Mwanza: Radi yaua wawili na bibi kujeruhiwa

Mwanza: Radi yaua wawili na bibi kujeruhiwa

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia na bibi yao kujeruhiwa baada ya kupigwa na radi katika Mtaa wa Bulola ‘A’, Kata ya Buswelu, wilayani Ilemela mkoani Mwanza.

mwananchi_official-20250808-0001.jpg

Soma pia:

Tukio hilo lilitokea jana Agosti 7, 2025 saa 7:30 mchana wakati mvua iliyoambatana na upepo na ngurumo kubwa ilipoanza kunyesha.

Hali hiyo ikitokea, Grace Kateti (52), ambaye ni mjasiriamali na mkazi wa Bulola, alikuwa akipika chakula cha mchana chini ya mti jirani na nyumba yao akiwa na wajukuu zake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amethibitisha vifo vya watoto hao Mwasi Michael (11), ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tano na Charles Michael (6), mwanafunzi wa darasa la pili. Walikuwa wakisoma katika Shule ya Msingi Bulola.

Kamanda Mutafungwa amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Sekou-Toure.

Amesema Grace, ambaye ni bibi wa watoto hao alijeruhiwa na anaendelea na matibabu katika Kituo cha Afya Buzuruga.

Chanzo: Mwananchi official
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom