Mwigulu Nchemba: Hawa wanaouwa sio Watanzania, ndio maana miili inapookotwa wananchi hawashtuki

Mwigulu Nchemba: Hawa wanaouwa sio Watanzania, ndio maana miili inapookotwa wananchi hawashtuki

Kwani tunapopeleka majeshi ya amani nchi jirani huwa tunakwenda kuwalinda nani kama vifo vya jirani zetu wasio na hatia havituhusu
 
Tangu apewe hiyo wizara naona upeo wake unazidi kudidimia kila kukicha.
Kwa hiyo anataka tuandamane ndio ajue kuwa tunaumizwa na miili inayootwa ufukweni kila kukicha?

Maandamano yenyewe yamepigwa marufuku. Sijui hizo kelele mtazipigaje?
 
Waziri Mwigulu Nchemba amesema yapo matukio yanayofanyika kwa ajili ya kuchafua taswira ya nchi na ndio maana dot zinazounganishwa ni nyingi mno

Amesema inapotokea miili inaokotwa baharini, bahari ambayo tunachangia na nchi nyingi sana ambayo upepo unaweza kusafirisha miili kutoka sehemu mbali, basi watu wanasema watu wanauawa ovyo

Amesema haiwezi watu wakawa wanauawa hovyo na kukawa shwari kama kulivyo, watu wangepiga kelele kwa sauti

Ameendelea kusema kila tukio linapotokea serikali inachukua hatua na maisha ya watu yanapopotea sio vyema kuhusisha siasa, maana maisha yana thamani sana


Huyu Hanna kitu,ni mchumia tumbo,uzalendo wake ni kuvaa skafu tuu basi.Ni mtu mwoga,kinyonga wa hali ya juu,haaminiki ni ndimi mblili kila kukicha
 
Maiti zinaokotwa, watu wanapotea. Hivi watu hawajapiga kelele kuhusu ndugu zao kupotea? Labda anamaanisha, kwa nini hawaandamani.
 
Waziri Mwigulu Nchemba amesema yapo matukio yanayofanyika kwa ajili ya kuchafua taswira ya nchi na ndio maana dot zinazounganishwa ni nyingi mno

Amesema inapotokea miili inaokotwa baharini, bahari ambayo tunachangia na nchi nyingi sana ambayo upepo unaweza kusafirisha miili kutoka sehemu mbali, basi watu wanasema watu wanauawa ovyo

Amesema haiwezi watu wakawa wanauawa hovyo na kukawa shwari kama kulivyo, watu wangepiga kelele kwa sauti

Ameendelea kusema kila tukio linapotokea serikali inachukua hatua na maisha ya watu yanapopotea sio vyema kuhusisha siasa, maana maisha yana thamani sana


Kwa hiyo anakubali ameshindwa kaziiii.. maana sijasikia wakikamatwa.. basi ajiuzulu
 
sasa mbona hiyo miili inayopatikana baharini tayari inakuwa na ndugu Tanzania?, anataka kusema hao ndugu ni wakimbizii nao? "We are here in order to handle shit like this" hiyo press arudie atueleze vzur hapo ni kujisafisha huku unalinda tumbo
"""Njaa ni mbaya sana"""
 
"Amesema haiwezi watu wakawa wanauawa hovyo na kukawa shwari kama kulivyo, watu wangepiga kelele kwa sauti"
Kweli kabisa....maana yako ipo hapa ndugu kiongozi....ushwari huu nawe unaushangaa ila kwa nafasi yako huwezi kuwaambia wafanye nini. Kazi kwetu wabongo
 
Huo upepo unaoleta miili unavuma kuja huku tu au na kwa wengine unakwenda.
Makelele anayotaka watu wapige kuzidi haya ya sasa ni ya aina gani. Waendelee tu, siku panic button ikibonyezwa ndo akili itamrudia.
 
Hapa ndipo napoaanza kuushangaa uzalendo wa viongozi wetu, hapa ndipo naposhangaa uwezo wa kufikiri wa viongozi wetu, waziri unajibu hoja ya mauaji as if ni hoja kuchapwa mtoto shule, majibu myepesi kama mtoto wa form two,
Ulitaka ajibu upendavyo wewe?, acha ujinga ,ni kweli kwani hatuchangii bahari,?,maiti haziwezi safirishwa na maji toka sehemu moja kwenda nyingine?
Acheni kuharibu taswira ya nchi, pambaneni kisera nyie
 
Swali la kumuuliza hili hapa.

Hiyo bahari iliaanza kuwepo baada ya utawala huu au ilikuwepo toka enzi zote? iweje sasa hivi miili iwe inaokotwa kila uchwao?
Nini kimeongezeka ni upepo unaenda kasi ya ksulisuli? tunauliza samaki papa na nyangumi wanakuwa wapi mpk wasubiri miili ije ilundikwe COCO beach.....

Mungu anakuona Nchemba
 
Swali la kumuuliza hili hapa.

Hiyo bahari iliaanza kuwepo baada ya utawala huu au ilikuwepo toka enzi zote? iweje sasa hivi miili iwe inaokotwa kila uchwao?
Nini kimeongezeka ni upepo unaenda kasi ya ksulisuli? tunauliza samaki papa na nyangumi wanakuwa wapi mpk wasubiri miili ije ilundikwe COCO beach.....

Mungu anakuona Nchemba

HAPO chacha
 
Anasema tusihusishe na siasa wakati yeye amejibu kisiasa.
 
Ulitaka ajibu upendavyo wewe?, acha ujinga ,ni kweli kwani hatuchangii bahari,?,maiti haziwezi safirishwa na maji toka sehemu moja kwenda nyingine?
Acheni kuharibu taswira ya nchi, pambaneni kisera nyie

Ingekuwa hivyo watu wanaozamaga coco beach ingekuwa hatuwaoni tena mbona tunawaonaga mnalani hujui chochote kuhusu bahar ww ni mara chache sana bahar kutupa mtu location ya mbali maana bahar haikai na uchafu
 
Hapa ndipo napoaanza kuushangaa uzalendo wa viongozi wetu, hapa ndipo naposhangaa uwezo wa kufikiri wa viongozi wetu, waziri unajibu hoja ya mauaji as if ni hoja kuchapwa mtoto shule, majibu myepesi kama mtoto wa form two,

Hivi unafikri hajuhi anachokiongea?

Kinachotokea ni kuwa anafikiri sote tunaupeo mfupi kama yeye.
 
Hiki ndio kilichonifaya nikaacha kwenda kusoma PhD, yaani ukiwa ni PhD holder basi unakua hivyo, sasa huyu nae ndio arguements gani amejenga hapo? Eti Dr. Mwigulu Nchemba !! Namkumbuka Prof. Victor Mlekwa kuwa unavyozidi kusoma ndio unavyozidi kiuwa mjinga
 
Waache waendelee kuzembea badala ya kukomesha hiyo hali, ipo siku tutawapigia hizo kelele wanazozitaka, hakuna askari wala risasi itakayoweza kunyamazisha kelele hizo.

Wasiombe tukafikia kikomo cha uvumilivu.....
Huyu naye ndo mwenye ushahidi atautoa hats mbinguni
 
Back
Top Bottom