japanese
Member
- Jul 28, 2015
- 13
- 16
Hakika ukawa ni mpango wa mungu kwa watanzania na siku si chache mpango huu unakwenda kutimia.
Tokea vuguvugu la ukawa lianze kuna mengi yametokea lakini kadri siku zinavyoenda ndio umoja huu unazidi kuimarika CCM na mawakala wake kwa nyakati mbalimbali wamejitahidi sana kuhujumu umoja huu lakini wamegonga mwamba,wametumia fedha nyingi kununua wanaukawa lakini wameshindwa.
CCM kuna siri kubwa inawatia hofu juu ya UKAWA ,moja ni kwamba katika chaguzi nyingi walifanikiwa kushinda kirahisi vyama vya upinzani kwa kuwa havikuwa na umoja,pili umma ulishindwa kujenga imani kwa vyama vya upinzani ukiamini kwamba upinzani hakuna watu makini wanaoweza kusukuma mbele matarajio yao,na fikra hizi potofu zilijengwa na ccm kwa miaka mingi.
Mwaka huu propaganda za CCM zimegonga mwamba kwani kwa Mara ya kwanza katika siasa za Tanzania bara watu wakubwa ndani ya CCM na serikali wameasi siasa za ccm na kujiunga na siasa za upinzani tena wakigombea nafasi nyeti ya uraisi,jambo hili limeongeza imani kubwa kwa wananchi na kufuta mawazo ya kuwa upinzani hawana uwezo wa kuongoza nchi,hivi sasa ni nadra sana kimsikia kiongozi tokea ccm akitamka kwa kujiamini kuwa upinzani hauwezi kuongoza nchi.
Na badala yake wanaccm na mgombea wao wa uraisi wanatumia muda mwingi kumnanga mgombea wa ukawa kuliko kuelezea Sera zao na mambo mengine ambayo mgombea wao anayemaliza muda wake aliwahidi wananchi kama vile maisha bora kwa kila mtanzania,katiba mpya, ujenzi wa reli ya kati ,meli mpya kanda ya ziwa,mahakama ya kaghi nk.
Tokea vuguvugu la ukawa lianze kuna mengi yametokea lakini kadri siku zinavyoenda ndio umoja huu unazidi kuimarika CCM na mawakala wake kwa nyakati mbalimbali wamejitahidi sana kuhujumu umoja huu lakini wamegonga mwamba,wametumia fedha nyingi kununua wanaukawa lakini wameshindwa.
CCM kuna siri kubwa inawatia hofu juu ya UKAWA ,moja ni kwamba katika chaguzi nyingi walifanikiwa kushinda kirahisi vyama vya upinzani kwa kuwa havikuwa na umoja,pili umma ulishindwa kujenga imani kwa vyama vya upinzani ukiamini kwamba upinzani hakuna watu makini wanaoweza kusukuma mbele matarajio yao,na fikra hizi potofu zilijengwa na ccm kwa miaka mingi.
Mwaka huu propaganda za CCM zimegonga mwamba kwani kwa Mara ya kwanza katika siasa za Tanzania bara watu wakubwa ndani ya CCM na serikali wameasi siasa za ccm na kujiunga na siasa za upinzani tena wakigombea nafasi nyeti ya uraisi,jambo hili limeongeza imani kubwa kwa wananchi na kufuta mawazo ya kuwa upinzani hawana uwezo wa kuongoza nchi,hivi sasa ni nadra sana kimsikia kiongozi tokea ccm akitamka kwa kujiamini kuwa upinzani hauwezi kuongoza nchi.
Na badala yake wanaccm na mgombea wao wa uraisi wanatumia muda mwingi kumnanga mgombea wa ukawa kuliko kuelezea Sera zao na mambo mengine ambayo mgombea wao anayemaliza muda wake aliwahidi wananchi kama vile maisha bora kwa kila mtanzania,katiba mpya, ujenzi wa reli ya kati ,meli mpya kanda ya ziwa,mahakama ya kaghi nk.