Mwanamke anayechepuka ni hatari sana

Fall Army Worm

JF-Expert Member
Jan 8, 2015
19,331
14,259
"Mwanaume anaweza kuchepuka na bado akawa na upendo wa dhati kwa mke wake lakini mwanamke hawezi kuchepuka na akaendelea kumpenda mume wake kwa dhati.Nasema hivi kwasababu mwanaume hafanyi tendo la ndoa kwa hisia, mwanamke hawezi kufanya tendo la ndoa bila hisia mguso.Ndiyo maana wanaume wanahitaji mahali pa kufanya tendo la ndoa ila wanawake wanahitaji sababu ya kufanya tendo la ndoa.

Wanawake wengi wanaoenda mahakamani kudai talaka kwa waume zao ni wale wachepukaji,mwanamke asiyechepuka hawezi kwenda mahakamani kudai talaka isipokuwa kama mumewe atakuwa amezidisha unyanyasaji wa kimwili na kiakili kiwango cha kukaribia kumuua mkewe.

Wanaume hawawezi kubadili tendo la ndoa na upendo. Mwanaume anaweza kufanya tendo la ndoa na mwanamke lakini bado akawa hampendi-ndiyo maana wanawake wanaojikuta kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanaume waliooa wanaowapenda wake zao kwa dhati hupata tabu saana kupata kufurahia mahusiano hayo kwani huwa wanatumika tu na hao wanaume wenye ndoa zao.

Lakini pindi tu mwanamke aliyeolewa anapolala na mchepuko wake huanza hata kusimulia habari za siri kuhusu mume wake na anaweza pia kusema ni kwa namna gani anamchukia mume wake; anaweza hata kukubali kuchukua sumu kwa mchepuko wake ili amwangamize mume wake.

Kwa mwanaume tendo la ndoa na upendo ni vitu viwili tofauti kabisa, lakini kwa mwanamke tendo la ndoa na upendo ni vitu viwili vinavyoenda sambamba.Kwa mwanaume tendo la ndoa huja kwanza kabla ya upendo (matamanio) lakini kwa mwanamke upendo huja kwanza kabla ya tendo la ndoa (upendo wa dhati); kwahiyo pindi mkeo anapoanza kuchepuka upendo wake huhama kutoka kwako kwenda kwa mchepuko, anaweza hata kuanza kumpa chakula kizuri na mahaba ambavyo amekuwa akikupa wewe tu.

Mwanaume kuchepuka haimaanishi kuwa ameacha kumpenda mkewe la hasha!, ila siwezisema hivyo kwa upande wa mwanamke.Pindi mwanamke anapoanza kuchepuka anakuwa ametumbuki kimapenzi kwa mchepuko huo na maisha kwenye ndoa hayawezi kuwa sawa kamwe; na anaweza hata kumuua mmewe endapo tu atakuwa ameanza kuchepuka.

Mkeo akianza kuchepuka utakuwa mwanaume mwenye bahati sana endapo hautakufa ndani ya miaka 10.Tafiti zinaonesha kuwa 95% ya wanawake wanaochepuka huwaombea waume zao wafe haraka, ndiyo maana ni hatari sana kwa mwanaume kuendelea kuishi na mwanamke anaechepuka; vilevile ndiyo maana inashauriwa kila mahali hata kwenye Biblia kumtaliki mwanamke pindi tu anapogundulika kuwa amezini(amechepuka).

Mwanamke anaechepuka ni hatari kwa uhai wa mume wake kuliko hata wauwaji au silaha.Kuna wanawake wengi wachepukaji duniani hualika wauwaji usiku waje watoe uhai wa waume zao na askari hata ndugu wa mume hawawezi kugundua hilo kwani msibani huyo mwanamke atakuwa analia kwa uchungu wa kuigiza na kuficha maasi yake.

Ndiyo maana wanasaikolojia hukataza sana mwanamke kuchepuka kuliko mwanaume.Wanawake hawawezi kuhimili mitafaruku ya kihisia itokanayo na kuchepuka; ndiyo sababu wanaume watafiti na wenye uelewa mkubwa watajua tu kuwa mkewe ameanza kuchepuka kwasababu huanza kumdharau mmewe na hujaribu hata kumnyima mumewe tendo la ndoa kwa visingizio lukuki.

Tafiti zinaonesha kuwa 90% ya wanawake wanaochepuka hawafurahii tendo la ndoa na waume zao hapo mwanaume makini atagundua tu hasa tabia za mkewe zitakapobadilika kuhusiana na tendo la ndoa, lakini mwanaume zube hawezi kugundua hili ataendelea kuvumilia sababu dhaifu za kunyimwa unyumba mpaka atakapoondolewa duniani.

