Mwanafunzi auwawa kisa kakataa kuolewa!

Mwanafunzi auwawa kisa kakataa kuolewa!

MAKOLE

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2012
Posts
618
Reaction score
280
Habari kutoka Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro zinasema kwamba Mwanafunzi MWAJUMA A. VUZO wa kidato cha Tatu katika shule ya sekondari Makanya amepigwa na baba yake mzazi hadi kusababishiwa maumivu makali na hatimaye Jumamosi ya tarehe 14/2/2015 alifariki dunia na kuzikwa leo 16/02/2015.

Habari zinasema kwamba Baba Mzazi wa mtoto huyo aliamua kumpiga binti yake kwa sababu ya kukaidi amri ya mzazi huyo ya kumtaka aolewe, jambo ambalo marehemu alilipinga kwa kuwa alipenda kuendelea na masomo.

Aidha, kabla ya kifo chake, marehemu aliwahi kwenda shuleni baada ya kipigo ambapo alianguka ghafla na akapelekwa Hospitali ya wilaya ya Same ambapo alipatiwa Rufaa kwenda KCMC na kugundulika kuwa maini na vitu vingine vya ndani viliharibiwa vibaya hali ambayo ilisababisha atapike mapande ya damu.

Baba wa marehemu ametoroka na hadi sasa hajapatikana na msako mkali unaendelea. Tunamuomba Mungu ailaze roho isiyo na hatia ya mwanafunzi Mwajuma
 
Poleni dada zeta mnaopigania elimu, hii damu ya huyu mwanafunzi iwe chachu ya kupigania elimu ya mtoto wa kike,
 
Huyo dada hajui utamu wa bamia lait kama agekuwa anajua asigefanya hayo maamuzi.

taip donkey kabsa huyu dada.
 
Allah ailaze roho ya marehemu mahala pena peponi Amen.


Muuaji ambaye ni baba mzazi wa marehemu asakwe na akipatikana auwawe na yeye am a afungwe maisha.
 
Inasikitisha...mwenyezi ampe punziko lililo jema...poleni familia,sheria ifuate mkondo.
 
wazaz wengine bhana hapo ni mbuzi mbili na debe la dengelua limefanya kamtoa mwanae roho
 
Sidhani kama ni baba yake mzazi huyo. Lazima atakuwa wa kufikia tu.
 
Huyooo atakuwaa baba mlezi maana uchungu wa mwana ajuae mzazazii wa really
 
Ni tamaa ya mali na pesa vimemponza baba. Mi naona mahari ifutwe.
 
Back
Top Bottom