KING ASSENGA
JF-Expert Member
- Oct 8, 2016
- 929
- 1,500
Duuh, aisee!MTOTO WANGU ANA BABA WAWILI .
Kama hili ni kweli (jaribu kuhakiki) basi mtoto atakuwa ni wako.Japokuwa ananiaminisha sana na mtoto ana vingi anafanana na mimi zaidi
Are you serious or just kidding???Wakuu maisha yangu yamejaa mapito magumu sana ambayo kuwa sitarajii kabisa kukutana nayo kwenye maisha yangu.
mwaka juzi mwezi wa kumi tarehe 9 nilitoka mbeya na kurudi dar na kesho yake nilikutana kimwili na mwanamke ambaye tulikuwa na mahusiano kitambo . Baada ya kumaliza yaliyonileta dar nilirudi kwenye harakati za mikoani . Baada kama ya mwezi yule mwanamke aliniambia ameshika ujauzito mimi nilifurahi ila nikawa na wasiwasi huenda mimba sio yangu .
Nikamjulisha hilo akadai kuwa ni uhakika mimba ni yangu . Nikamjulisha basi kama mimba ni yangu lazima ajifungue tarehe 10 mwezi wa saba mwaka jana.
Na kweli alijifungua tarehe hiyo hiyo nilikuwa nisharudi dar na nilimhudumia vizuri tu japo sio kwa ukubwa ambao ningemhudumia kama nisingekuwa na mashaka.
Naomba niwajulishe zaidi kuhusu huyu mwanamke. Alikuwa na mtoto mmoja alizaa na jamaa mmoja . wakati nipo kwenye mahusiano nae nikiwa dar alikuwa kwa wazazi sikuwa nimepata taarifa kuwa tayari alienda kuishi na jamaa.
Sasa mwaka jana mwezi wa 12 nikawa nimepigiwa simu na namba ngeni nikapokea . Baada ya salamu jamaa akaniuliza unamfahamu Rose ( sio jina halisi)
Nikamjibu ndio namfahamu
Ninani kwako . Nikamjibu kwanini unaniuliza
Ndio akaniambia kuwa amekuwa akiona mawasiliano yangu na rose mda mrefu ila kuwa hajui kinachoendelea na muda mrefu anaishi na rose
Nikaamua kumuuliza mtoto wa mwisho niwa kwako akadai ni wake aisee?
Moyo ulishtuka sana ?
Ikabidi nimwambie ukweli kuwa ni mtoto wangu na nipo kwenye mahusiano na rose kitambo kumwaminisha zaidi ni cheti cha kuzaliwa cha mtoto ambacho kina jina langu na jina nililompa mtoto mimi
Japokuwa baadae niligundua nyumbani kuwa wanamwita jina jingine
Basi jamaa tulitulizana kiume na akadai kwenda kupima DNA ila jioni yake nikampigia akiwa na rose nikamwambia ampe simu rose aweke loud speaker aseme mtoto ni wanani ila rose aligoma katu , tukapanga tutakutana tuongee na jamaa
Ila akapotea moja kwa moja na alinyamaza.
Mahusiano yao yaliyumba akamwacha mwanamke mwenyewe mpaka sasa anafika mara chache sana na hahudumii kama awali na mimi vivyo hivyo nimepunguza sana kuhudumia.
Japokuwa ananiaminisha sana na mtoto ana vingi anafanana na mimi zaidi ila mashaka yapo . Hata wazazi wake aliwaambia mtoto Mtoto ni wangu ila bado hata nao siwaamini sijui nifanyeje moyo wangu uwe huru
Ni mtoto kike mzuri sana
Natamani sana hili likae vizuri
Kama ni mtoto wangu nimpe matunzo asilimia mia na nimweke moyoni nifurahie
Kama sio mwanangu basi ni move on.
Hili linaniumiza sana maana sina ujasiri wa kukemea malezi anayolelewa mwanangu na ningependa kuandaa future yake nimfungulie account mapema nianze kumwekea vishilingi lakini ndio hivyo nipo katikati
Mnanishauri nifanyeje wakuu??
Upo sawa mkuu.Kapime DNA upate uhakika, kwa wanawake wa sasa inawezekana hata nyie wote wawili mtoto sio wenu.
