Mwenge wa uhuru kuzindua baa!!

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
2,334
Reaction score
3,567
Siku ya tarehe 12-07-2018 majira ya asubuhi nilikutana na adha kubwa ya usafiri maeneo ya mbezi goba. Nilipouliza nini sababu ya hiyo adha, nikajibiwa kwamba mwenge wa uhuru unaweka jiwe la msingi kwenye baa iliyopo karibu sana na barabara hivyo wamelazimika kuiblock barabara. Je ni halali mwenge uzindue hadi baa!!??
 

Serikali ya viwanda mkuu, ukute bar nazo zimekuwa upgraded kama ilivyokuwa kwenye vyerehani na saluni.
 
so long as those bar contribute towards national income improvement, sioni ajabu ya mwenge wa uhuru kuwepo pale

KIM JONG UN-LUMUMBA (Ila kwa sasa nipo Tazara hapa kwa MFUGARE FLY OVER)
 
Uliuliza bar ni ya nani? Kama ni mradi wa serikali ya mtaa au kijiji wenye lengo la kukusanya mapato hakuna maajabu ni sahihi!!
 
Mkuu.. Ulipata Nafasi Ya Kwenda Kushuhudia/Kujiridhisha Ulichoambiwa Au Uliridhika Na Hearsay..
 
Taarifa yako haina ukweli, tarehe 12 Julai 2018, MWENGE uliamkia MBAGALA Zackeem ambako ulikesha pia asubuhi hiyohiyo MWENGE ulikabidhiwa kwa uongozi WA mkoa WA Pwani eneo LA Kongowe mpakani Temeke na Mkuranga. Mkianza kudanganya ujaribu kuwa makini katika kuweka kumbukumbu
 
mwenge wa uhuru una " philosophy " zake ukikuta unazindua miradi binafsi jua philosophy hazifuatwi. ni ukasuku.
 
Nini bar hata guest house unatakiwa uzindue kwasababu ni biashara halali na inaliingizia taifa pato kupitia kodi, ajira na huduma kwa raia. Kwa taarifa yako wanywaji ndio wanachangia kiasi kikubwa sana pato la taifa kupitia unywaji wao. Wasipokunywa viwanda vitafungwa hivyo kupoteza ajira nyingi sana, kodi na viwanda kufa. Ukiona mtu katoka bar anayumba yumba msaidie kwani ametoka kuchangia pato la taifa tena kwa kutumia bidhaa zinazozaliwa na viwanda vyetu vya ndani. Hapa ni suala la mind set change tu.
 
Siyo kweli,ni poroja tu hiyo.
mwenge wa uhuru huwa unaweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo ya taifa tu
 
Hivi unajua walevi wanachangia kiasi gani serikalini.. Mleta thread bhana
 

Kwa awamu hii kila kitu kinawezekana mkuu.
 
Hakuna mradi wowote uliozinduliwa na Mbio za mwenge uliodumu hata miezi 6 , hiyo bar ijiangalie
 
Kuzindua Bar na Guest House mbona kawaida siku hizi??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…