beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, UDA Rapid Transit (UDART), inaujulisha umma kuwa, huduma za mabasi hayo kwa baadhi ya njia zimesitishwa kuanzia saa 11:00 alfajiri tarehe 15/04/2018 kutokana kufungwa kwa Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kwa sababu ya mafuriko yaliyosababisha maji kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi.
Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza. Deus Bugaywa, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART.
UPDATES:
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Lazaro Mambosasa amesema, watu watatu wamefariki dunia ambapo miili yao imeokotwa eneo la Tabata Kisiwani, Dar es Salaam.
Watu wawili kati ya hao (mama na mtoto) wameangukiwa na ukuta wa nyumba, na mwingine mwili wake umeokotwa mtoni.
=====
Mvua inayoendelea kunyesha kwa siku ya tatu leo Jumatatu Aprili 16, 2018 imesababisha barabara kutopitika, huku baadhi ya wanafunzi wakirejeshwa nyumbani.
Wanafunzi wa shule ya St. Florence Academy iliyopo Mikocheni wamerudishwa nyumbani kutokana na maji kujaa shuleni.
Kutokana na hofu ya madhara ya mvua, baadhi ya wazazi wamewazuia watoto wao kwenda shuleni.
Baadhi ya barabara ikiwamo inayopita eneo la Shoppers Plaza Mikocheni haipitiki kutokana na kujaa maji.
Msongamano wa magari ni mkubwa barabara za Mandela na Nyerere ambako licha ya mvua baadhi ya watu wameamua kutembea kwa miguu.
======
Watu saba wamefariki dunia kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es salaam.
Kamanda wa polisi kanda maalum jiini Dar es salaam Lazaro Mambosasa amethibitisha vifo hivyo, na kueleza kwamba mwili mmoja umekutwa ukielea kuelekea maeneo ya Jangwani jijini Dar es salaam.
Sambamba na hilo Kamanda Mambosasa amesema maeneo mengi jijini Dar es salaam yamejaa maji, na kuwataka watu kuwa makini wanapotumia barabara hasa sehemu zenye makorongo, na kuwaangalia zaidi watoto ambao wanapita mara kwa mara wakienda shule au wakiwa wanarudi kutoka shule.
“Watu wasijaribu maji, ukijaribu maji ujue utaondoka nayo, kwa hiyo watoto wetu wanapokwenda shuleni tuwasindikize, sehemu nyingi zenye makorongo kwa mfano kule Kinyerezi, kule Goba kule Makongo, zile shortcut zote maji yamejaa, watu wajiepushe kutumia njia hizo, watapoteza watoto wakiwa wanaenda au kutoka shule”, amesema Kamanda Mambosasa.
Jeshi la Polisi limesema litaendelea kutoa taarifa za sehemu mbali mbali kuhusu hali ya mvua, ambayo inaendelea kuathiri sehemu kubwa ya nchi.
MWENDELEZO: Idadi ya watu waliofariki kutokana na Mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar imefikia 9 huku wengine 6 wakijeruhiwa
> Kamanda Mambosasa amedai jiji linapokea maji mengi kutoka maeneo ya Kisarawe ambayo ndio yanaleta madhara makubwa
Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza. Deus Bugaywa, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART.
UPDATES:
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Lazaro Mambosasa amesema, watu watatu wamefariki dunia ambapo miili yao imeokotwa eneo la Tabata Kisiwani, Dar es Salaam.
Watu wawili kati ya hao (mama na mtoto) wameangukiwa na ukuta wa nyumba, na mwingine mwili wake umeokotwa mtoni.
=====
Mvua inayoendelea kunyesha kwa siku ya tatu leo Jumatatu Aprili 16, 2018 imesababisha barabara kutopitika, huku baadhi ya wanafunzi wakirejeshwa nyumbani.
Wanafunzi wa shule ya St. Florence Academy iliyopo Mikocheni wamerudishwa nyumbani kutokana na maji kujaa shuleni.
Kutokana na hofu ya madhara ya mvua, baadhi ya wazazi wamewazuia watoto wao kwenda shuleni.
Baadhi ya barabara ikiwamo inayopita eneo la Shoppers Plaza Mikocheni haipitiki kutokana na kujaa maji.
Msongamano wa magari ni mkubwa barabara za Mandela na Nyerere ambako licha ya mvua baadhi ya watu wameamua kutembea kwa miguu.
======
Watu saba wamefariki dunia kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es salaam.
Kamanda wa polisi kanda maalum jiini Dar es salaam Lazaro Mambosasa amethibitisha vifo hivyo, na kueleza kwamba mwili mmoja umekutwa ukielea kuelekea maeneo ya Jangwani jijini Dar es salaam.
Sambamba na hilo Kamanda Mambosasa amesema maeneo mengi jijini Dar es salaam yamejaa maji, na kuwataka watu kuwa makini wanapotumia barabara hasa sehemu zenye makorongo, na kuwaangalia zaidi watoto ambao wanapita mara kwa mara wakienda shule au wakiwa wanarudi kutoka shule.
“Watu wasijaribu maji, ukijaribu maji ujue utaondoka nayo, kwa hiyo watoto wetu wanapokwenda shuleni tuwasindikize, sehemu nyingi zenye makorongo kwa mfano kule Kinyerezi, kule Goba kule Makongo, zile shortcut zote maji yamejaa, watu wajiepushe kutumia njia hizo, watapoteza watoto wakiwa wanaenda au kutoka shule”, amesema Kamanda Mambosasa.
Jeshi la Polisi limesema litaendelea kutoa taarifa za sehemu mbali mbali kuhusu hali ya mvua, ambayo inaendelea kuathiri sehemu kubwa ya nchi.
MWENDELEZO: Idadi ya watu waliofariki kutokana na Mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar imefikia 9 huku wengine 6 wakijeruhiwa
> Kamanda Mambosasa amedai jiji linapokea maji mengi kutoka maeneo ya Kisarawe ambayo ndio yanaleta madhara makubwa