Mwana CHADEMA apata ajali mbaya muda huu - Arusha

Mwana CHADEMA apata ajali mbaya muda huu - Arusha

mtendaji wa kijiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2012
Posts
533
Reaction score
115
Maeneo ya Ngarenaro kituo cha polisi, kuna kijana anayekadiriwa kuwa na miaka 35 amepata ajali kwa kugongwa na gari ya mizigo. Kijana huyo anasadikiwa kuwa ni mwanachadema kwani alikua amevaa kombati za CHAMA Na pikipiki yake ilifungwa bendera ya Chama.

Aidha hatukuweza kutambua jina kwa maramoja kwani hakuweza kuongea. Tayari Polisi wamemwandikia pf3 na mda huu anapelekwa hospitali.

Nawaomba vijana wenzangu wa CDM kupunguza Munkari wa shamrashamra ili mwenyez Mungu akijalia kesho tar 22 tukampokee Kamanda Lema kwa pamoja.

Peoplez
 
nimepita hapo sasa hivi ni msongamano mkubwa kuja hapa Narok Pub..ila kweli they need to slow down.
 
Pole sn kijana mwenzetu, unaonyesha ni kwa jnc gani unakerwa sn na uozo wa mafisadi wa taifa hili, Mungu akujalie upate afya njema na hatimaye urudi tupambane jm kawaida.
 
Mungu atamponyesha hata hiyo kesho ataungana na wenzake,vijana waende taratibu kwani huu mwisho wa mwaka una mambo mengi sana so ili tuweze kumpokea Kamanda twende kwa umakini ziadi kwani Tulianza na Mungu na Tuko naye hadi leo wakati wa ushindi na tutazidi kuwa nae daima dawama.Wao Magamba na mipesa yao sie Chadema na Mungu wetu aliye hai.Peoples Power
 
Nawaomba Vijana kuwa makini hasa wakati huu aw siku kuu. Taifa linawahitaji. Pole na Mungu akujalie upone haraka.
 
Navunja nguvu ya mauti. Kamanda amka, simama tayari kwa kumpokea kamanda wako kesho.
 
Pole kamanda, chezea kupata haki wewe lazima mzuka upande.
 
MUNGU amponye mwenyewe mpiganaji wetu!

Na bila shaka tutamjua tu!
 
Back
Top Bottom