Mwelekeo wa Serikali kwa sasa

Mwelekeo wa Serikali kwa sasa

B22

Member
Joined
Mar 31, 2021
Posts
22
Reaction score
43
Naomba tujadili kidogo kuhusu suala la mwelekeo wa Serikali yetu kwa sasa juu ya kushughulika na kero za wananchi.

Je, ni kweli Serikali ya chama Cha Mapinduzi wameshindwa kuongoza nchi?
Je, CHADEMA wana sera nzuri zitazoweza kutuvusha na kusafisha pale CCM waliposhindwa?

Tuanze na maswali hayo mawili ndio yanaweza kutufanyq tukajenga hoja nzuri
 
Bi Mkubwa hana mwelekeo wowote wa taifa kwa sasa. Labda ziara za nje, na hamishahamisha ambayo nayo imefikia tamani. Msiseme sijawaambieni, sawa!?
 
Kwenye suala la tozo za miamala nimeamini maneno ya Diallo, kwamba serikali ya ccm haisikilizi hata maoni ya wana ccm.
Dawa ni kuwa na katiba mpya kwamba serikali ikiboronga inabadilishwa.
 
Mama yuko vizuri
CCM ikubali kumuondoa Spika/Naibu bila kumung'unya.

Pili baadhi ya mawaziri futilia mbali.
 
Je nini kifanyike ?
Sisi wenzenu mapema tushajua la kufanya. I hope wewe una akili timamu, sawa!??? Kama hujui la kufanya, basi endelea kuvumilia maumivu huenda yakaisha sooooooooooooooooooooooooooon!!! 🙂
 
Sisi wenzenu mapema tushajua la kufanya. I hope wewe una akili timamu, sawa!??? Kama hujui la kufanya, basi endelea kuvumilia maumivu huenda yakaisha sooooooooooooooooooooooooooon!!! 🙂
Naamini serikali imeishaweka kipaumbele chake kwa Sasa ...kuwa ni kujenga uchumi .
 
Naomba tujadili kidogo kuhusu swala la mwelekeo wa serikali yetu kwa Sasa juu ya kushughulika na kero za wananchi.....je ni kweli serikali ya chama Cha mapinduzi wameshindwa kuongoza nchi ? Je chadema wanasera nzuri zitazoweza kutuvusha na kusafisha pale CCM waliposhindwa? Tuanze na maswali hayo mawili ndio yanaweza kutufanyq tukajenga hoja nzuri
Mama yupo vizuri sana tu ila nafikiri waliopo chini yake siyo wazuri wengi yaani hawana uzalendo, fikiria kama Mbunge wenye mshahara wa zaidi ya ML 7 hachangii kodi,anaye changia kodi ni mtu wa chini kabisa ambaye hata mlo mmoja kwa siku ni shida ndiye anaye kamuliwa zaidi na wanao panga yote hayo ni wabunge na mawaziri husika.

Fikiria mkulima ambaye amelima kwa kujinyima mno kwa kutumia mfuko mmoja wa mbolea ya kupandia tshs lk70 mpaka lk1 lini anauza gunia moja la mahindi kwa shl 21000/-,na ndiye anaye lipia kodi.
 
Ukweli ni kwamba raisi Samia alikosea kupokea ushauri kwamba aondoe watu wote ambao waliteuliwa na hayati JPM.

Alichotakiwa kukifanya ni marekebisho katika idara na ikulu kama alivyofanya.

Hio imejidhihirisha wazi kwamba utekelezaji wa maamuzi yake mengi umetegemea sana ushauri wa watu ambao wana ajenda zao binafsi.

Na hiyo pia inajidhihirisha kwa kutengua uteuzi wa yule DC wa mahali fulani ambae hakuwa na sifa.

Sasa wale watu ambao yeye mama Samia aliwatoa kwa shinikizo la watu wenye ajenda zao, ndo walewale watu ambao huenda wapo nyuma ya figisufigisu zinazoendelea.

Kwa mfano mama Samia hakupaswa kutoa nafasi kule kwenye mkutano wa CCM kwa kusema " yoyote mtakayempendekeza mimi atanifaa" jambo lililotoa mwanya wa kumwondoa Dr Mpango kutoka wizara ya fedha, bila yeye kung'amua mpango ulokuwapo.

Kwenye hilo la kumwondoa Mpango pale hazina ni kosa la kiufundi ambalo haliwezi kurekebishwa hadi 2025.

Hawa watu watahakikisha wanamyumbisha hadi ikifika 2025 ambapo lile kundi ambao Mwanzo Mwaka yumo litakuwa linaanza kujitokeza kuanza kampeni ya uraisi.

Kwa watu kama mimi ambae ni mfuatiliaji wa mambo naona kwamba nchi kwa sasa ipo njia panda na mambo yatakuwa mabaya zaidi endapo litatokea jambo la kuhuzunisha huko mbele.

Nashauri kwa raisi Samia kusimama imara katika serikali yake ni kuachana na kundi lenye ajenda ambalo linamletea shida.
 
ngoja nkaupige mwingiii kisha ntarudi kuchangia hoja
 
Naomba tujadili kidogo kuhusu swala la mwelekeo wa serikali yetu kwa Sasa juu ya kushughulika na kero za wananchi.....je ni kweli serikali ya chama Cha mapinduzi wameshindwa kuongoza nchi ? Je chadema wanasera nzuri zitazoweza kutuvusha na kusafisha pale CCM waliposhindwa? Tuanze na maswali hayo mawili ndio yanaweza kutufanyq tukajenga hoja nzuri
Mkuu wewe unaonaje? Mwenye macho haambiwi "tazama".
 
Back
Top Bottom