Mtu mwenye pesa anatakiwa aweje?

Mtu mwenye pesa anatakiwa aweje?

kevin strootman

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2017
Posts
1,114
Reaction score
1,879
Jana nimepitia Uzi mmoja unaojadili Nyumba mpya ya mwijaku, wengine wanamsifia Kwa kupambana na kufikia uwezo wa kujenga Nyumba nzuri ya gorofa, wengine wanamtukana Kua hela amepata kwakua anakatwa marinda pia anasafirisha madawa ya vigogo (hawana ushahidi), pia wapo wanaosema kua nyumba sio ya kwake.

Mimi nasema HONGERA MWIJAKU KWA KUJENGA NYUMBA YA GOROFA KIGAMBONI, TENA SIO KIGAMBONI TUU NI KIGAMBONI KISOTA USHUANI, VIWANJA BEI YAKE YA MOTO SANA.

Mimi nimempongeza kwakua kafanya kitu kimeonekana, kwakua kazi zake za ubalozi WA Makampuni mbalimbali, deals za matangazo anazopata ukiachilia mbali ajira ya pale mawingu FM, mke ni CPA, muasibu wa moja ya bank hapa mjini kwanini asijenge??

Wabongo wenzangu Leo nawapa code:
Hata kama umesoma fungia vyeti kabatini, jitafute.

Mifano hii ikufikirishe uanze kujitafajari upya

*Mtoto WA Ruge ni Dj Tena msomi mzuri tuu lakini nani anamjua? Kwanini Udj haumtoi inavyotakiwa?! Halafu njoo Kwa mtoto WA mtwara miso misondo, Dogo misondo ukiachilia mbali ni RDJ EFM lakini Kila weekend anapiga kazi sana viwanja mbali mbali ndani na nnje ya dar Yani mzigo unaingia balaa, (Ubunifu, yeye kaja na wazee wa Makoti)

*Page za umbea ni nyingi sana Instagram, wanaokosoa serikali ni wengi sana Instagram, lakini Kuna mangekimambi app, Instagram ana followers Million 7 anawahamasisha walipie app wapate exclusive content, pia na Adult content anapost pia, ana subscribers zaid ya laki1 kwenye app yake wanalipia Kila mwezi Ili kuona umbea wa mastaa na sometimes videozao za uchi, kujiunga na app Kwa mwezi ni 2000
Hapo 2,000X100,000 Kwa mwezi anapata shingap? Ndio maana anakua na jeuri ya kununua umbea kuanzia laki5 kwenda mbele na anawalipa vijana wake mshahara mkubwa, kashajua kucheza na akili za wabongo

*Joti alishasemwa sana, Anti kiboga, anavaa nguo za kike na kua kama mwanamke, wengine wakasema anahamasisha ushoga, lakini Leo yule pale, aliweka aibu pembeni

Mifano ni mingi lakini kwakifupi watanzania wengi tunapenda vitu vya Kijinga kijinga, ukajua kucheza na akili za wabongo, ukaweka aibu pembeni mbona unatajirika tuu?! Njoo kwenye miziki ya bongo flava mingi inayowapa watu maisha ni ile ambayo watu wanaimba ngono, Kuna tofauti ya nyimbo za Mapenzi na nyimbo za Ngono.

Ni kukaa tuu chini kujitafuta, weka vyeti kabatini, angalia wabongo wanapenda Nini ishi nao, lakini kuchukia waliofanikiwa hakutafanya maisha yetu yawe mazuri au tupate ajira.

Pia tujue namna Bora ya kutumia mitandao ya kijamii kutupa maisha, Doto Magari mtoto wa mama kizimkazi nahapaipo, kimzaha mzaha huyu hapa anakuja, dalali maarufu hapa nchini kwasasa, anauza magari ya gharama Kwa udalali wake yadi mbalimbali za magari, kashakua balozi wa kampuni mbalimbali, kashapata deal GNM CARGO week iliopita alikua china, na jamaa unaambiwa alikua Teja tuu kinondoni pale anashusha udenda, Leo kipato chake ni kikubwa sana ambacho wasomi wengi hawana.

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
"A wealthy person can survive 6 months with the same lifestyle as before without adding income"
 
Toka watu washangae Mbowe kumiliki nyumba ya ghorofa moja tena mtu mzima yupo kwenye game ya kukusanya hela zaidi ya miaka 40 acha zile alizorithi kwa baba yake niliona sisi wabongo tuna tabu sana.

Ikiwa dalali tu wa magari anaweza akaunga unga akajenga nyumba ya Tsh 80 million huku sisi tunaofanya biashara za kuunga unga tena tuna miaka 30+ tunamiliki vibanda angalao vya 120 mill hao watashindwa nini?
 
Toka watu washangae Mbowe kumiliki nyumba ya ghorofa moja tena mtu mzima yupo kwenye game ya kukusanya hela zaidi ya miaka 40 acha zile alizorithi kwa baba yake niliona sisi wabongo tuna tabu sana.

Ikiwa dalali tu wa magari anaweza akaunga unga akajenga nyumba ya Tsh 80 million huku sisi tunaofanya biashara za kuunga unga tunamiliki vibanda angalao vya 120 mill hao watashindwa nini?
Nimeshangaa Sana
Ukiwa hustler smarter mil 500 kujenga nyumba nzuri ni jambo la kawaida pasipo hata kumuibia MTU au kumuhujumu MTU.
 
Toka watu washangae Mbowe kumiliki nyumba ya ghorofa moja tena mtu mzima yupo kwenye game ya kukusanya hela zaidi ya miaka 40 acha zile alizorithi kwa baba yake niliona sisi wabongo tuna tabu sana.

Ikiwa dalali tu wa magari anaweza akaunga unga akajenga nyumba ya Tsh 80 million huku sisi tunaofanya biashara za kuunga unga tunamiliki vibanda angalao vya 120 mill hao watashindwa nini?
Tatizo wabongo tunachukuliana poa sana

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu usihangaike nao sana,watu walioshindwa hutafuta njia za kujifariji ili kuhalalisha kushindwa kwao,

Unakuta mtu anatoa hukumu ya aibu kwa mwenzake tena bila ushahidi!

Wazowee tu mkuu ndio maisha waliyo yachagua.
 
Mkuu usihangaike nao sana,watu walioshindwa hutafuta njia za kujifariji ili kuhalalisha kushindwa kwao,

Unakuta mtu anatoa hukumu ya aibu kwa mwenzake tena bila ushahidi!

Wazowee tu mkuu ndio maisha waliyo yachagua.
Wivu mbaya sana, kukubali mtu amefanikiwa bila kumuonea wivu sijui tunakwama wapi wabongo

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Mbona ni jambo linalofahamika mkuu.
Sio kila mtu anaweza kua joti, miso misondo sijui mwijaku..

Na kila mtu ana namna yake ya kuona jambo, ukimwambia muislam auze kitimoto ili awe tajiri utapigwa mawe.

Vivyo hivyo kwa wengine hawawezi kua kin ant kiboga etc.

Njia za mafanikio ni nyingi, hili la mwijaku binafsi naona ni la kawaida ila tu wanazi wake mmeamua kulishikia bango.

Na hao uliowtataja hapo karibu wote wana hivyo vipaji.
Inyeshe mvua lije jua katu kuna watu labda ukiwemo na wewe hamuwezi kuifanya kazi anayoifanya.
Miso ni kipaji
Joti kipaji

Mnawananga sana wasomi wa nchi hii aisee.
 
Back
Top Bottom