Waziri Simbachamwene anajaribu kuwauzia wana Mtwara mbuzi ndani ya gunia.
"Baada ya gesi kuanza kuzalishwa na kuuzwa, kazi ya wananchi wa Mtwara kupitia halmashauri zao za wilaya itakuwa ni kusoma mita kuangalia kiasi gani kimekwenda Dar es Salaam na kimeingiza fedha kiasi gani na kukokotoa asilimia zao ambazo lazima zirejeshwe kwa ajili ya maendeleo yao," alisema Simbachawene
Hivi tatizo la umeme Tanzania linatokana na kutokuwepo Bomba la gesi toka Mtwara???
Kweli Serikali ya CCM ina vituko vya mwendawazimu.
"Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene amesisitiza kuwa mgogoro na vurugu zinazoendelea mkoani Mtwara kuhusu gesi unachangiwa na wanasiasa.Alisema kuwa watu hao aliodai wanakosa uzalendo na utaifa, wanalenga kuhakikisha tatizo la umeme linaendelea kuwepo nchini hadi uchaguzi mkuu ujao ili wapate ajenda ya kisiasa jukwaani."