Mwenyekiti wa CCM Dodoma ashangaa jina lake kutajwa kwenye list ya waliofoji vyeti

ECONOMY

JF-Expert Member
Apr 10, 2017
680
480
Habari za asubuhi wanajamii forum.
Leo kipindi nasikiliza magazeti radio .Nimesikia mwenyekiti wa CCM Dodoma anashangaa jina lake kutwajwa kwenye list ya waliofoji cheti cha elimu ya kidato cha nne ilihali yeye hajawahi kusoma elimu ya kidato cha nne.

========

Mwenyekiti CCM ashangaa kutajwa cheti feki cha kidato cha nne wakati hakusoma

Matokeo ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma yameibua mapya mengine.

Hiyo inatokana na mwenyekiti wa CCM wilayani Chamwino, Charles Ulanga kuhoji sababu za kutajwa katika orodha ya walioghushi vyeti vya kidato cha nne wakati hajawahi kusoma elimu ya sekondari.

Sakata la mwenyekiti huyo ni mwendelezo wa utata ulioibuka baada ya ripoti ya matokeo ya uhakiki huo ulioibaini wafanyakazi 9,932 wa Serikali na taasisi zake kuwa na vyeti vya kughushi, kutumia vya watu wengine au cheti kimoja kutumiwa na zaidi ya mtu mmoja.

Akizungumza na gazeti hili jana baada ya jina lake kuwa miongoni mwa wenye vyeti feki, Ulanga, ambaye pia ni Mratibu wa Elimu wa Kata ya Buigiri wilayani Chamwino mkoani Dodoma, alisema wakati wa uhakiki alipeleka cheti cha darasa la saba na cha ualimu daraja la tatu ‘A’.

“Nawashangaa wapi walipopata cheti cha kidato cha nne kwa sababu mimi nilipeleka vyeti viwili; cha darasa la saba na cha ualimu. Sasa hiki cha kidato cha nne walichokikuta feki sijui wamekitoa wapi?” alihoji Ulanga.

[HASHTAG]#Mwananchileo[/HASHTAG]
 
Habari za asubuhi wanajamii folum.Leo kipindi nasikiliza magazeti radio .Nimesikia mwenyekiti wa ccm Dodoma anashangaa jina lake kutwajwa kwenye list ya waliofoji cheti cha elimu ya kidato cha nne ilihali yeye hajawahi kusoma elimu ya kidato cha NNE.
Ndiyo maana amefoji Cheti, kwani unafikiri wanaofoji ni wale waliosoma kidato cha nne tu
 
Matokeo ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma yameibua mapya mengine.

Hiyo inatokana na mwenyekiti wa CCM wilayani Chamwino, Charles Ulanga kuhoji sababu za kutajwa katika orodha ya walioghushi vyeti vya kidato cha nne wakati hajawahi kusoma elimu ya Sekondari.

Sakata la Mwenyekiti huyo ni mwendelezo wa utata ulioibuka baada ya ripoti ya matokeo ya uhakiki huo uliobaini wafanyakazi 9,932 wa Serikali na taasisi zake kuwa na vyeti vya kughushi, kutumia kwa watu wengine au cheti kimoja kutumiwa na zaidi ya mtu mmoja.

Utata huo umeibuka mkoani Kigoma, ambako jina la mganga mkuu wa mkoa limetajwa, likionekana kutumiwa na mfanyakazi wa Hifadhi ya Gombe iliyoko Kigoma.

Akizungumza na gazeti hili jana baada ya jina lake kuwa miongoni mwa wenye vyeti feki, Ulanga, ambaye pia ni Mratibu wa Elimu wa Kata ya Buigiri wilayani Chamwino mkoani Dodoma, alisema wakati wa uhakiki alipeleka cheti cha darasa la saba na cha ualimu daraja la tatu 'B'.

"Nawashangaa wapi walipopata cheti cha kidato cha nne kwa sababu mimi nilipeleka vyeti viwili; cha darasa la saba na cha ualimu. Sasa hiki cha kidato cha nne walichokikuta feki sijui wamekitoa wapi?" alihoji Ulanga.

Mwenyekiti huyo alisema baada ya kumaliza darasa la saba aliomba kujinga na masomo ya ualimu kama utaratibu ulivyokuwa ukitaka wakati huo.

