Mungu akubariki kwa uamuzi huo. Ila kwenye safari yako ya marejeo, ukitaka umwone Mungu, wala usilenge kwamba umrudie ili mambo yako yawe bora, material things kwa Mungu wetu ni sawa na kachumbari au pilipili ya kuweka kwenye chakula tu, yaani ni kitu cha ziada ila chakula halisi kipo. Bali utafuteni kwanza Ufalme wake na haki yake na mengine yote mtazidishiwa.
nakuomba, lenga kutakaswa roho yako na kukaa katika uwepo wa Mungu moyoni mwako, yaani Mungu akae ndani yako, akishafika tu, hayo mengine ni marupurupu tu atakupa hata yale usiyoyaomba kwasababu anajua tunayohitaji. sawa na mtoto anaomba umpe pipi kumbe wewe ulipanga umnunulie baiskeli, mtoto wako yupo shule anaomba umpe elfu kumbi wakati wewe unaona uhitaji wakeni zaidi na ulipanga umpe laki moja. Mungu akiwa ndani yako hayo mengine ni ziada tu na tutapata na kusaza.
uwepo wa Mungu utakujaje kwako? ni kwa kusoma sana Neno la Mungu, tenga muda wa kusoma sana, pili, kwa kufanya maombi na kama umebahatika kujazwa Roho Mtakatifu, maombi ya Roho na kushiriki ibada.