Kama kuvunja muungano kutatatua matatizo kama rushwa, kupanda hovyo kwa bei za bidhaa(leo nimenunua mafuta ya taa kwa tshs 5000 kwa lita!), uongozi mbovu, upatikanaji wa nishati,udhaifu wa miundombinu n.k. nitakua tayari kuunga mkono jitihada hizo, tofauti na hapo itabidi nijifikirie kwanza. Hoja yangu ni kwamba Watanzania wenzangu tujifunze kuyaangalia matatizo tuliyonayo na namna ya kuyatatua badala ya kutafuta mengine ambayo ndio kwanza yanaonesha dalili zote za kutuongezea matatizo mengine.