Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,657
- 218,147
Anord Swai mkazi wa Dodoma , kijana aliyekataa kukubali bendera ya Chadema kushushwa kwenye kijiwe cha boda boda na wanaccm , alivamiwa na kupigwa tofali la kichwa , ambapo pamoja na kushambuliwa bado alipambana na kuhakikisha bendera haishushwi kibwege.
Baada ya kulidhibibiti kundi kubwa la wanaccm wenye visukari na BP akiwemo Aden Rage , majeruhi huyo alikimbizwa hospital ya mkoa na kushonwa utitiri wa nyuzi na kuruhusiwa .
Lakini sasa imegundulika kwamba kumbe alipata tatizo kubwa kwenye ubongo na ameshauriwa kupumzika na kutofanya shughuli yoyote kwa angalau kwa miezi 6 , mtu huyu ambaye shughuli yake ni udereva wa boda boda huku akiwa na familia yake maharamia wameamua kumletea dhiki nyumbani kwake , kuna haja ya jamii kuingilia kati .