Rafiki yangu askari wa wanyama alinipa stori hii kuhusu fisi:
'Watu wengi wanafikiri fisi ni mnyama mwenye via vyote vya uzazi:vya kike na kiume, kumbe siyo. Dhana hii inatokana na umbo la via uzazi vya fisi jike. Kinembe cha fisi jike kina uwezo wa kusimama kama kifaa cha
fisi dume. Watu wanapoona sehemu ya fisi jike imesimama kama uume, wanafikiri fisi jike huyo ana vifaa vya kiume, kumbe si hivyo. Jike ni jike na dume vivyohivyo kama walivyo wanyama wengine.
Habari hii niliyosimuliwa na askari nyamapori naikumbuka mpaka leo na nadhani mleta mada ameielewa.