FDR.Jr
JF-Expert Member
- Jun 17, 2008
- 1,359
- 353
JK ,umri usiwe kigezo tafuta wachapakazi
WAKATI tuhuma za utendaji mbovu wa mawaziri ambao unadaiwa kuwa chanzo cha kukwamisha mkakati wa kasi mpya zikipamba moto, Rais Jakaya Kikwete amewapa matumini vijana kuwa akichaguliwa tena mwaka 2010, wazee hawatakuwa na nafasi katika serikali yake.
Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye mkutano wa vijana kutoka sehemu mbalimbali barani Afrika jijini Dar es Salaam, uliohusu mpango wa uongozi wa Afrika (Africa Initiative), Rais Kikwete alisema: Kama nitajaliwa kuchaguliwa tena (2010), nitahakikisha naubadilisha uongozi wa Tanzania kwa kuufanya kuwa wa vijana.
Hii inamaanisha kwamba, akifanikiwa kuchaguliwa tena kipindi kijacho atatoa nafasi kubwa kwa vijana na kuifanya serikali yake kuwa ya vijana tofauti na sasa ambapo asilimia kubwa ya mawaziri na maafisa wa ngazi mbalimbali ni wazee.
Kauli ya JK ni changamoto muhimu kwa maendeleo ya taifa na hasa katika masuala ya ajira nchini, ingawa hatuna uhakika kama kweli vijana wataweza kufanikisha utendaji kwa kiwango kinachotakiwa na kwa mazingira salama kutokana na hulka ya vijana katika kushughulikia mambo.
Ni dhahiri kwamba, hata kama ataweka vijana kwa vyovyote vile kutakuwa na wazee wa kupooza mambo kama alivyosema wakati anaingia madarakani akikumbuka maneno ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kuwa, ukiwaachia vijana nchi itawaka moto.
Kama kweli rais anajiandaa kuondoa wazee kwa sababu anataka vijana, awe makini kwani kuna wazee wenye uwezo wa kiutendaji na wapo vijana wasioweza kitu.
Kuna ushahidi wa kutosha kwamba, hata walioko katika baraza lake la mawaziri safari hii kutokana na kazi walizopewa kuna ufa mkubwa kuliko hata za baadhi ya wazee wanaotumia uwezo na elimu yao vizuri kulisaidia taifa.
Maana yake ni kwamba, suala si bora vijana ili kupata watu wenye elimu nzuri, uwezo kwa kutumia ujuzi wao na si bora vyeti, wenye uchungu na nchi yao na waliotayari kulitumikia taifa kwa moyo wote na kulinda rasilimali za umma.
Pia kama kweli anataka vijana, asiangalie urafiki kupitia mtandao wa ushindi na mchakato huo uanzie kwenye uchaguzi wa wabunge kwa kuweka taratibu zinazowaondoa wazee waliokalia viti vya ubunge kwa muda mrefu na hawana mpango wa kuondoka kwa kisingizio cha kuwa wanapendwa na wananchi hata kama hawana mchango wowote na wengi wanagombea kwa ajili ya ndoto ya kupata uwaziri au unaibu waziri.
Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye mkutano wa vijana kutoka sehemu mbalimbali barani Afrika jijini Dar es Salaam, uliohusu mpango wa uongozi wa Afrika (Africa Initiative), Rais Kikwete alisema: Kama nitajaliwa kuchaguliwa tena (2010), nitahakikisha naubadilisha uongozi wa Tanzania kwa kuufanya kuwa wa vijana.
Hii inamaanisha kwamba, akifanikiwa kuchaguliwa tena kipindi kijacho atatoa nafasi kubwa kwa vijana na kuifanya serikali yake kuwa ya vijana tofauti na sasa ambapo asilimia kubwa ya mawaziri na maafisa wa ngazi mbalimbali ni wazee.
Kauli ya JK ni changamoto muhimu kwa maendeleo ya taifa na hasa katika masuala ya ajira nchini, ingawa hatuna uhakika kama kweli vijana wataweza kufanikisha utendaji kwa kiwango kinachotakiwa na kwa mazingira salama kutokana na hulka ya vijana katika kushughulikia mambo.
Ni dhahiri kwamba, hata kama ataweka vijana kwa vyovyote vile kutakuwa na wazee wa kupooza mambo kama alivyosema wakati anaingia madarakani akikumbuka maneno ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kuwa, ukiwaachia vijana nchi itawaka moto.
Kama kweli rais anajiandaa kuondoa wazee kwa sababu anataka vijana, awe makini kwani kuna wazee wenye uwezo wa kiutendaji na wapo vijana wasioweza kitu.
Kuna ushahidi wa kutosha kwamba, hata walioko katika baraza lake la mawaziri safari hii kutokana na kazi walizopewa kuna ufa mkubwa kuliko hata za baadhi ya wazee wanaotumia uwezo na elimu yao vizuri kulisaidia taifa.
Maana yake ni kwamba, suala si bora vijana ili kupata watu wenye elimu nzuri, uwezo kwa kutumia ujuzi wao na si bora vyeti, wenye uchungu na nchi yao na waliotayari kulitumikia taifa kwa moyo wote na kulinda rasilimali za umma.
Pia kama kweli anataka vijana, asiangalie urafiki kupitia mtandao wa ushindi na mchakato huo uanzie kwenye uchaguzi wa wabunge kwa kuweka taratibu zinazowaondoa wazee waliokalia viti vya ubunge kwa muda mrefu na hawana mpango wa kuondoka kwa kisingizio cha kuwa wanapendwa na wananchi hata kama hawana mchango wowote na wengi wanagombea kwa ajili ya ndoto ya kupata uwaziri au unaibu waziri.