Muhimu kwako mpiga kura mwenzangu

Muhimu kwako mpiga kura mwenzangu

Mu-sir

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2010
Posts
3,621
Reaction score
1,640
Wakati huu ni wa kuhakiki taarifa zako kwenye Daftari la kudumu la kupiga kura. Ni muhimu kuhakiki ili tusipoteze Fursa ya kupiga kura pale ambapo ukienda kupiga kura unakuta taarifa siyo sahihi kwani hutoruhusiwa kupiga kura.

kuna tetesi za chama tawala kutumia fursa hii kufanya utafiti wa ni kundi gani katika jamii linalojitokeza kwa wingi kuhakiki taarifa zao ili liwe kundi mahususi kulilenga wakati wa kampeni kwani ndilo litapiga kura. Wenye kusikia wasikie.

kwa taarifa nilizozipata usipohakiki ni vigumu kuruhusiwa kupiga kura. Mikoa iliyotangazwa na tume kuhakiki taarifa zao kuanzi tarehe 1 agosti ni:
NJOMBE, IRINGA, MTWARA, LINDI, RUVUMA, KATAVI, RUKWA, MBEYA, DODMA, SINGIDA, TABORA, KIGOMA NA KAGERA.

NB:

Usipuuzie taarifa hii kama uko katika hiyo mikoa kuhakiki ni mojawapo ya kigezo muhimu.
 
Hawa jamaa wanatuona sisi mabwege eti.
Mbona mi nipo Mbeya sijasikia?
Mtoa mada una uhakika unachoongea?
 
Nilisikia kuwa wana mpango wa kuhakiki sijasikia kama wametangaza
 
Bwana BRO SANTANA Tangzao la tume hilo hapo kama linavyoonekana. Nililiona humu humu JF
 

Attachments

  • 1439312716444.jpg
    1439312716444.jpg
    48 KB · Views: 211
Last edited by a moderator:
Nilisikia kuwa wana mpango wa kuhakiki sijasikia kama wametangaza

Hilo ni kweli ndio maana matangazo kama haya hayapewi uzito hata na wanahabari. Wengi wata relax siku ya kura inakuwa tofauti na matarajio yao
 
Hizi taarifa ni za kweli ila ni tecnic ya kupunguza wapiga kura watu wengi tumebweteka kwa kupata kadi lakini huenda wengi tusipige kura
 
Hizi taarifa ni za kweli ila ni tecnic ya kupunguza wapiga kura watu wengi tumebweteka kwa kupata kadi lakini huenda wengi tusipige kura

Haswaa kuhakiki ndio kitu cha muhimu wandugu
 
Kama kuna aliyefanikiwa kuhakiki pia kupitia *152*00# atujulishe kwangu inasumbua. Hii namba nimetoa kwenye thread moja humu humu
 
Kama kuna aliyefanikiwa kuhakiki pia kupitia *152*00# atujulishe kwangu inasumbua. Hii namba nimetoa kwenye thread moja humu humu

Hiyo njia siiamin sana kwani Tume ya uchaguzi haijaitangaza kama mojawapo ya njia ya uhakiki. Wajuzi watuambie
 
Kama kuna aliyefanikiwa kuhakiki pia kupitia *152*00# atujulishe kwangu inasumbua. Hii namba nimetoa kwenye thread moja humu humu

Me nmejaribu kichinjio changu kipo sawa kabisaaa. Sema halipewi uzito sana ilo jambo Cjui kwann hawatangaz
 
Hiyo njia siiamin sana kwani Tume ya uchaguzi haijaitangaza kama mojawapo ya njia ya uhakiki. Wajuzi watuambie
Nilimwona wa tume alitaja hyo number kuhakiki nimejaribu hyo inazingua ila kwa tigo inakubali.
 
Back
Top Bottom