Mvua ya leo ni dalili mwezi uliandama jana

kipapi

JF-Expert Member
Sep 13, 2016
1,056
1,374
Wakuu habari za swaum,

Kwa wale waliofunga kama mimi na eid Mubarak kwa wanaokula sikukuu siku ya leo. Ama kwa hakika mimi kwa mtazamo wangu kwenye suala la muandamo wa mwezi naona leo (Jumapili) ilipaswa iwe sikukuu kwa dalili na sababu zangu zifuatazo;

1.Mvua inayoendelea kunyesha leo ni dalili kabisa ya kuwa mwezi umeandama jana, wajuzi wa mambo ya mwezi wamenithibitishia kuwa mwezi uliandama ila haukuonekana, leo asubuhi nilionana na mzee mmoja mashuhuri kwa shughuli za uvuvi pale ferry sokoni akanambia kwa ufupi tu "kwa dalili za Jana mwezi uliandama ila haukuweza kuonekana" na kwakuwa Tanzania kuna baraza kuu yaani (BAKWATA) kiitifaki tunabidi tusubiri tamko lao kama ilivyo ada maana ukiipinga BAKWATA sawasawa na kuipinga serikali.

2.Ikiwa kitovu na chimbuko la uislam, alipozaliwa mtume Muhammad (S.A.W), ilipoteremshwa Qur'an tukufu katika nchi ambayo ndio tunaenda kufanya hijja na nchi ambayo baadhi ya miji yake imetajwa mpaka kwenye Quran leo hii wanakula Eid el Fitr.

Hitimisho:
Tuendelee kuzingatia itifaki maana leo uonekane usionekane lazima kesho tule Eid maana tunasubiri kuonekana sio kuandama.
 
Hiyo namba 2 sio sababu ya msingi,kuonekana kwa mwezi kunategemea nchi na nchi,haina maana eti Saudi arabia ikiwa Eid basi dunia nzima iwe eid,tunaambiwa "fungueni/kuleni sikukuu mnapouona mwezi umeandama"
Hatukuambiwa tuifuate Saudi arabia,ndio maana utaona leo Saudi arabia ni Eid ila majirani zake kama Oman leo sio Eid.
 
Hiyo namba 2 sio sababu ya msingi,kuonekana kwa mwezi kunategemea nchi na nchi,haina maana eti Saudi arabia ikiwa Eid basi dunia nzima iwe eid,tunaambiwa "fungueni/kuleni sikukuu mnapouona mwezi umeandama"
Hatukuambiwa tuifuate Saudi arabia,ndio maana utaona leo Saudi arabia ni Eid ila majirani zake kama Oman leo sio Eid.
Itauona leo lkn mwez utakaouona leo sio wa leo ni wajan nyie ngojen mwez wa bakwata
 
Wakuu habari za swaum,

Kwa wale waliofunga kama mimi na eid Mubarak kwa wanaokula sikukuu siku ya leo. Ama kwa hakika mimi kwa mtazamo wangu kwenye suala la muandamo wa mwezi naona leo (Jumapili) ilipaswa iwe sikukuu kwa dalili na sababu zangu zifuatazo;

1.Mvua inayoendelea kunyesha leo ni dalili kabisa ya kuwa mwezi umeandama jana, wajuzi wa mambo ya mwezi wamenithibitishia kuwa mwezi uliandama ila haukuonekana, leo asubuhi nilionana na mzee mmoja mashuhuri kwa shughuli za uvuvi pale ferry sokoni akanambia kwa ufupi tu "kwa dalili za Jana mwezi uliandama ila haukuweza kuonekana" na kwakuwa Tanzania kuna baraza kuu yaani (BAKWATA) kiitifaki tunabidi tusubiri tamko lao kama ilivyo ada maana ukiipinga BAKWATA sawasawa na kuipinga serikali.

2.Ikiwa kitovu na chimbuko la uislam, alipozaliwa mtume Muhammad (S.A.W), ilipoteremshwa Qur'an tukufu katika nchi ambayo ndio tunaenda kufanya hijja na nchi ambayo baadhi ya miji yake imetajwa mpaka kwenye Quran leo hii wanakula Eid el Fitr.

Hitimisho:
Tuendelee kuzingatia itifaki maana leo uonekane usionekane lazima kesho tule Eid maana tunasubiri kuonekana sio kuandama.
Umefanya maamuzi yako kwa kutimiziza siku 29 nawa wasiku 30 nao leo watatmiza
 
Itauona leo lkn mwez utakaouona leo sio wa leo ni wajan nyie ngojen mwez wa bakwata
JF ni open forum inayojumuisha member toka nchi mbalimbali hapa duniani,acha kukariri kua kila mtu anaishi chini ya hiyo sijui Bakwata.
 
bb6d766cfc3b3da531d36c8ff681697c.jpg
karibun
 
Itauona leo lkn mwez utakaouona leo sio wa leo ni wajan nyie ngojen mwez wa bakwata
Wenzetu hawatumii macho ya binadamu kuuona mweziwbali wanatumia periscopes. Sasa ukisubiri kuona lazima ukae siku moja nyingine yani nashangaa sana kama Australia washauona na Mecca imeshauona then unasubiri nini?
 
Back
Top Bottom