Nenda kapime DNA Na mtotoWakuu maisha yangu yamejaa mapito magumu sana ambayo kuwa sitarajii kabisa kukutana nayo kwenye maisha yangu.
mwaka juzi mwezi wa kumi tarehe 9 nilitoka mbeya na kurudi dar na kesho yake nilikutana kimwili na mwanamke ambaye tulikuwa na mahusiano kitambo . Baada ya kumaliza yaliyonileta dar nilirudi kwenye harakati za mikoani . Baada kama ya mwezi yule mwanamke aliniambia ameshika ujauzito mimi nilifurahi ila nikawa na wasiwasi huenda mimba sio yangu .
Nikamjulisha hilo akadai kuwa ni uhakika mimba ni yangu . Nikamjulisha basi kama mimba ni yangu lazima ajifungue tarehe 10 mwezi wa saba mwaka jana.
Na kweli alijifungua tarehe hiyo hiyo nilikuwa nisharudi dar na nilimhudumia vizuri tu japo sio kwa ukubwa ambao ningemhudumia kama nisingekuwa na mashaka.
Naomba niwajulishe zaidi kuhusu huyu mwanamke. Alikuwa na mtoto mmoja alizaa na jamaa mmoja . wakati nipo kwenye mahusiano nae nikiwa dar alikuwa kwa wazazi sikuwa nimepata taarifa kuwa tayari alienda kuishi na jamaa.
Sasa mwaka jana mwezi wa 12 nikawa nimepigiwa simu na namba ngeni nikapokea . Baada ya salamu jamaa akaniuliza unamfahamu Rose ( sio jina halisi)
Nikamjibu ndio namfahamu
Ninani kwako . Nikamjibu kwanini unaniuliza
Ndio akaniambia kuwa amekuwa akiona mawasiliano yangu na rose mda mrefu ila kuwa hajui kinachoendelea na muda mrefu anaishi na rose
Nikaamua kumuuliza mtoto wa mwisho niwa kwako akadai ni wake aisee?
Moyo ulishtuka sana ?
Ikabidi nimwambie ukweli kuwa ni mtoto wangu na nipo kwenye mahusiano na rose kitambo kumwaminisha zaidi ni cheti cha kuzaliwa cha mtoto ambacho kina jina langu na jina nililompa mtoto mimi
Japokuwa baadae niligundua nyumbani kuwa wanamwita jina jingine
Basi jamaa tulitulizana kiume na akadai kwenda kupima DNA ila jioni yake nikampigia akiwa na rose nikamwambia ampe simu rose aweke loud speaker aseme mtoto ni wanani ila rose aligoma katu , tukapanga tutakutana tuongee na jamaa
Ila akapotea moja kwa moja na alinyamaza.
Mahusiano yao yaliyumba akamwacha mwanamke mwenyewe mpaka sasa anafika mara chache sana na hahudumii kama awali na mimi vivyo hivyo nimepunguza sana kuhudumia.
Japokuwa ananiaminisha sana na mtoto ana vingi anafanana na mimi zaidi ila mashaka yapo . Hata wazazi wake aliwaambia mtoto Mtoto ni wangu ila bado hata nao siwaamini sijui nifanyeje moyo wangu uwe huru
Ni mtoto kike mzuri sana
Natamani sana hili likae vizuri
Kama ni mtoto wangu nimpe matunzo asilimia mia na nimweke moyoni nifurahie
Kama sio mwanangu basi ni move on.
Hili linaniumiza sana maana sina ujasiri wa kukemea malezi anayolelewa mwanangu na ningependa kuandaa future yake nimfungulie account mapema nianze kumwekea vishilingi lakini ndio hivyo nipo katikati
Mnanishauri nifanyeje wakuu??
Mzee wa kupambaniaAlikuwa na mtoto mmoja alizaa na jamaa mmoja .
Hii sitanii ni zaidi ya seriousAre you serious or just kidding???
Sijabaki nae japo nikitaka napewa nae jamaa anapewa just emaginePindi wanaume wawili mnapogundua mna mahusiano na mwanamke mmoja yule atakaebaki na huyo mwanamke ndo mwanaume dhaifu zaidi
Nawaza ilo ila laki tano inauma sana
SawaNawaza ilo ila laki tano inauma sana
Yakikukuta kama unapenda watoto aisee utateseka sanaBaba wawili tu unalialia, vipi ukijua na hao wengine?