Mwema akiri uwezo wa Polisi mdogo

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Mwema akiri uwezo wa Polisi mdogo
Gloria Tesha
Daily News; Tuesday,January 13, 2009 @20:00​

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, amekiri kuwa uwezo wa Polisi kuhimili ajali za barabarani ni mdogo kutokana na askari wengi kushindwa kufanya kazi kwa umahiri na taaluma. Kutokana na hali hiyo, Mwema ameahidi kutoa tamko lenye mwelekeo wa namna walivyojipanga kuzuia ajali za barabarani nchini.

IGP alisema hayo jana katika taarifa yake ya mradi wa ujenzi wa nyumba mpya za makazi za polisi wa kambi ya Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye aliweka jiwe la msingi la ujenzi huo.

Mwema alisema alisikitishwa na taarifa za ajali ya juzi Tanga iliyosababisha vifo vya watu 28 na wengine 22 kujeruhiwa vibaya na ya Uchira, Kilimanjaro siku chache zilizopita na kusababisha vifo vya ndugu 11, kuwa ni ishara kwamba bado tatizo lipo.

Alisema matatizo hayo wakati mwingine hutokana na baadhi ya askari kutokuwa mahiri katika kufanya kazi kitaaluma, hivyo nia ya Polisi ni kuhakikisha mihimili yake mikuu ambayo ni Weledi, Usasa na Ulinzi Shirikishi, vinakuwa na tija kwa jamii.

Mwema alisema miongoni mwa mambo yanayopewa kipaumbele na Polisi ni kuhakikisha ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao, ikiwa ni pamoja na kulinda usalama wao barabarani kwa kuzuia ajali zitokanazo na uzembe wa ama madereva, abiria au polisi.

“Wakati tunafurahia maendeleo ya nyumba hizi za askari bado Watanzania wenzetu wanaendelea kupoteza maisha kwa ajali za barabarani, naweza kukiri kuwa bado kiwango cha kuhimili ajali za barabarani ni kidogo ila tunaendelea kushughulikia suala hilo ipasavyo,” alisema Mwema.

Akizungumzia suala hilo, Rais Kikwete alitumia fursa hiyo kuwapa pole walioguswa na ajali hiyo kwa kupotelewa na ndugu zao na majeruhi waliopo hospitalini na kuahidi kuwa Serikali inawajali wananchi wake, hivyo itaendelea kufuatilia na kusisitiza usalama barabarani.
 
Polisi shule kiduchu,na waliopo wenye shule zao wanaonewa gele na hao hao kina "Mwema".Utakakuta kakuu ka kituo kana shule ndooogo lakini akitokea askari wake kamaliza say ki diploma chake zinaanza chuki.

sasa wewe Mwema wewe ina maana hujui kuwa ili upewe huo u-tirafiki lazima uwe mtoto wa afande????polisi ovyoooooooooo
 
Au ni kukosa uwezo wa menejimenti, oganaizesheni na ubunifu miongoni mwa polisi.

Ninaamini wakati umefika wakuwa na polisi wasomi wachache lakini wanaoweza kutumia mbinu za kisayansi na kiteknolojia kuendesha majukumu yao.

Ninakumbuka siku moja tulibambikiziwa kesi na mwenye hoteli mmoja marehemu kwa hivi sasa, mimi na waandishi wangu kama 6 hivi.

Doh, kikundi cha polisi 20 pale Msimbazi walikuja kuandika stetimenti zetu kwa penseli na karatasi chafu! Kweli uwezo kama ndivyo, mdogo?

Ninafikiri tumekaa na vyombo na mifumo tuliyo nayo kwa muda mrefu na tunahitaji kuifumua na kufuma upya kulingana na wakati na mabadiliko yanayoendelea kutokea ndani na nje ya nchi.
 
ILISHASEMWA huwezi kumsaidia mtu asiyetaka kujisaidia mwenyewe. Ndugu yangu hapa unatwanga juisi kwenye kinu na kuchoma badala ya kukaanga chapati ya maisha!

Muda umekwisha na kilichobaki sasa ni mkakati wa Chama kimoja kisichokuwa na ukabila, udini, upendeleo na siasa za kinafiki kuvimeza vyama vingine vyote mbadala kwa mkakati wa kiainaaina bila vyenyewe kuwa na habari. Lakini kiongozi wa kfuanya hilo 2009 sioni. Wote watu wa njaa kali tu! Ngoja ruzuku itoke au isitoke uone watu watakavyohama upinzani mwaka 2009-2010!
 
Kama uwezo wa polisi ni mdogo by extension uwezo wa IGP nao ni mdogo aachie ngazi....
 
Back
Top Bottom