Mzanzibari ni nani?

Mzanzibari ni nani?

jMali

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2010
Posts
8,412
Reaction score
5,012
kila siku tunasikia "wazanzibari" wanadai hiki na kile, hususani kwenye katiba mpya, je wazanzibari ni kina nani hasa? Tuzingatie mifano kama: Rais ali hasan mwinyi kazaliwa bagamoyo lakini ni mzanzibari, Dr shein mzaliwa wa pemba ni mzanzibari, Mmasai, mchaga au "mbara" yoyote atayehamia zanzibar na kukaa miaka kadhaa naye anapewa uzanzibari (kama rais mwinyi).
Hivi mpemba aliyezaliwa bara na kukulia bara anaweza kuwa mzanzibari automatically tu kwa sababu babu yake alizaliwa zanzibar? au yeye atakuwa mbara?
Na je mbara aliyehamia zanzibar akawa mzanzibari (kisheria), akirudi bara na kuzaa watoto, hawa "wanyamwezi" nao watakuwa wazanzibari vile vile? Naomba tusaidiane.
 
Mzanzibar ni aliezaliwa Zanzibar au alizaliwa nje ya Zanzibar na kupewa Uraia wa Zanzibar.
 
Ni swali la msingi sana na jibu lake linategemea katiba ya zanzibar na sheria zake zinamtaja mzanzibari ni nani. Mimi sifahamu ila nadhani katiba ya zanzibar itakupa jibu.
 
Hivi visiwa ni shida tupu. Kuna kiongozi kutoka Zanzibar aliwahi kuwaambia Wazanzibar kuwa 'vichwa/akili kama samaki'. Hiyo kauli naikumbuka,aliyesema nimemsahau.
 
kila siku tunasikia "wazanzibari" wanadai hiki na kile, hususani kwenye katiba mpya, je wazanzibari ni kina nani hasa? Tuzingatie mifano kama: Rais ali hasan mwinyi kazaliwa bagamoyo lakini ni mzanzibari, Dr shein mzaliwa wa pemba ni mzanzibari, Mmasai, mchaga au "mbara" yoyote atayehamia zanzibar na kukaa miaka kadhaa naye anapewa uzanzibari (kama rais mwinyi).
Hivi mpemba aliyezaliwa bara na kukulia bara anaweza kuwa mzanzibari automatically tu kwa sababu babu yake alizaliwa zanzibar? au yeye atakuwa mbara?
Na je mbara aliyehamia zanzibar akawa mzanzibari (kisheria), akirudi bara na kuzaa watoto, hawa "wanyamwezi" nao watakuwa wazanzibari vile vile? Naomba tusaidiane.

Kasome katiba ya znz utapata jibu sahihi sio la mitaani.
 
Mzanzibari n mtu anaenyanyaswa sna mtanganyika kwenye kivuli cha muungano
 
Dah ukikaaa hapa miezi kadhaa unakuwa Mzanzibari. ...
 
mtu aliyezaliwa Pemba ama ugunja huyo ndo mzazibari ama wazazi wake wana asili ya huko
 
Mzanzibari ni mtu aliezaliwa katika visiwa vya zanzibar au alieishi kisheria zanzibar kwa miaka kumu mfululizo au mmoja ya wazaziwake ni mzanzibari wa kuzaliwa.

Zanzibar ni Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo vilivyo zunguka visiwa vya Unguja na Pemba
Kama vile visiwa vya tumbatu kojani mtambwe.nk.
 
Mzanzibar ni aliezaliwa Zanzibar au alizaliwa nje ya Zanzibar na kupewa Uraia wa Zanzibar.

zanzibar haina kitu kinaitwa uraia kwa sababu si nchi, uraia ni wa tanzania. labda unataka kusema ukazi?
 
Mpemba+muunguja. Sijui kama kuna mwingine
Hapo umetaja wakazi wa visiwa viwili tu Unguja na Pemba ,vipi kisiwa cha Tumbatu,wale sio wazanzibari?au kisiwa cha kojani wale pia nao sio wazanzibari?Au hujui kuwa Zanzibar ni muunganiko(archipelago) wa visiwa takriban 50 na kati ya hivyo kuna zaidi ya 5 ni makazi ya watu?
 
Mzanzibar ni mzaliwa wa Pemba na Unguja kwa mujibu wa katiba ya taifa la Zanzibar.Mzanzibar huyo huyo ana sifa nyingine ya ziada ambayo anaweza kuitumia kutegemeana na mazingira husika Mzanibari ni mTanzania lakini Mtanzania (Mtanganyika) si mzanzibar hata kidogo kwasababu haweza kumiliki ardhi Zanzibar,hawezi kugombea nafasi ya uongozi Zanzibar,hana sifa ya kuchagua au kuchaguliwa akiwa katika nchi ya Zanzibar.

Kwajinsi Sitta anavyolipeleka hili bunge la katiba uchwara naona sifa hizi zikiendelea kuwepo katika katiba mpya.
 
mke wangu anamimba nataka aende akajifungulie zanzibar;
je mtoto akizaliwa atakuwa mzanzibar????
 
Mzanzibari ni mtu aliezaliwa katika visiwa vya zanzibar au alieishi kisheria zanzibar kwa miaka kumu mfululizo au mmoja ya wazaziwake ni mzanzibari wa kuzaliwa.

Zanzibar ni Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo vilivyo zunguka visiwa vya Unguja na Pemba
Kama vile visiwa vya tumbatu kojani mtambwe.nk.




mkuu vp kuhuhu kisiwa cha mafia?
 
Hivi visiwa ni shida tupu. Kuna kiongozi kutoka Zanzibar aliwahi kuwaambia Wazanzibar kuwa 'vichwa/akili kama samaki'. Hiyo kauli naikumbuka,aliyesema nimemsahau.

Hakuwaambia WaZanzibari Bali CCM Kama nyie ndio walioambiwa
 
Mtu yeyote Mtanzania ana haki Zote zanzibar, ile ili uwe na Kadi ZAN-ID japo uwe umeishi miaka 5 Zanzibar, kwa sasa Wachaga, Wasukumu, Wamasa, Wageni na makabila mengi ya Tanzania washachukua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom