Raggy Singo
JF-Expert Member
- Dec 8, 2015
- 308
- 292
Mimi ni mwanamke mwenye miaka 33, naishi hapa Tanzania, mkoa naogopa kutaja. Nimeolewa na nimebahatika kuzaa watoto wawili katika ndoa yangu. Ila hapa siku za karibuni niliamua kuokoka na tumefundishwa kusema ukweli huko kanisani..
Sasa ukweli nilionao mimi ni kuhusu huyu mtoto wangu wa mwisho, sio wa mume wangu wa ndoa. Nilichepuka tu huko nje kwa ushawishi wa huyu jamaa maana nilijikuta nimevutiwa naye ghafla. Ila mimi kama mama najua ukweli huyu mtoto sio wa mume wangu, ila mume wangu anajua ni wake na pia hata yule baba wa mtoto naye hajui kama ni wake hii ni siri ambayo nimekuwa nayo toka muda sana..
Sasa kila nikienda kanisani nafsi inanisuta hata amani ya kusali inakosa najiuliza nimwambie ukweli mume wangu au niendelee kunyamaza. Kuhusu kunipenda mume wangu ananipenda na anipa kila kitu hadi gari alininunulia ni shetani tu alinipitia na kujikuta nafanya tukio hilo..
Naombeni ushauri ndugu zangu nifanyeje kuhusu hili
Kwa niaba.
Sasa ukweli nilionao mimi ni kuhusu huyu mtoto wangu wa mwisho, sio wa mume wangu wa ndoa. Nilichepuka tu huko nje kwa ushawishi wa huyu jamaa maana nilijikuta nimevutiwa naye ghafla. Ila mimi kama mama najua ukweli huyu mtoto sio wa mume wangu, ila mume wangu anajua ni wake na pia hata yule baba wa mtoto naye hajui kama ni wake hii ni siri ambayo nimekuwa nayo toka muda sana..
Sasa kila nikienda kanisani nafsi inanisuta hata amani ya kusali inakosa najiuliza nimwambie ukweli mume wangu au niendelee kunyamaza. Kuhusu kunipenda mume wangu ananipenda na anipa kila kitu hadi gari alininunulia ni shetani tu alinipitia na kujikuta nafanya tukio hilo..
Naombeni ushauri ndugu zangu nifanyeje kuhusu hili
Kwa niaba.