Mtoto wa kambo

bikira mzee

Member
Joined
Apr 21, 2014
Posts
45
Reaction score
6
Mimi ni binti nilichelewa kidogo kuolewa nilipoolewa nilimkuta mume wangu na mtoto wa miaka saba,ambe bado alikua anaishi kwa mama yake alioolewa na mtu mwingine.baada yakufunga ndoa tu tulifanya taratibu zakumchukua kwa mama yake aliekua akihudumiwa yeye na mtoto toka mimba.

Chakushangaza mtoto tulilupa nursery ya english medium lakini tulikuja kugundua hasomi huko tunapolipa fedha anasoma shule ya hapo hapo mtaani kwao.toka kuzaliwa mumewangu alikua akinyimwa kumuona mtoto mara kwa mara licha ya kumuhudumia.siku waliotupa mtoto walitupa akiwa uchi na mwenye afya duni.

Nimejitahidi kama mama kurekebisha afya ya mtoto nakumuombea kwa Mungu .

Hasalimii mtu akisema sijawazoea.anazungumza maneno magum kiasi kwamba nakufa moyo wakumpenda nimemchapa ilipobidi sijawahi kumuonea.

Amekua akienda kwa mama yake kusalimia naakirudi anarudi na mambo ya ajabu kuliko mwanzo,nampenda mume wangu namhurumia kwani anaumia sana juu ya jambo la mtoto .

Mama mtoto hajawahi hata nipigia simu hatakunisalimia wala hatakujua mtoto analala wapi na anaishije.nifanyaje wanajamii sitakikufanya roho mbaya japo naumia
 
Pole wakati mwingine kulea mtoto si wa kambo tu hata wa ndugu ambae kwa namna moja ama nyingine labda mzazi wake ana hali ngumu huwa ni kazi, kuna wa mama wengine huwajenga watoto katika pozi la kumchukia mama wa kambo mpaka baba na ndio maana wakati mwingine ni vyema kama tatizo limetokea mwanaume umezaa nje ukamchukua mtoto mapema na kukaa nae kwako pia na mnakaa na huyo mliezaa nae na kuweka mkakati wa pamoja wa nini mtoto hapaswi kuambiwa lakini kila mtu akichukulia hasira matokeo yake ndio hayo akienda kwa mama analishwa sumu akija kwako ukimkanya kidogo itaonekana kwa kuwa sio mwanao. Hapo huyo mumeo anatakiwa aongee na mzazi mwenzake na kumweleza kila kitu kinachotokea pia amwombe ampe maneno mazuri ya busara huyo mtoto ili muweze kukaa nae vizuri lakini hata mfanye nini kama mama yake mcharuko mtaendelea kupata shida.
 
Dah!
Pole sana dada yangu,hayo ni ya kawaida kabisa kwenye maisha ya ndoa

Kuna jambo naliona hapo,jambo lenyewe ni muda wa huyo mtoto kuzoea na kuamini kuwa wewe unaweza kuwa ni mama yake na utaweza kumpenda kama mama yake mzazi

Nachokushauri hebu jaribu kumshauri baba yake amzuie kwenda huko kwa mama yake kwa muda kama wa miezi miwili halafu uone maendeleo yake yanakuwaje

Kama utaona anabadilika mwambie mumeo mumzuie kabisa kwenda kwa mama yake kwa muda wa kutosha kwa huyo mtoto kusahahu kabisa anayokuwa anakutana nayo huko kwa mama yake na ikiwezekana asiende kabisa

Suala la huyo mama kutokuwasiliana na wewe achana nalo kwani kuna watu wengine kizuri kwao ni kibaya

Cha kuzingatia ni usalama wa mtoto na mumeo basi

Ukiambiwa kukua ni kuona mengi sio maghorofa ya kariakoo bali ni hayo unayokuitana nayo!
 
