Mwalimu Mwakasege: Corona ndio Tauni kwa mujibu wa Biblia

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
85,000
143,680
Mwalimu Mwakasege amesema wanadamu wanapaswa kujihoji ni wapi tumemkosea Mungu kisha tutubu na kumrudia.

Mwakasege amesisitiza kuwa hii Corona siyo mpya bali ni ile Tauni iliyosemwa katika Biblia takatifu.

Mwalimu Mwakasege amesema hayo wakati wa semina inayoendelea huko Njiro Arusha na kesho ndio siku ya kufunga semina.

Source Upendo tv!
 
Kama hajasoma historia ninamkumbusha tu kuwa dunia kupitia nyakati ngumu haijaanza leo. Yapo magonjwa yaliua 20 millions per year, mengine 50 millions per 5 yrs. Mengine 250 millions per few years.
Corona ndani ya nusu mwaka imeua laki 3 tu licha ya idadi kubwa ya wanadamu kwasasa ukilinganisha na miaka hiyo.
 
Hawa matapeli kumbe bado wapo na kushindwa kuponyesha corona? Ona linavyopotosha , plague/Tauni inaletwa na bacterium Yersinia pestis , corona ni virus, wapi na wapi!
Bado utapeli umejichimbia kwenye vichwa vyao
 
Kwanza tauni ni plague sio corona na kama hii hali ya sasa ndo hio iliyotabiriwa....... hii tauni yenyewe ya enzi hizo ilikua ni kitu gani kwenye biblia?
 
Kwa mujibu Wa Mwl Mwakasege kama umesikiliza vizuri..alichosema ni kuwa kwenye biblia Tauni inamaanisha ugonjwa wowote unaoambukiza haraka na akalinganisha na Corona kwa sasa na bado ameongeza kwa kusema kuwa yeye anasimamia neno na si sayansi yetu hii ambayo ukitafsiri wote tutasema kuwa ni plague na organism ni Yersnia kama mdau alivyosema juu hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Corona siyo tauni waache kulisha watu matangopori.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…