KUNA MAKALA MOJA NILISOMA JUU YA KESI ZA EPA na uendeshaji pale kisutu. kwa bahati nzuri, mimi kama mwanasheria wa kujitegemea kwa muda mrefu, kuna jambo limekuwa likiniuma sana, na ni muhimu watu wajue.
wakati KANUMBA alipokufa, viongozi hata wa serikali wengi walihudhuria, wabunge walihudhuria, na watu wa vyama mbalimbali. WAKATI SHAROBARO alipokufa, NAPE alienda kule na wengine wakuu wa wilaya sijui. kanumba na sharo walikuwa watz waliotoa mchango mkubwa kwa taifa kupitia sanaa zao, hilo halipingiki na walistahili misiba yao kufanyiwa vile ilivyofanyiwa. ajabu yake, kuna mtu mmoja alikufa pale kwa DPP, ni kijana ambaye nimefanya naye kwazi kwa muda mrefu yeye kama wakili wa serikali, anaitwa marehemu BONIFAS. huyu ni mashine ambayo imekuwa ikiendesha kesi nyingi sana na tegemeo kubwa kwa kesi za epa, na zile kuukuu, conviction nyingi zinatokea pale kisutu , appeal zote, kesi ya MURO ambayo rushwa ilitembezwa sana ushaidi upo wazi lakini hakimu akaamua atakavyo pamoja na rushwa za mahakimu, yeye ndiye amekuwa kiongozi. ni mara nyingi ametishiwa hadi maisha kwasababu ya kesi za epa. lakini alipokufa, hakuna kiongozi hata mmoja alienda kumzika. hakuna wa chadema, wa ccm, mbunge, waziri, mkuu wa wilaya wala mkoa wala nani. pamoja na kwamba kazi aliyokuwa anafanya ni moja ya kazi hatari mno, ni kazi iliyofunga watu na kurudisha hela zilizoibiwa nyingi. IKUMBUKWE KUWA, PAMOJA NA KWAMBA WATU WENGI WANAFIKIRI WALE WEZI WA EPA HAWAFUNGWI, WENGI TU WAPO WAMEPEWA CONVICTION.
JAMBO KUU ninalopenda kuliongea hapa ni seriousness ya serikali yetu katika kuchangua maeneo ya vipaumbele. kwa bahati, kabla sijaenda private, nilishafanya kazi kama wakili wa serikali kwa muda mrefu, na bado kwenye damu yangu kazi hiyo ipo pamoja na kwamba kwa nje simo tena, niliondoka kwasababu ya maslahi.
ukitembelea pale kisutu, au mahakama yeyote ila ya wilaya, mkazi, mahakama kuu au rufaa, utawakuta mawakili wa serikali na visuti vyao vyeusi, wanashitaki watu badala ya serikali. hawa ni watu wanaobeba maslahi ya umma sana, wanaitetea serikali na kushitaki watu badala ya serikali ili uhalifu upungue. lakini mchango huu hautambuliwi sawia na serikali kiasi kwamba ilishindwa HATA KWENDA KUMZIKA BONIFAS, ambaye kwa kifo chake ni furaha kubwa kwa akina MRAMBA na akina KATITI etc ambao kesi zao bado zinaendelea pale kisutu. hakika yake, bonifas akiwa anatoa submissions zake, hadi mahakimu wengine walikuwa wanaacha mahakama zao wanaenda kumsikiliza ili wajifunze, kwasababu alikuwa na uzoefu wa muda mrefu mno na mahakimu wa kisutu wenyewe walikuwa wanajifunza toka kwake. wakili gani wa kujitegemea alikuwa na ujasiri wa kutosha mbele yake? amehatarisha maisha yake kwa kitambo kwa kazi hizi za kujitoa mhanga, lakini HATA SERIKALI NGAZI ZA JUU WALE WALIOENDA KUMZIKA KANUMBA HAWAKUJA KWAKE. sijui niseme ni aibu kwa serikali au ni nini, au tuseme hujali ili waonwe tu ila haitoki moyoni.
pamoja na polisi kujitahidi kuharibu ushahidi wa kesi mara nyingi (wao ndio wapelelezi, prosecutors wanaletewa tu vitu ili wa present mahakamani kisheria), mawakili wa serikali bado wameendelea kufanya kazi katika mazingira magumu, fungu na hawatambuliwi sana. hivi wakila rushwa tutawalaumu? wakiharibu kesi tutawalaumu? ulinzi wao uko wapi? mbona ulinzi wao tofauti na ule tunaouona pccb? unajua ni wangapi wanaikimbia hiyo ofisi karibia kila mwezi? watu wanaajiriwa wanaona uzushi wanaacha wanakuja kwenye private, kwasababu ya mambo kama haya. unaitumikia serikali kwa kujitoa mhanga kwenye mazingira magumu ya kutishiwa na washitakiwa ambao haujui watakuvamia saa ngapi, halafu mtu kama bonifas akifa mawaziri hata rais hawaji; kama kazi ya yule jamaa ingekuwa imeandikwa kwenye magazeti na kesi zake zote zile, hakika rais angekuja kwasababu ule mchakato wa mafisadi wa epa na wengine bonifas ndiye aliyekuwa mashine pale kisutu na mahakama kuu etc kuhakikisha kesi zinaenda vizuri. NI JAMBO AMBALO LIMEKUWA LIKINIUMA KWA MUDA MREFU, NASHUKURU NIMELITUA KWA JAMII ILI MZIGO MOYONI MWANGU UTULIWE. kama tunataka wahalifu, mafisadi etc wafungwe na kurudisha mali zetu, ni lazima wale wanawashugulikia tuwapromote na kuonyesha tunawajali. mishahara yao midogo, hata kwenda kuwazika jamani mmeshindwa? kama kuna mtu alihudhuria ule msima atajua ninachoongea hapa.....yule jamaa likuwa na hadhi ya jaji, hata majaji wenyewe akiwa high court akiongea walikuwa wanamsikiliza kwa makini ili wapate vitu toka kwake, ilikuwa mashine kubwa sana, na taifa hili limepoteza mtu muhimu sana ambaye mchango wake kwa jamii haujatambulika hadi sasa. MUNGU IBARIKI TANZANIA.