Mtu anayechapa viboko ana matatizo gani

Mtu anayechapa viboko ana matatizo gani

bahati93

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
1,385
Reaction score
2,587
Habari ndugu zangu, kutokana na tukio lililotokea hivi karibuni nyanda za juu kusini la Vijana kupigwa bakora hadharani limenisukuma nitoe ufafanuzi hukusiana na tukio hilo.

Nitaeleza vitu vinavyosukuma fikra za mtu kutia maumivu katika mwili wa binadamu mwenzie na kutoa maelezo uhusiano baina ya bakora na utumwa.

Vyanzo ndani ya mtu anayechapa bakora
Mtu huyo ni muovu. Uovu ( evil) unatafririwa kama kukosa heshima kwa binadamu mwenzio, ndiko hupelekea mtu kutenda uovu kwa mwenzie.

Mtu anayejiona ni bora kuliko wengine na hivyo kupelekea kukosa heshima juu ya utu walionao wanyonge wake ( binadamu kama viumbe pekee walio na ufahamu yatupasa kuheshimiana kwa fursa pekee ambayo ulimwengu umetupatia )

Kukosa mlinganyo katika hisia (emotion sickness). Kuwa na hasira kupita kiasi ama chuki kupita kiasi, furaha kupita kiasi, hudhuni kupita kiasi ni baathi ya matatizo yanayomkabili.

Matatizo haya ya kihisia huwa yanatokana na malezi au nature ya mtu husika, endapo mtu alikulia katika mazingira ya kupigwa bakora, kutokupewa upendo, basi mtu huyu atakosa balance katika hisia hivyo kupelekea kufanya maamuzi mabovu kutokana na hisia zake za chuki kupita kiasi ( mtu mzima mwenye hisia za kitoto)

Kupata sababu kutekeleza chuki ( motive). Jambo la mwisho mtu muovu atakalo hitaji ni sabubu amboyo hata ikiwa ndogo kivipi ataijumuisha na mamuzi yake ya kutenda uovu, kwa case tuliyonayo kuwa na simu, kuchoma moto, kuvaa mlegezo

Haya tushamaliza na psychology behind mtu anapiga bakora Lakini hili jambo chanzo chake ni nini haswa, jibu linalopatikana ni kwamba WAKOLONI walikuja na hili jambo kama njia ya kutufunza mababu zetu kwani katika kipindi hicho WAKOLONI hawakuamini kama Wafrika ni binadamu ambao wanaupeo wa kuelewa jambo pasi kutumia bakora,( wakoloni hawatukupa heshima kama binamu their equal) walituchapa bakora kuonyesha msisitizo.

Sasa wakoloni washaondoka wametuacha tujitawale wenyewe, WAKOLONI washafuta bakora mashuleni kwao na hadi majumbani kwao, LAKINI kwanini sisi tunabaki kungangania mambo ya kale? ambayo hadi aliyetufundisha kupiga bakora ANATUOMBA tuache tabia hiyo!.

Wandugu tufikiri kwa pamoja, kadharauliana kama wanyama ni sahihii? Kushidwa kutumia akili na kutumia nguvu kutatatua shida zetu? Kuingilia majukumu ya kazi ambayo siyo yako ni sahii? Je ni sahihi kwa baba mlevi kupiga watoto wake akiwa kalewa?kuna utofauti gani ya kipigo halali na kipigo ambacho sio halali kwa watoji?

UTU NI JAMBO TUNU, TULIHESHIMU.
 
Me bila viboko ningeshafeli kitambo saana... Hivyo mfumo wetu wa elimu viboko ni lazima kwa sababu hatusomi on passion wala Talent. Cha mhimu ni kubadilisha Mfumo wa elimu ya Ukoloni na kuweka mfumo Updated ndo tuanze kufikilia kuondoa viboko
 
Usipotoshe umma mkuu bakora zitaendelea kuwepo tuacheni unafiki jamani wewe unataka kuniambia hujawahi kuchapwa? Haiwezekan kwa watoto wakibongo akue bila bakora unaweza ukakuza shoga
 
Usipotoshe umma mkuu bakora zitaendelea kuwepo tuacheni unafiki jamani wewe unataka kuniambia hujawahi kuchapwa? Haiwezekan kwa watoto wakibongo akue bila bakora unaweza ukakuza shoga
Kama umewahi chapwa haihalalishi n wengine wachapwe
 
afu mbona wa TZ tunaogopa sana ushoga??? Kwa kuogopa ndo kunafanya jambo hili liendelee yatupaswa kulielewa na sio kuliogopa
 
Kama Baba yako hajakuchapa ukiingia kwenye kumi na nane zetu unachezea Bakora mpaka uchakae.

Endelea kuongea hivyo lakini jihadhari kwenye kumi na nane zetu. Tunawasha mpaka roho ihisi kutoka.

Kenge wewe.
 
Kama Baba yako hajakuchapa ukiingia kwenye kumi na nane zetu unachezea Bakora mpaka uchakae.

Endelea kuongea hivyo lakini jihadhari kwenye kumi na nane zetu. Tunawasha mpaka roho ihisi kutoka.

Kenge wewe.
Hahahaaa mbuzi
Ila sio kosa lako shida ni kwamba mbongo yako inaukinzani na changee of time,
You on wrong side of history.
 
Hahahaaa mbuzi
Ila sio kosa lako shida ni kwamba mbongo yako inaukinzani na changee of time,
You on wrong side of history.


Ndio nakuambia hivyo Mkuu.
Jichanganye uone utakavyochakaa. Hakuna atakaye kuokoa kwenye mkono wangu. Watapiga tuu kelele lakini wewe utakuwa umekwenda na maji.

Karibi duniani Mkuu.
 
Usimnyime mtoto Viboko ni njia moja wapo ya kumrekebisha.
 
Usimnyime mtoto Viboko ni njia moja wapo ya kumrekebisha.
NO BIG NO,
kwanza jua kuwa mtoto ana akili za kitoto, kwa nini umwadhibu kwa kufanya makosa ambayo yapo nje ya uwezo wake?
Sijui kama unanielewa lakini!
Na pia huyo mtoto hakukuomba umzae, umemzaa mwenyewe kwa nini sasa una hasira nae?
Au ndugu huna msawazo wa emotions zako?
 
Jamaani hivi kweli mwashidwa kuona sisi wanadamu ni zaidi ya myama,
ingawa tuna nyama,
Hivyo yatupasa kujistili hulka zetu za kinyama,
 
Bora ya viboko kuliko upewe adhabu ya kulala na njaa na kesho yake uende shule.Viboko kuwepo au kutokuwepo inahitajika ufanyike utafiti mpana, sio majibu ya mihemko tunayotoa hapa,bahati mbaya sana Watanzania tunafanya maamuzi bila kufanya tafiti.
 
Back
Top Bottom