 
Sawa ni vizuri JK akaacha ku mu over shadow JPM,lakini.
1.Tunaambiwa kuna kazi anaombwa na JPM kuzifanya au kumuwakilisha JPM,je akatae?.

2.Saa zingine JK anaponzwa na haiba yake.JK ana haiba Kali sana, akisema au akitokea mahali ana mfunika kila mtu. Ni vizuri siku ya uzinduzi wa daraja hakuwepo, maana angekuwepo, wengine wasinge onekana kabisa.
3.Mitandao ya kijamii pia inachangia sana kumfanya JK aonekane kama bado yupo in power. Maana kila kukicha JK hivi JK vile. Ni kama vile watu wanashindwa ku deal na JPM badala yake wanatupa hasira zao kwa JK.
 
Hamjui kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa chama chetu ambacho rais wetu naye ni mwanachama wake. Acheni wivu wa kike alahh?
Katiba inamruhusu kukusanyika na kutoa maoni,kwani JPM amazuiwa sehemu kutokua rais?
Dunia inafahamu yeye kwa sasa ndiye presidaa wa TZ
 
Salaam,
Naheshimu sana uamuzi wa hekima wa kutong'ang'ania madaraka ya kuendelea kuongoza taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanywa na mzee wetu Dr Jakaya Kikwete..Angeliweza kabisa kutumia nguvu ya dola/Nguvu ya ushawishi kwenye chama/Kofia zake zote za kimamlaka kubadiri katiba ili kuongeza vipindi vingine vya kuongoza lakini hakuthubutu kufanya japo kauli za watu fulani fulani kutaka aendelee zilikuwapo huku na kule kama ambavyo zilikuwapo wakati wa Hayati Mwl J.K.Nyerere,Alhaji Mzee A.H.Mwinyi na Hatimae Mzee B.W.Mkapa.

Si kazi rahisi kuachia enzi kuu kama ya urais wa nchi yenye vinono vya kiuongozi japo pia ni mzigo mzito mnoo.Rais wa JMT ana mamlaka makubwa sana tena sana kikatiba yahusuyo mamlaka,nguvu na uweza wa utendaji kazi zikiwepo amri,teuzi,maelekezo,kukata majina/kupitisha majina ya wanaotakiwa ama wasiotakiwa na taifa/nchi kiuongozi n.k.Umaarufu wa Dr. Jakaya Kikwete ndani na nje ya mipaka ya JMT si wa kubezwa kuzingatia ya kuwa ni juzi juzi tu alikuwa madarakani kama raia namba moja wa taifa lenye kuinuka katika nyanja nyingi za kifulsa,rasilimali {madini,mafuta,gesi,etc} na wingi wa ukarimu kwa wawekezaji na wageni mbalimbali.

Taratibu Mh. Rais JPM ameanza kuchomoza katika shughuri za kitaifa na kiplomasia kimataifa kwa kushiriki matukio ya kitaifa katika nchi jirani kama Rwanda kisha Uganda yamkini baadae Kenya n.k n.k. Haiba ya kisiasa hujiweka wazi kwa sasa mahari wanapokutana mh. Rais JPM na Mh.Dr. Kikwete kama ambavyo imejitokeza nchini Uganda{Hekima itumike kulielewa hili}.Dr.J.Kikwete bado amekuwa na mwonekano rasmi kana kwamba bado ni rais wa JMT na hili limekuwa likijidhihirisha maeneo kadhaa anakopita ama kunena jambo lenye mguso wa kimamlaka {Mfano:Alipotembelea daraja la Nyerere,n.k}.

