Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Mwendawazimu akimbiza watu Benki | |
Friday, August 05, 2011 12:26 PM WAFANYAKAZI wakiwemo wateja waliofika jana Benki ya CRDB, tawi la Azikiwe walijikuta wakikimbia huku wengine wakianguka kwa presha kufutia kijana mmoja aliyekadiriwa kuwa na upungufu wa akili kurusha mawe kwenye vioo vya benki hiyo. | |
Majira ya mchana jana tukio hilo lilitokea na kusababisha wafanyakazi na wateja waliokuwemo ndani ya benki hiyo kuanza kukimbia ovyo wakidhani wamevamiwa na majambazi. Huku baadhi ya wafanyakazi wakiacha majukumu yao na kulala chini huku wengine wakikimbia ovyo kwa kunusuru maisha yao bila kujua kilichokuwa kikijiri nje Hali hiyo ilifanya askari polisi kufyatua risasi hewani, ili kuzuia uharifu zaidi na ndipo kijana huyo alipoonekana akiwa katikati ya Barabara ya Azikiwe na Maktaba eneo la Posta Mpya akiendelea kurusha mawe kwenye vioo hivyo Ndipo kijana huyo alipokamatwa na kutiwa mbaroni japo alionekana si mwenye akili timamu huku baadhi ya watu wakidai kijana huyo ni mwendawazimu huku wengine wakidai ameathirika kutokana na utumiaji wa dawa za kulevya Kufuattia hali hiyo baadhi yawateja walizirai kwa hofu na wengine wakionekana wakilia kutokana na kupotelewa na nyaraka zao muhimu, fedha wakiwa ndani ya benki hiyo zikiwemo kadi na fedha taslimu. NIFAHAMISHE ilibahatika kuona mwanamke mmoja aliyekuwa ameanguka chini kwa hofu na hali yake iloikuwa tata kutokana na hali hiyo |