Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,662
Yaani sijui nianze kwa kujieleza kiasi gani maana sijui kama nitaeleweka ama nitawafurahisha watu..........Ukweli nashindwa kujua iwapo Watanzania sasa hivi wamejiajiri ama wameajiriwa maana kwa jinsi wanavyotumia muda mwingi katika mtandao (including simu, kuchati na kuswap) kama wameajiriwa sijui wanautumiaje muda wa mwajiri ama kazi zao maana kujigawa inakuwa ni ngumu! Ingawa kuna watu majiniaz katika kufikiri poit lakini wengi ni wale wakufikiri kwa kiwango cha kawaida ama kufanya rejea kitu kinachochukua muda mwingi.
Sasa sijui wanafanya na kufikiria about their jobs saa ngapi na wanabonyezabonyeza simu zao ama laptop zao saa ngapi!!!! Ikiwa wanatumia muda mwingi kwenye kubonyezabonyeza katika simu zao ama laptops zao (ikiwa kubonyeza huko hakuhusiani na kazi) sisi wahasibu ule muda uliopotea badala ya kufanya kazi tunaita 'iddle time....'. Sasa accounting ya iddle time kwenye management accounting tunajua....... kunafanya production capacity isiwe 100% efficient.
Kwa mtazamo huo na kwa assumptions kuwa kila mtanzania anao muda wa kupoteza katika kubonyezabonyeza simu yake ama komputa yake ina maana ya kwamba kila mahala panapohitaji watu wafanye kazi ufanisi wake uko chini ya kiwango. Which means kama kuna deadline inayohitaji kazi imalizike kwa muda fulani, basi pressure ya kazi itasababisha products kuwa sub-standard. Na madhara ya sub-standard kihasibu ni makubwa sana....Hii ina maana kuwa ama bidhaa zinazozalishwa Tanzania na Watanzania au huduma zinazotolewa na Watanzania ziko chini ya kiwango!!!! Hapa ni katika kampuni binafsi ama hata serikalini uhafifu utaendelea kukua sana!!!!
Na kwa upande wa pili yaani kule kunakotumika muda mwingi wa kuswap ama kubonyezabonyeza vifaa vya electronics tunapata mazao mawili makuu (faida ama tuziite hasara?):
Kwanza, watu wanakuwa ni wepesi wa kung'amua mambo na kuyasemea kwa haraka kabla hayajasahaulika. Upeo wa kuona mbali pia huongezeka sana pia weledi wa kucheza na maandishi unakuwa mkubwa sana maana ili mtu aweze ku-think critically ni lazima afanye rejea sahihi na kwa undani zaidi.
Pili, shughuli za viwandani na mashambani zitafifia na hatimaye kufa kabisa maana watu watakuwa wanafanya kazi kwa kusema ama kutumia vidole tu......Yaani ni kama watakuwa wanauzoefu wa kazi theoretically!!!! Na hii itasababishwa na watu kuwa na uwezo mkubwa wa kuongea kuliko kufanya kazi maana tayari damu yao iko iddle.
Nihitimishe kwa kusema kwamba baada ya miaka kadhaa ya tabia hii ya kushinda kwenye mitandao bila kitu muhimu kinachokusukuma kufanya hivyo, taifa litakuja kuwa na wataalamu wa kuongea badala ya kufanya kazi. Matokeo yake ni kuwa wananchi wa nchi zisizoendekeza sogonyola watakuja na kutwaa kazi zetu na sisi kuendelea kuwa iddle officially!!! Na kwa kuwa ni wataalamu wa kuongea tutaongea sana na kujaza ma-volume ya makaratasi ya kulalamikia ujio wa watu wengine kutwaa kazi zetu. Mwisho wa siku tutashindwa kupata hata pesa ya kulisha familia zetu....Na hatimaye tutahangaika sana katika ardhi yetu wenyewe tuliyoishindwa kuitumia.
Sasa sijui wanafanya na kufikiria about their jobs saa ngapi na wanabonyezabonyeza simu zao ama laptop zao saa ngapi!!!! Ikiwa wanatumia muda mwingi kwenye kubonyezabonyeza katika simu zao ama laptops zao (ikiwa kubonyeza huko hakuhusiani na kazi) sisi wahasibu ule muda uliopotea badala ya kufanya kazi tunaita 'iddle time....'. Sasa accounting ya iddle time kwenye management accounting tunajua....... kunafanya production capacity isiwe 100% efficient.
Kwa mtazamo huo na kwa assumptions kuwa kila mtanzania anao muda wa kupoteza katika kubonyezabonyeza simu yake ama komputa yake ina maana ya kwamba kila mahala panapohitaji watu wafanye kazi ufanisi wake uko chini ya kiwango. Which means kama kuna deadline inayohitaji kazi imalizike kwa muda fulani, basi pressure ya kazi itasababisha products kuwa sub-standard. Na madhara ya sub-standard kihasibu ni makubwa sana....Hii ina maana kuwa ama bidhaa zinazozalishwa Tanzania na Watanzania au huduma zinazotolewa na Watanzania ziko chini ya kiwango!!!! Hapa ni katika kampuni binafsi ama hata serikalini uhafifu utaendelea kukua sana!!!!
Na kwa upande wa pili yaani kule kunakotumika muda mwingi wa kuswap ama kubonyezabonyeza vifaa vya electronics tunapata mazao mawili makuu (faida ama tuziite hasara?):
Kwanza, watu wanakuwa ni wepesi wa kung'amua mambo na kuyasemea kwa haraka kabla hayajasahaulika. Upeo wa kuona mbali pia huongezeka sana pia weledi wa kucheza na maandishi unakuwa mkubwa sana maana ili mtu aweze ku-think critically ni lazima afanye rejea sahihi na kwa undani zaidi.
Pili, shughuli za viwandani na mashambani zitafifia na hatimaye kufa kabisa maana watu watakuwa wanafanya kazi kwa kusema ama kutumia vidole tu......Yaani ni kama watakuwa wanauzoefu wa kazi theoretically!!!! Na hii itasababishwa na watu kuwa na uwezo mkubwa wa kuongea kuliko kufanya kazi maana tayari damu yao iko iddle.
Nihitimishe kwa kusema kwamba baada ya miaka kadhaa ya tabia hii ya kushinda kwenye mitandao bila kitu muhimu kinachokusukuma kufanya hivyo, taifa litakuja kuwa na wataalamu wa kuongea badala ya kufanya kazi. Matokeo yake ni kuwa wananchi wa nchi zisizoendekeza sogonyola watakuja na kutwaa kazi zetu na sisi kuendelea kuwa iddle officially!!! Na kwa kuwa ni wataalamu wa kuongea tutaongea sana na kujaza ma-volume ya makaratasi ya kulalamikia ujio wa watu wengine kutwaa kazi zetu. Mwisho wa siku tutashindwa kupata hata pesa ya kulisha familia zetu....Na hatimaye tutahangaika sana katika ardhi yetu wenyewe tuliyoishindwa kuitumia.