Alijiunga na Chuo cha Ualimu Bustani kilichopo wilayani Kondoa mwaka 1980 na kutunukiwa cheti daraja la tatu "B".

"Wakati ule ulikuwa unaomba kwenda darasa saba niliomba kwenda chuo cha ualimu nikakubaliwa nikaenda Bustani na nilipata cheti cha ualimu daraja la tatu "B", alisema Ulanga.

Alisema waliohitajika walipaswa kuwa wawe wamemaliza kidato cha nne ili wasomee ualimu na ndiyo waliohitimu ualimu wa daraja "A". Nitakwenda huko huko Utumishi (Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) waniambie wapi walikotoa hicho cheti cha kidato cha nne walichokihakiki", alisema.

Ulanga pia anakabiliwa na utata mwingine kuhusu utumishi wa umma na nafasi ya kisiasa. Kwa kuwa mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Chamwino, Ulanga alitakiwa kuachia nafasi yake ya Mratibu wa elimu kwa kuwa Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Namba 1 wa mwaka 2015 unazuiwa mtumishi wa umma kugombea nafasi yoyote ya uongozi katika chama cha siasa kutokana na hali hiyo kusababisha mkanganyiko wa shughuli za siasa na Serikali na kuweka mwanya wa upendeleo katika utoaji huduma kwa wananchi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Athumani Masasi alipoulizwa kuhusu Mwenyekiti huyo atafutwe leo kwa ajili ya kulizungumzia.

Jumla ya watumishi 435,000 walihakikiwa. Rais John Magufuli aliagiza wote waliobainika kuwa na vyeti bandia waondoke kazini mara moja na atakayesalia hadi katikati ya mwezi ujao afikishwe mahakamani.



Chanzo: Mwananchi
 
Sasa hapa ndio utaona magumashi ya hili zoezi, serikali KURUPUFU sana hii kuwahi kutokea.

Kufanya vetting HAWAWEZI(ref Bashite and the like)

Kuhakiki vyeti HAWAWEZI

kuaajili HAWAWEZI,

kupandisha madaraja HAWAWEZI,

kuongeza mishahara HAWAWEZI,

kupanga mipango mizuri ya kuteka na kupoteza HAWAWEZI,

Kufanya purchasing zenye akili HAWAWEZI(ndege-terrible teens jeneza)

Wao wanaweza KICK na Kushushua tu.

Mungu awalaani sana waliohusika kwenye Bao la Mkono.
 
Mwenyekiti CCM ashangaa kutajwa cheti feki cha kidato cha nne wakati hakusoma

Matokeo ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma yameibua mapya mengine.

Hiyo inatokana na mwenyekiti wa CCM wilayani Chamwino, Charles Ulanga kuhoji sababu za kutajwa katika orodha ya walioghushi vyeti vya kidato cha nne wakati hajawahi kusoma elimu ya sekondari.

Sakata la mwenyekiti huyo ni mwendelezo wa utata ulioibuka baada ya ripoti ya matokeo ya uhakiki huo ulioibaini wafanyakazi 9,932 wa Serikali na taasisi zake kuwa na vyeti vya kughushi, kutumia vya watu wengine au cheti kimoja kutumiwa na zaidi ya mtu mmoja.

Akizungumza na gazeti hili jana baada ya jina lake kuwa miongoni mwa wenye vyeti feki, Ulanga, ambaye pia ni Mratibu wa Elimu wa Kata ya Buigiri wilayani Chamwino mkoani Dodoma, alisema wakati wa uhakiki alipeleka cheti cha darasa la saba na cha ualimu daraja la tatu ‘A’.

“Nawashangaa wapi walipopata cheti cha kidato cha nne kwa sababu mimi nilipeleka vyeti viwili; cha darasa la saba na cha ualimu. Sasa hiki cha kidato cha nne walichokikuta feki sijui wamekitoa wapi?” alihoji Ulanga.

[HASHTAG]#Mwananchileo[/HASHTAG]
 
Mratibu ajasoma secondary? Wanapeana kwa ukada tu?bora alivyooonyesha zoezi la.uhakiki limefanywa ndivyosivyo
 
Back
Top Bottom