tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema linaendelea kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi katika kuimarisha ulinzi kwenye maeneo mbalimbali ya jiji.
Kwa mujibu wa taarifa ya siku ya Jumamosi ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, SACP Jumanne Muliro hali ya usalama inaendelea kuwa ya kuridhisha, huku taarifa za raia zikisaidia kwa kiasi kikubwa kugundua na kuzuia mipango ya vitendo vya kihalifu.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa maandalizi ya kiusalama yameongezwa kuelekea mchezo wa kimataifa wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, utakaofanyika Jumapili, Novemba 23, 2025, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kati ya Simba SC ya Dar es Salaam na Petro Atletico ya Angola.
Jeshi la Polisi limewakumbusha mashabiki na wapenzi wa mchezo huo kufuata taratibu, kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani, na kuhakikisha mchezo unafanyika katika mazingira salama na yenye nidhamu.
Kwa mujibu wa taarifa ya siku ya Jumamosi ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, SACP Jumanne Muliro hali ya usalama inaendelea kuwa ya kuridhisha, huku taarifa za raia zikisaidia kwa kiasi kikubwa kugundua na kuzuia mipango ya vitendo vya kihalifu.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa maandalizi ya kiusalama yameongezwa kuelekea mchezo wa kimataifa wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, utakaofanyika Jumapili, Novemba 23, 2025, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kati ya Simba SC ya Dar es Salaam na Petro Atletico ya Angola.
Jeshi la Polisi limewakumbusha mashabiki na wapenzi wa mchezo huo kufuata taratibu, kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani, na kuhakikisha mchezo unafanyika katika mazingira salama na yenye nidhamu.