Unataka ushukuriwe na mke mwenzio? Una kiranga weye. Jadilianeni na mmeo mjilue way foward, mtoto wa miaka 7 mdogo sana.
 
simama na Mungu, yatatokea mengi ya kukera kuumiza moyo na kukatisha lakini tenda mema tu USIACHE, mwisho ushindi utakuwa kwako
 
rafiki ilikua mtoto achukuliwe mapema mama alikataa kwakisingizio cha mtoto kutesrka chaajabu familia ya mume wangu siombaya na wanakaa na watoto yatima wengi tu
baadae mama alupobanwa akasema yeye hanakazi hivyo matumizi ya mtoto tunayotuma yanamsaidia hivyo hawezi kumuachia nilimtumia mtaji kama sh laki4 ili aanze biashara ndogondogo lakini wapi aliila na kuishia kufanya arobaini ya mama yake
 
pole sana ila huyo mwanamke aliyezaa nae anakuonea wivu sana na ndio maana anamjaza mtoto upumbavu ili aivuruge ndoa yenu, jitahidi kuongea na mzee wako kuhusu kuwa mtoto asiende ende sana kwa mama kwani wewe upo au kuwe na uangalizi wa kina anapoenda huko ili kuepusha kumjaza mambo yasiyofaa, hata hivyo Mungu awe mbele kwani anaweza hata kukuloga ili uachike
 
Mpelekeni boarding atabadilika
 
kwanza wewe sio binti, wewe ni mke! majina yako bana, bikira mzee, binti, kama mama nk! jitambue! adha ya mapenzi kabla na nje ya ndoa ndo product zake. nakuambia tu hilo mama unalo inabidi uvae roho ya uvumilivu na muda si mrefu mme wako naye atakuwa upande wa motto! lol! uwe unatupa updates
 
Mpelekeni boarding atabadilika
Boarding ni suruhisho la muda mkuu maana likizo lazima arudi na kulianzisha upya yaani kama vile mtu yupo kwenye matatizo makubwa alafu anajipoza na pombe alafu baadae ikitoka kichwani mambo ni yaleyale, kazi kubwa inachotakiwa ni kumjenga aweze kujitambua na aelewe kwamba hayo ndio aina ya maisha anapaswa kuishi kutokana na mzazi mwingine kuwa ameolewa na mwingine ameoa mke mwingine. Baada ya zoezi hilo kueleweka ndipo suala la boarding lifuate huku akirudi likizo anakwenda kwa mama yake siku kadhaa na kwa baba yake siku kadhaa then likizo ikiisha anakwenda shule. Hapo huyo mama yake mzazi ndio ndio kikwazo kama ni project mlengwa wa kwanza ni mama mzazi wa mtoto (anatakiwa abadilike) alafu then mtoto maana watoto hata watu wazima tu huwasikiliza sana mama zao
 
Maana yangu ni kuwa akienda boarding angalau huyu dada atapumzika kiasi fulani. Kukaana mtoto wa aina hiyo 24:7 inachochosha, na inapoteza malovre ndani ya nyumba. Kule shule atajichanganya na wenzake, kwanza atakua kiakili. Ilishanitokea mimi na ikafanya kazi. Pia msimamo wa baba ndio unaweza kujenga au kubomoa nyumba
 
wanajamii boding nilifikiria ila mtt mdogo huyu hajui upendo wa familia bado ,hapendi shule kabisa nikimpeleka uko nani atamsimamia?nikiangalia atakua ndugu wa watoto wangu nisipomkazania leo atakua mzigo kwa wenzie badala yakua msaada cha ajabu zaidi anaemdai mtt mara kwa mara ni baba wa kambo kuliko hata mama.
 
Jicho wote tunaelewa sera ya humu.hayonimajina tu.najitahid huu ni mtihani geuzia kwako uone kisha nisaidie mawazo ,kiuhalisia kuhamia kwa mtoto sio rahisi mama ndio mtoa huduma kati yao wote inahitajika huruma ya kiMungu tu.huyu mtt awe kama wengine
 
Hapa mabazazi wanatakiwa watoe ushauri aisee ,mnawatesa watoto za watu mkija kuoa na haao watoto wenu wa outdoors
 
umejitoa ubazazini?

mleta mada..usichoke...wewe na mumeo wote inabidi mshirikiane..miaka saba bado mdogo...kama akienda kwa mama yake anarudi na tabia mbaya kuliko mwanzo,acheni kumpeleka....muda wa kumkunja samaki huyu ni sasa
Hapa mabazazi wanatakiwa
watoe ushauri aisee ,mnawatesa watoto za watu mkija kuoa na haao watoto
wenu wa outdoors
 
daah inakumba weng hilo, na ni mtihan jaman labda jaribun kumpeleka kwa bibi yake mzaa baba akakae huko kwanza..
 
mwanaume mwenye mtoto nje huwa namuangalia kwa jicho la tatu. jitahidi tu kumtreat kama mtoto wako, mtoto akinyea kiganja huwezi kukikata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…