Mtwara: D.B SHAPRIYA Vs DANGOTE...

Mtwara: D.B SHAPRIYA Vs DANGOTE...

Hivi unategemea nani ampinge Dangote?
Kama vijihela ya Rostam tu vina tikisa wakubwa wa nchi,
itakua interest ya Dangote kuwekeza Tanzania?
 
Kwa kiasi fulani inatia moyo kwamba sauti zilizopazwa na wanaMtwara zimelazimisha serikali kufanya chochote. Iwe hiyo mikampuni ina uhusiano na serikali au la, but hizo project zikimaterialize tunatarajia money flow kwenda Mtwara itaongezeka. Hizo hela zitakazo'mwagwa' Mtwara kwa kiasi kikubwa zitawanufaisha wanaMtwara. Wavuvi watapata soko kubwa zaidi la samaki wao, wakulima watapata soko kubwa zaidi la vyakula wanavyozalisha, wafanyabiashara (wadogo, wa kati na wakubwa kama wapo), watapata wanunuzi wengi zaidi wa bidhaa zao.
Lakini kikubwa zaidi tutashuhudia ongezeko la 'cultures' tofauti Mtwara. Watu wa mataifa na makabila mengine wataongezeka Mtwara na itawafungua zaidi upeo wanamtwara. Shule, huduma za afya (zahanati, hospitali na vituo vya afya), na huduma nyingine zinazotolewa na serikali itabidi ziimarishwe kukidhi ongezeko la idadi (na caliber?) ya watu, na hii apparently itaongeza kiasi cha fedha za serikali zitakazotolewa kama mishahara ya wafanyakazi wake na kugharamia huduma hizo.
WanaMtwara wanaomiliki ardhi pia watafaidika kwani thamani ya ardhi yao itaongezeka kutokana na mahitaji. 'Wageni' watakaokuja watahitaji kujenga na hapa tutarajie kuongezeka kwa kipato kwa wauzaji na wabebaji mchanga, vifusi, mawe, kokoto na kadhalika, pia mafundi wa nyumba, na naamini wafaidikaji wakubwa wa mambo haya ni wanamtwara wenyewe...

KOMAENI BANA, ISITOKE GESI HAPO, YATOKE MAZAO YA GESI...

Hopefully, vijana wakutoka Mtwara wanomiminika kuja Dar. kuzurula na mizigo mikononi mchana kutwa[ wamamchinga] watapungua kwani watapatiwa ajira huko huko kwao!!
 
Mtwara kuna mengi sana na kwa mtu ambaye ana weledi mkubwa wa Uchumi naweza kusema kuwa Katika miaka mitano ijayo kama hamtawabania Mtwara itakuwa ya pili kwa kuchangia pato la Taifa lenu nyuma ya Dar. Na katika miaka kumi ijayo itaongoza.

Wamebarikiwa sana na Mola kila kitu wanacho.

Je vipi gas itatoka?

Barubaru umenena vyema. Tatizo la viongozi wetu wanaotokea Mtwara kwa sasa ambao karibu wote ni wawakilishi wa chama cha mapinduzi(ccm) hawana mikakati ya kuweza kuwaunganisha wanainchi wao wakawa ktk mazingira ya kuja kunufaika na hii fursa muhimu ya gesi.

Wana mtwara walipobaini ulaghai wa viongozi wao ndipo walipoamua kwenda kwenye kutumia msuli kufikisha ujumbe.na kwa jinsi suala hili linavyoshughulikiwa inaonyesha ni jinsi gani walivyokuwa hawajajiandaa.

Hadi leo hii hakuna jibu la moja kwa moja juu ya mustakhabali wa suala la gesi zaidi ya watawala kuzuia mikutano ya kisiasa na kujadili suala la gesi. watawala wajue kuwa kama suala hili wanataka liwe endelevu ni lazima ushirikishwaji wa wanamtwara uwepo na uwe wazi kuliko wanavyolichukulia sasa hivi.