Mwanamke hawezi kuchepuka na mtu ambae hampendi, huwa wanaitoa mioyo yao kwa kila kitu, ndiyo maana huwezi kuamini maamuzi yao.Kichekesho kikitolewa wanawake wengi wanaocheka hawacheki eti kwa sababu kichekesho ni kizuri ila ni kwasababu huwapenda wale waliotoa vichekesho hivyo; na endapo hawakupendi hata kichekesho chako kingekuwa kizuri kwa kiasi gani hawatacheka, ila mwanaume akicheka kuhusu kichekesho fulani ni kwasababu kichekesho chenyewe ni kizuri lakini si kwasababu eti anampenda mchekeshaji hii ni kwasababu wanaume wana uwezo wa kukabili hisia.

Tafiti zinaonesha kuwa ndoa nyingi huanza kuyumba pindi mwanamke anapoanza kuchepuka.Kuna wanaume wengi wanaochepuka lakini bado wanawaonesha wake zao upendo wa dhati, ila ni vigumu kukuta ndoa imesimama na mambo yanaenda sawa huku mwanamke akiwa mchepukaji.

Ninarudia, karibia 100% ya wanawake wanaochepuka huwaombea waume zao wafe haraka au hulazimisha talaka ili wawe na uhuru wa kufurahia penzi la kwenye mchepuko, ila wanaume wengi hawawezi kuruhusu wake zao wa ndoa wanyanyaswe ama kwa vitendo au kwa maneno na michepuko yao, siku zote wanaume husimama upande wa wake zao.

Mwanaume anaweza kuchepuka na bado akampenda mkewe lakini mwanamke hawezi kuchepuka na bado akampenda mmewe.

Pindi mkeo anapoanza kulala na mwanaume/wanaume wengine ujue kifo chako ki karibu.
 
Mimi naona hii concept ya mwanamke kufanya tendo la ndoa kwa hisia badala ya tamaa ni sisi wanaume ndo tunataka iwe hivyo kwa sababu tunaogopa kuchapiwa ila ukirudi kiuhalisia mwanamke na mwanaume wote ni sawa linapokuja suala la tamaa ya ngono.

Wote tuna tamaa tu ila mwanamke ameandamwa sana na jamii ndo maana inamuia vigumu kubadili mwanaume pale anapotamani jambo la tofauti.
 
Kuna siku atakuondoa katika USO wa Dunia ili awe huru zaidi. Anafuata mahaba ya kumridhisha huko nje, wewe ni kama boya, heri uondoke ila awe huru.
 
Mpaka sasa bado iko hivi?

NI Vile, Naona kama Binadamu wame mutate sana, Na kama Mioyo ya watu ilishakuwa baridi. Ila sawa, NImesikia.
 
Sku za mwsho upendo wa weng utapoa, na maas yataongezeka watu watajipenda wenyewe na kupenda pesa.......

Hii iko waz kila mtu akihitaj kitu hujifanya kupenda na akipata anachokihitaj bas uhalisia wake udhihirika, sasa hawa wanaokuwa na wanaume zaid ya mmoja ama wanawake zaid ya mmoja huwa hawana upendo bali wanafanya ili kuiridhsha nafs yake

Kamwe mtu(awe wakike ama wakiume, n mtu) hawez tumikia mabwana wawili lzma atampenda mmoja na kumchukia mwngne, ataambatana na mmoja na kumuacha(anaweza kuwa na we kimwli lkn kiroho asiwe nawe) mwngne

Usilete kusema wakiume ama n wakike, wote tuna moyo mmoja huez penda upendo wa dhat wotee.....lkn kama unampenda n kwann urukeruke kama ngedere.
 
SIKU MKEO AKIANZA KULALA NA MWANAUME MWINGINE JUA KIFO CHAKO KI KARIBU.......

"Mwanaume anaweza kuchepuka na bado akawa na upendo wa dhati kwa mke wake lakini mwanamke hawezi kuchepuka na akaendelea kumpenda mume wake kwa dhati.Nasema hivi kwasababu mwanaume hafanyi tendo la ndoa kwa hisia, mwanamke hawezi kufanya tendo la ndoa bila hisia
Hizi falsafa za mwanamke hatoi chezo mpaka apende zinatokaga wapi!?

Hamuoni mnaharibu mfumo wa ufikiri wa watu Kwa mitazamo mifupi mifupi kama hii!?.

Kwa makahaba napo mnasemaje!?

Asee sikubaliani na hoja ya kupenda na kufanya mapenzi kuw sambamba
 
Mm naona hii concept ya mwanamke kufanya tendo la ndoa kwa hisia badala ya tamaa ni sisi wanaume ndo tunataka iwe hivyo kwa sababu tunaogopa kuchapiwa ila ukirudi kiuhalisia mwanamke na mwanaume wote ni sawa linapokuja suala la tamaa ya ngono.

Wote tuna tamaa tu ila mwanamke ameandamwa sana na jamii ndo maana inamuia vigumu kubadili mwanaume pale anapotamani jambo la tofauti.
Bro naungana na wewe
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom