Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,971
- 10,649
Mtoto wa miaka 5 akiwa katika dimbwi la maji
Waokoaji wakiutoa mwili wa mtoto kwenye dimbwi
Mtoto mwenye umri ya miaka 5 afariki dunia kwenye dimbwi la maji machafu karibu na mtaa wa stendi ya mabasi Mafinga, wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Mtoto huyo alipotea nyumbani takribani siku 3 zimepita ambapo mama mzazi alitoa taarifa jeshi la polisi liweze kumsaidia lakini juhudi hizo haikuzaa matunda ambapo hii leo amekutwa kwenye dimbwi la maji.
My take:
Huu ni uzembe wa hali ya juu kwa wahusika waliochimba hilo shimo,haiwezekani kuchimba dimbwi hilo alafu ushindwe kuweka tahadhari ikiwa pamoja na kuzungushia uzio eneo lote la dimbwi.
Usalama wa watoto wetu hapo sijui ukoje? Mtoto wa miaka mitano bado mdogo sana kuweza kuchukua tahadhari ya maafa hivyo kuepusha shari bora maeneo yote yenye hatari kuzungushiwa uzio ili kuweza kuokoa hawa malaika wetu.