Ujio wa Dangote na wengineo hautakuwa na tija kwa wanamtwara kama ushiriki wa wanainchi wa Mtwara kwenye fursa hii nyeti na adimu haufahamiki.
 
Caspian na Shapriya ni tofauti,Shapriya wana ka-some history kidogo ka mbali kuliko Caspian as you know.
Shapriya,hii,kama,sikosei,ina,uhusiano,na,kampuni,ya,ujenzi,ya,ROSTAM,AZIZ,iliyopata,tenda,yakusomba,vifusi,katika,mgodi,wa,mwadui.
Hapo,siasa,itakuwa,ina,nafasi,kubwa.
 
Hizi kampuni ndiyo zinavyoingia kwanza zinapewa masharti kibao lakini baada ya miezi 6, hayo masharti yote hayafuatwi tena, utaona maafisa na wafanyakazi wote wageni na vibali vinatoka serikalini.
 
Mkuu chezea D.B Shapriya! Hii kampuni nayo wala haina uzalendo ni kampuni ya vyesi tu


Mtoa mada anafananisha Mjusi na Mamba kwa sababu wote wana miguu minne, lakini ukweli ni kwamba D.B Shapriya ni kajikapuni ka ujanja ujanja tu ka ujenzi,
Tena ni local Company ya hapa hapa Tanzania, kuna uwezekana aliyesema ni ya bwana Azizi akawa sahihi ,,, Welcome to db Shapirya co ltd :: .....................
 
Mtwara kuna mengi sana na kwa mtu ambaye ana weledi mkubwa wa Uchumi naweza kusema kuwa Katika miaka mitano ijayo kama hamtawabania Mtwara itakuwa ya pili kwa kuchangia pato la Taifa lenu nyuma ya Dar. Na katika miaka kumi ijayo itaongoza.

Wamebarikiwa sana na Mola kila kitu wanacho.

Je vipi gas itatoka?

a false dawn
 
Mtoa mada anafananisha Mjusi na Mamba kwa sababu wote wana miguu minne, lakini ukweli ni kwamba D.B Shapriya ni kajikapuni ka ujanja ujanja tu ka ujenzi,
Tena ni local Company ya hapa hapa Tanzania, kuna uwezekana aliyesema ni ya bwana Azizi akawa sahihi ,,, Welcome to db Shapirya co ltd :: .....................

Ni kweli its local company lakini huijui shapriya wewe!!! Na si kijikampuni kama unavyotaka watu waaamini!!
 
Ni kweli its local company lakini huijui shapriya wewe!!! Na si kijikampuni kama unavyotaka watu waaamini!!
sasa wewe unataka kulinganisha kiji LOCAL companya na lijikampuny la kimataifa? hiyo kampuni ina hela karibi sawa na GDP ya Tanzania kwa mwaka mzima.
hicho kikampuni cha ujenzi kinawezaje lingana na kampuni kubwa kama hiyo?
Point uliyosahau ni kwamba DANGOTE wanatoa pesa ya miradi yao na wanaimiliki, hao SHAPRIYA wanapiga day walk [ mpaka washinde tenda wapate mradi in other word ni kampuni mbili tofauti]
 
sidhani haya matumaini mnayatoa sayari gani lakini kama ni dunia hii the theory will not work. what i think ni kuwa tunawakaribisha makupe wengine pande hizi za kusini mwa tanganyike where natural resources are greatly un-exploited. poleni sana wabonge mtaambulia jasho tu mnofu mmh????
 
sijui haya matumaini mnayatoa sayari gani lakini kama ni dunia hii the theory will not work. what i think ni kuwa tunawakaribisha makupe wengine pande hizi za kusini mwa tanganyike where natural resources are greatly un-exploited. poleni sana wabonge mtaambulia jasho tu mnofu mmh????
 
Back
Top Bottom