Mungu husema na Watu

Kwahiyo mleta mada yeye aliongea waziwazi na Mungu yupi kati ya hao Miungu unaosema wapo wengi?

Au wewe ndio mleta mada umeamua kuja kivungine?
Mungu wake kupitia Roho mtakatifu aliyemsema

Kila mtu anaishi anavyoona sawa kama kitu kwako hukiamin kwa wenzako wanaamini haina haja wewe kukibeza

Katiba ya Tanzania inatoa uhuru wa kuabudu hata angesema anaongea na mawe nisingembishia ndo njia na maisha aliyochagua
 
Jibu swali,Mungu yupi? si umesema wapo miungu wengi?
 
Jibu swali,Mungu yupi? si umesema wapo miungu wengi?
Kama ni mkristo Mungu wake ni Yahweh ambaye anatumia Roho mtakatifu
Mbona imekua ni ugomvi tena

Kwa wakristo ni kawaida Mungu kuongea na watu wake direct hata mimi Mungu anaongeaga na mimi direct
 
Mbali na kusikia kupitia sauti ya Mungu kupitia sauti,

Mara nyingi nikifunua BIBLIA na kusoma, Huwa naisikia sauti yake direct kupitia NENO.

Amen
 
Kuna vitu ukivijua Maisha yako yanakua yanaandamwa na furaha sana, about 25 years back nilikua mtu mmoja mwenye furaha ya kutisha na kutosha zingatia neno 'kutosha', nahisi Ile furaha ya miaka Ile inaanza kuja na kurejea tena baada ya miaka zaidi ya 25 kupita sababu nimetambua kitu kilichopo ndani yangu kinasema na kuongea na Mimi kila wakati, huyo natambua ni Mimi halisi ni Mimi mwenyewe ni Mimi haswa ni Mimi yuleyule re-"member"-ing the inner true me from way back,
 
Mbali na kusikia kupitia sauti ya Mungu kupitia sauti,

Mara nyingi nikifunua BIBLIA na kusoma, Huwa naisikia sauti yake direct kupitia NENO.

Amen
Unajisikia au unaisikia?

Hivi ushawahi fumba macho ukaanza kufanya body scan kwenye hali ya utulivu? Ushawahi fanya hivyo? Ulihisi nini na uliona nini?
 
Mungu akubariki sana kwa ushuhuda mzuri. Binafsi pia Mungu ameongea nami kwa namna mbalimbali nyingi mno, kuna siku nitafundisha hapa kwa ushuhuda wa maisha yangu kuhusu kusikia sauti ya Muntu, sauti ya ndani rohoni mara nyingi mno, kwenye ndoto kila kitu kibaya kinachokuja mbele yangu huwa naonyeshwa kabla na najiandaa nikipuuzia huwa nakutana nacho na napata shida kwelikweli, kuna namna nyingi nitakuja kueleza namna Mungu alivyoongea nami. Ukiona umebarikiwa kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu hadi anaongea na wewe kwa namna mbalimbali, shikilia hapohapo.
 
hiyo furaha ya binafsi yako hiyo kuna siku utakuja kuiona ni takataka kabisa ukijazwa Roho Mtakatifu, hakika utajisikia raha ya ajabu, moyo wenye furaha, imani kuu, Nguvu za Mungu, uhakika wa maisha, uhakika wa uzima haielezeki, its beyond description.
 
Ndugu yangu, tunaongea na Mungu hivi hivi tukiwa hai, kabisa kabisa. Mungu huwa anaongea na watu, anaamua tu aina ya communication ipi atumie, wengine wanasikia sauti kabisa kama mimi na wewe tunapoongea na kujibizana kabisa, Mungu ni halisi, sio story. wengine Mungu anaongea nao kwa ndoto, wengine kwa sauti ya ndani, wengine kwa Neno la Mungu unasoma Biblia halafu mistari yote unaona ya kawaida ila upo mmoja tu ambao unachoma na kuongea na wewe na unajua kwamba ni Mungu anaongea, wengine Mungu anaongea nao kwa maono ya waziwazi au ya usingizini n.k,

wengine Mungu anawatumia malaika waje kukuambia wakiwa wamevaa aidha mwili wa mwanadamu au wakiwa vilevile kama malaika walivyo. Samweli alisikia sauti ya Mungu kabisa ikimuita, Yesu aliposhuka kubatizwa sauti ilitoka mbinguni ikisema Huyo ndiye mwanangu mpendwa msikieni yeye na wote waliokuwepo walisikia ile sauti, Yesu alipopanda mlimani na Petro yohana na yakobo kuomba akabadilika sura ikawa inamng'aa Musa na Eliya wakashuka kumhudumia sauti ilitoka na wanafunzi hao walisikia kabisa,

Petro alipokuwa gerezani malaika alienda kumtoa gerezani akamwambia aelekee wapi hadi nje, mambo mengi mengi. mimi binafsi Mungu ameongea na mimi mara nyingi sana hadi huwa naogopa.

Juzi wakati natype hapahapa JF Mungu aliongea nami kwa sauti ya ndani kwamba "MUNGU ANAPENDA SANA KUWA NA UHUSIANO WA KARIBU NA WANADAMU", yaani kama uhusiano wa baba na mtoto, umwabudu, umsifu, umheshimu, umsikilize, umuombe mahitaji mbalimbali n.k, Mungu anapenda hivyo, ameongea na mimi. sijui nikuelezeje?
 
Shetani oyeeeee
 
anaamua tu aina ya communication ipi atumie,
That's the communication between mind (brain) and heart (soul), hayo ni mawasiliano baina ya Nafsi na Roho, like what do you feel? What do you experience? The eyes, after all, are the mirrors of the soul,
 
Huu mwaka nmechelewa sanaa....ila kuanzia mwez huu nimeamua kufanya Toba na kumrudia Mungu kwani nmejiona kama nmejiweka mbali nae...Kuna mambo yangu naona kabisa hayaendi kwa sababu ya kutokumshirikisha Mungu....hakika naona atanionekania na kunifanya kuwa mpya
 
Umefunga na kusaidia wenye uhitaji?
 
Mmmhhh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…