Kwa desturi tumeshuhudia na tulishuhudia ukimya na utulivu mkubwa ktk tamalaki ya kimamlaka pale Mzee Mwinyi alipomwachia madaraka Mzee Mkapa,Vivo hivyo Mzee Mkapa alipomwachia madaraka Mzee Kikwete.Kwamba ilifika wakati Mzee Mkapa alikataa baadhi ya miariko/Ushiriki wa matukio/n.k kuepuka kuikwadha serikali {Rais} aliepo madarakani

Nadhani Mh. JPM na Serikali yake anapaswa kupewa nafasi pana zaidi katika kutekeleza/kujiachia/kujinafasi kiuongozi na majukumu yake yakinifu kimadaraka.Hivyo ni ushauri kwa marais waliomaliza vipindi vyao,waliostaafu kuwa wakimya,watulivu,wapole,ikibidi kujichimbia mahari ambako awatavuta attention ya namna yeyote kuepusha mgongano wa nguvu/mwangwi/vigelegele vya madaraka.

Yawezekana nakashindwa kueleweka kwa baadhi ya wabobezi ktk uandishi ulionyooka,hata hivyo nina imani kubwa ujumbe wangu yawekekana umeeleweka
Huna hoja kaa chini.....
 
Binadamu hawakosi neno! Akiamua kukataa Mialiko mtakuja na story za CCM yapasuka, Rais Kamtuma China mnataka awe mtovu wa nidhamu akatae? Kuhusu ile picha aliyokuwa na Kenyata na Magu msishangae ile ndo haiba yake popote wenye watatu yeye ndo anawapigisha story wenzie na wenzie huishia kutikisa Mbavu.
Mkubali mkatae Jakaya ana mvuto sana pamoja na jitihada kubwa ya kumsakama bado popote anapokuwepo ana shine!
 
tatizo wakati alipokuwa madarakani hakufanya kazi yake kwa ufasaha anatamani arudishe siku nyuma ili atumbue majipu lakini haiwezekani na ukiangaliaMagufuli anafuta nyayo zake taratibu kwa kuondoa wale watendaji mizigo ila mwisho wa siku atasahaulika kabisa
 
Unajua unapomkabidhi gari lena akuendeshe unakuwa haumuamini mara kila saa utakamata usteling, gia n.k ili tu kuhakikisha mnafika salama... Hiyo mentality hata kwenye politics ipo...
 
tatizo wakati alipokuwa madarakani hakufanya kazi yake kwa ufasaha anatamani arudishe siku nyuma ili atumbue majipu lakini haiwezekani na ukiangaliaMagufuli anafuta nyayo zake taratibu kwa kuondoa wale watendaji mizigo ila mwisho wa siku atasahaulika kabisa

Taifa linasumbuliwa na Foleni za sukari sio Nyayo za Jakaya! Hizo jitihada za kufuta nyayo zake tumieni kuvamia magodown ya sukari!
 
Vijana wa chadema na midomo wazi muda wote kama domo la lisu vile sasa mnataka rais amtume lowassa akajinyee kwenye gari
 
Vijana wa chadema na midomo wazi muda wote kama domo la lisu vile sasa mnataka rais amtume lowassa akajinyee kwenye gari
 
kwa hulka za jk,mtasubiri sanaa ili kumuona akiwa anakatiza mitaa ya msoga pekeee,labda baada ya jpm kuondoka madarakani.
 
Sawa ni vizuri JK akaacha ku mu over shadow JPM,lakini.
1.Tunaambiwa kuna kazi anaombwa na JPM kuzifanya au kumuwakilisha JPM,je akatae?.

2.Saa zingine JK anaponzwa na haiba yake.JK ana haiba Kali sana, akisema au akitokea mahali ana mfunika kila mtu. Ni vizuri siku ya uzinduzi wa daraja hakuwepo, maana angekuwepo, wengine wasinge onekana kabisa.
3.Mitandao ya kijamii pia inachangia sana kumfanya JK aonekane kama bado yupo in power. Maana kila kukicha JK hivi JK vile. Ni kama vile watu wanashindwa ku deal na JPM badala yake wanatupa hasira zao kwa JK.
Hamna chochote!!!!
 
Back
Top Bottom